Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Chroniques 30.11
Bible en Swahili de l’est


Célébration de la Pâque

1 Hezekia akatuma wajumbe kwa Israeli wote na Yuda pia; akawaandikia nyaraka Efraimu na Manase, waje nyumbani kwa Bwana Yerusalemu, ili wamfanyie pasaka Bwana, Mungu wa Israeli.
2 Chroniques 30.10-30.11 1 Corinthiens 5.7-5.8 2 Chroniques 25.7 Exode 12.3-12.20 2 Chroniques 35.6
2 Kwa maana mfalme na wakuu wake, na kusanyiko lote katika Yerusalemu walifanya shauri kufanya pasaka mwezi wa pili.
Nombres 9.10-9.11 1 Chroniques 13.1-13.3 2 Chroniques 30.15 Ecclésiaste 4.13 Proverbes 15.22
3 Kwa sababu hawakuweza kuifanya wakati ule, kwa kuwa makuhani walikuwa hawajajitakasa wa kutosha, wala watu hawajakusanyika huko Yerusalemu.
2 Chroniques 29.34 Exode 12.6 Exode 12.18 2 Chroniques 29.17
4 Likawa neno jema machoni pa mfalme, na kusanyiko lote.
1 Chroniques 13.4
5 Basi wakafanya amri kupiga mbiu kati ya Israeli yote, toka Beer-sheba mpaka Dani, ya kwamba watu waje wamfanyie pasaka Bwana, Mungu wa Israeli, huko Yerusalemu; maana tangu siku nyingi hawakuifanya kama vile ilivyoandikwa.
Juges 20.1 2 Chroniques 36.22 Lévitique 23.2 Esther 3.12-3.15 Esdras 6.8-6.12
6 Wakaenda matarishi wenye nyaraka za mfalme na wakuu wake, kati ya Israeli yote na Yuda, na kwa amri ya mfalme, kusema, Enyi wana wa Israeli, mrudieni Bwana, Mungu wa Ibrahimu, na Isaka, na Israeli, apate kuwarudia waliosalia wenu waliookoka mikononi mwa wafalme wa Ashuru.
Esther 8.14 Jérémie 51.31 2 Rois 15.29 Job 9.25 Jérémie 4.1
7 Wala msiwe kama baba zenu, na kama ndugu zenu, waliomwasi Bwana, Mungu wa baba zao, hata akawatoa kuwa ushangao, kama mwonavyo.
2 Chroniques 29.8 Ezéchiel 20.13-20.18 Zacharie 1.3-1.4
8 Msiwe sasa wenye shingo ngumu kama baba zenu; lakini mjitoe kwa Bwana, mkaingie katika patakatifu pake, alipopatakasa milele, mkamtumikie Bwana, Mungu wenu, hasira yake kali iwageukie mbali.
Exode 32.9 2 Chroniques 29.10 Deutéronome 10.16 Romains 6.22 Psaumes 63.2
9 Kwa kuwa mkimrudia Bwana, ndugu zenu na watoto wenu watahurumiwa machoni pa hao waliowachukua mateka, nao watairudia nchi hii; kwa kuwa Bwana, Mungu wenu, ndiye mwenye neema, na mwenye rehema, wala hatawageuzia mbali uso wake, mkimrudia.
Psaumes 106.46 Michée 7.18 1 Rois 8.50 Exode 34.6-34.7 Esaïe 55.7
10 Basi matarishi wakapita mji kwa mji kati ya nchi ya Efraimu na Manase, hata kufika Zabuloni; lakini waliwacheka-cheka, na kuwadhihaki.
2 Chroniques 36.16 2 Chroniques 30.6 Job 9.25 Luc 16.14 Esther 3.15
11 Ila watu wengine wa Asheri, na wa Manase, na wa Zabuloni walijinyenyekeza, wakaja Yerusalemu.
2 Chroniques 30.21 2 Chroniques 30.18 2 Chroniques 30.25 Luc 14.11 2 Chroniques 33.19
12 Tena katika Yuda mkono wa Mungu ulikuwa ukiwapa moyo mmoja, waitimize amri ya mfalme na wakuu kwa neno la Bwana.
Philippiens 2.13 Jérémie 32.39 Ezéchiel 36.26 Psaumes 110.3 Deutéronome 4.2
13 Basi wakakusanyika Yerusalemu watu wengi ili kuifanya sikukuu ya mikate isiyochachwa katika mwezi wa pili, kusanyiko kuu sana.
Psaumes 84.7 2 Chroniques 30.2
14 Wakainuka, wakaziondoa madhabahu zilizokuwamo Yerusalemu, nazo madhabahu za kufukizia wakaziondoa, wakazitupa katika kijito Kidroni.
2 Chroniques 28.24 2 Chroniques 15.16 2 Chroniques 29.16 2 Samuel 15.23 2 Rois 18.22
15 Kisha wakaichinja pasaka siku ya kumi na nne ya mwezi wa pili, nao makuhani na Walawi wakatahayarika, wakajitakasa, wakaleta sadaka za kuteketezwa nyumbani mwa Bwana.
2 Chroniques 29.34 Exode 19.10 2 Chroniques 29.15 Ezéchiel 16.61-16.63 Exode 19.22
16 Wakasimama mahali pao kwa taratibu yao, sawasawa na torati ya Musa, mtu wa Mungu; nao makuhani wakainyunyiza damu, waliyoipokea mikononi mwa Walawi.
Deutéronome 33.1 2 Chroniques 35.15 Hébreux 11.28 2 Rois 11.14 2 Chroniques 35.10-35.11
17 Kwa maana kulikuwa na wengi katika kusanyiko ambao hawajajitakasa; kwa hiyo Walawi wakamchinjia pasaka, kila mtu asiyekuwa safi, ili kuwatakasa kwa Bwana.
2 Chroniques 29.34 Exode 12.6 2 Chroniques 35.3-35.6
18 Kwani wingi wa watu, naam, wengi wa Efraimu, na wa Manase, na wa Isakari, na wa Zabuloni, hawakujisafisha, lakini wakala pasaka, ila si kama ilivyoandikwa. Naye Hezekia alikuwa amewaombea, akisema, Bwana mwema na amsamehe kila mtu,
Psaumes 25.8 Exode 12.43-12.51 1 Jean 5.16 Psaumes 86.5 Daniel 9.19
19 aukazaye moyo wake kumtafuta Mungu, Bwana, Mungu wa babaze, hata ikiwa si kwa utakaso wa patakatifu.
2 Chroniques 19.3 2 Chroniques 20.33 Psaumes 10.17 Nombres 19.13-19.20 1 Samuel 7.3
20 Bwana akamsikia Hezekia, akawaponya watu.
Psaumes 103.3 Exode 15.26 Jacques 5.15-5.16
21 Nao wana wa Israeli waliohudhuria Yerusalemu wakafanya sikukuu ya mikate isiyochachwa siku saba kwa furaha kubwa; Walawi na makuhani wakamsifu Bwana siku kwa siku, wakimwimbia Bwana kwa vinanda vyenye sauti kuu.
Exode 12.15 Exode 13.6 2 Chroniques 20.21 Deutéronome 12.12 2 Chroniques 7.10
22 Hezekia akawafurahisha mioyo Walawi wote waliokuwa wastadi wa kumtumikia Bwana. Basi muda wa siku saba wakala sikukuu, wakitoa dhabihu za sadaka za amani, na kumtolea shukrani Bwana, Mungu wa baba zao.
Néhémie 9.3 2 Chroniques 32.6 Esdras 10.11 2 Chroniques 17.9 Néhémie 8.7-8.8
23 Na kusanyiko lote wakafanya shauri kufanya sikukuu siku saba nyingine; wakafanya sikukuu siku saba nyingine kwa furaha.
1 Rois 8.65 2 Chroniques 7.9
24 Maana Hezekia, mfalme wa Yuda, aliwatolea kusanyiko matoleo ya ng’ombe elfu, na kondoo elfu saba; na wakuu wakawatolea kusanyiko ng’ombe elfu, na kondoo elfu kumi; tena wakajitakasa makuhani wengi sana.
2 Chroniques 29.34 2 Chroniques 35.7-35.8 1 Chroniques 29.3-29.9 Ezéchiel 45.17 Ephésiens 4.8
25 Na kusanyiko lote la Yuda, pamoja na makuhani na Walawi, na kusanyiko lote waliotoka Israeli, na wageni waliotoka katika nchi ya Israeli, nao waliokaa Yuda, wakafurahi.
2 Chroniques 30.11 2 Chroniques 30.18 1 Chroniques 16.10-16.11 Exode 12.43-12.49 Psaumes 104.34
26 Ikawa furaha kuu katika Yerusalemu; kwa sababu tangu siku za Sulemani mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli, hayajakuwako mambo kama hayo huko Yerusalemu.
2 Chroniques 7.8-7.10
27 Ndipo wakasimama makuhani Walawi, wakawabariki watu; ikasikiwa sauti yao, sala yao ikafika hata makao yake matakatifu, yaani, mbinguni.
Psaumes 68.5 Deutéronome 26.15 2 Chroniques 23.18 Nombres 6.23-6.26 Esaïe 66.1

Cette Bible est dans le domaine public.