Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Chroniques 12.8
Bible en Swahili de l’est


Invasion de Juda

1 Ikawa ulipothibitika ufalme wa Rehoboamu, naye amepata nguvu, aliiacha torati ya Bwana, na Israeli wote pamoja naye.
2 Chroniques 11.17 2 Chroniques 12.13 2 Chroniques 26.13-26.16 1 Rois 14.22-14.24 Michée 6.16
2 Ikawa katika mwaka wa tano wa mfalme Rehoboamu, akapanda Shishaki, mfalme wa Misri, juu ya Yerusalemu; kwa kuwa walikuwa wamemwasi Bwana;
1 Rois 11.40 Néhémie 9.26-9.27 Jérémie 44.22-44.23 Lamentations 5.15 Psaumes 106.43-106.44
3 mwenye magari elfu moja na mia mbili, na wapanda farasi sitini elfu; na watu wasiohesabika, waliotoka Misri pamoja naye; Walubi, na Wasukii, na Wakushi.
2 Chroniques 16.8 Nahum 3.9 Daniel 11.43 Apocalypse 9.16 1 Samuel 13.5
4 Akaitwaa miji yenye maboma iliyokuwa ya Yuda, akaja Yerusalemu.
2 Chroniques 11.5-11.12 Esaïe 36.1 Esaïe 10.11 2 Rois 18.17 Jérémie 5.10
5 Ndipo akaja Shemaya nabii kwa Rehoboamu, na kwa wakuu wa Yuda, waliokusanyika Yerusalemu kwa sababu ya Shishaki, akawaambia, Bwana asema hivi, Ninyi mmeniacha mimi, kwa hiyo nami nimewaacha ninyi mkononi mwa Shishaki.
2 Chroniques 15.2 2 Chroniques 11.2 1 Rois 12.22 2 Samuel 24.14 Jérémie 2.19
6 Ndipo wakajinyenyekeza wakuu wa Israeli na mfalme; wakasema, Bwana ndiye mwenye haki.
Exode 9.27 Daniel 9.14 Jérémie 13.15 Luc 18.14 Exode 10.3
7 Naye Bwana alipoona ya kwamba wamejinyenyekeza, neno la Bwana likamjia Shemaya, kusema, Wamejinyenyekeza; sitawaharibu; lakini nitawapa wokovu punde, wala ghadhabu yangu haitamwagika juu ya Yerusalemu kwa mkono wa Shishaki.
2 Chroniques 34.25 Psaumes 79.6 Apocalypse 14.10 Luc 15.18-15.21 2 Rois 13.4-13.7
8 Walakini watamtumikia; ili wapate kujua utumwa wangu, na huo utumwa wa falme za nchi.
Esaïe 26.13 Deutéronome 28.47-28.48 Osée 8.10 Néhémie 9.36 Juges 3.1
9 Basi Shishaki, mfalme wa Misri, akapanda juu ya Yerusalemu, akazichukua hazina za nyumba ya Bwana, na hazina za nyumba ya mfalme; akazichukua zote. Akazichukua pia ngao za dhahabu alizozifanya Sulemani.
2 Chroniques 9.15-9.16 1 Rois 10.16-10.17 Lamentations 1.10 1 Rois 14.25-14.28 1 Rois 15.18
10 Mfalme Rehoboamu akafanya ngao za shaba mahali pake, akawakabidhi wakuu wa walinzi, waliongoja mlangoni pa nyumba ya mfalme.
Lamentations 4.1 Cantique 3.7-3.8 1 Rois 14.27 2 Samuel 8.18 1 Chroniques 11.25
11 Ikawa kila wakati mfalme alipoingia nyumbani mwa Bwana, wakaja walinzi wakazichukua, wakazirudisha tena chumbani mwa walinzi.
12 Naye alipojinyenyekeza, ghadhabu ya Bwana ikamgeukia mbali, asimharibu kabisa; tena yalionekana katika Yuda mambo mema.
2 Chroniques 19.3 2 Chroniques 12.6-12.7 1 Rois 14.13 Esaïe 57.15 1 Pierre 5.6
13 Basi mfalme Rehoboamu akajitia nguvu katika Yerusalemu, akatawala; maana Rehoboamu alikuwa na umri wa miaka arobaini na mmoja alipoanza kutawala, akatawala miaka kumi na saba huko Yerusalemu, mji aliouchagua Bwana miongoni mwa kabila zote za Israeli, ili aliweke huko jina lake. Na jina la mamaye aliitwa Naama Mwamoni.
1 Rois 14.21 Deutéronome 12.5 2 Chroniques 6.6 Exode 20.24 Néhémie 13.26
14 Naye akatenda yaliyo maovu, kwa kuwa hakuukaza moyo wake amtafute Bwana.
2 Chroniques 19.3 Matthieu 7.7 Esaïe 45.19 1 Corinthiens 16.13 Ezéchiel 33.31
15 Basi mambo yake Rehoboamu, ya kwanza na ya mwisho, je! Hayakuandikwa katika tarehe za Shemaya nabii na Ido mwonaji, kwa jinsi ya kuandika nasaba? Kulikuwa na vita kati ya Rehoboamu na Yeroboamu siku zote.
2 Chroniques 9.29 2 Chroniques 12.5 1 Rois 12.22 2 Chroniques 13.22 1 Rois 14.29-14.30
16 Rehoboamu akalala na babaze, akazikwa katika mji wa Daudi. Na Abiya mwanawe alitawala mahali pake.
Matthieu 1.7 2 Chroniques 13.1 1 Chroniques 3.10 2 Chroniques 11.20 1 Rois 14.29-14.31

Cette Bible est dans le domaine public.