Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Chroniques 28.5
Bible en Swahili de l’est


Instructions de David pour la construction du temple

1 Kisha Daudi akawakusanya huko Yerusalemu wakuu wote wa Israeli, wakuu wa kabila, na maakida wa vikosi wenye kumtumikia mfalme kwa zamu, na maakida wa maelfu, na maakida wa mamia, na wenye kutawala juu ya mali na milki za mfalme, na za wanawe, pamoja na matowashi, na mashujaa, naam, waume mashujaa wote.
1 Chroniques 11.10-11.47 1 Chroniques 23.2 1 Chroniques 27.1-27.34 Josué 24.1 Josué 23.2
2 Ndipo Daudi mfalme akasimama kwa miguu yake, akasema, Nisikilizeni, ndugu zangu, na watu wangu; Mimi nalikuwa na nia ya kuijenga nyumba ya kustarehe kwa ajili ya sanduku la agano la Bwana, na kiti cha kuwekea miguu yake cha Mungu wetu; hata nalikuwa nimeweka tayari kwa kujenga.
Esaïe 66.1 Psaumes 99.5 Lamentations 2.1 1 Chroniques 17.1-17.2 2 Samuel 7.1-7.2
3 Lakini Mungu akaniambia, Wewe hutajenga nyumba kwa ajili ya jina langu, kwa sababu umekuwa mtu wa vita, nawe umemwaga damu.
1 Chroniques 22.8 1 Rois 5.3 1 Chroniques 17.4 2 Samuel 7.5-7.13 2 Chroniques 6.8-6.9
4 Walakini Bwana, Mungu wa Israeli, alinichagua katika nyumba yote ya babangu kuwa mfalme juu ya Israeli milele, kwa kuwa amemchagua Yuda awe mkuu; na katika nyumba ya Yuda, alichagua nyumba ya babangu, na miongoni mwa wana wa babangu, aliniridhia mimi ili kunitawaza niwe mfalme juu ya Israeli wote;
1 Chroniques 5.2 1 Samuel 16.1 1 Samuel 16.6-16.13 Genèse 49.8-49.10 1 Chroniques 17.27
5 tena katika wana wangu wote (kwani Bwana amenipa wana wengi), amemchagua Sulemani mwanangu ili aketi juu ya kiti cha enzi cha ufalme wa Bwana, juu ya Israeli.
1 Chroniques 23.1 1 Chroniques 3.1-3.9 1 Chroniques 22.9-22.10 2 Chroniques 1.8-1.9 1 Chroniques 29.23
6 Akaniambia, Sulemani, mwanao, ndiye atakayeijenga nyumba yangu na nyua zangu; kwa kuwa nimemchagua awe mwanangu, nami nitakuwa babaye.
2 Samuel 7.13-7.14 1 Chroniques 22.9-22.10 1 Chroniques 17.11-17.14 Hébreux 3.6 Hébreux 3.3
7 Na ufalme wake nitauweka imara milele, akijitia kwa bidii kuzitenda amri zangu na hukumu zangu, kama hivi leo.
1 Chroniques 22.13 Psaumes 89.28-89.37 1 Rois 9.4-9.5 1 Chroniques 28.10 Josué 1.6-1.7
8 Basi sasa, machoni pa Israeli wote, hilo kusanyiko la Bwana, na masikioni pa Mungu wetu, angalieni na kuzitafuta amri zote za Bwana, Mungu wenu, ili mpate kuimiliki nchi hii njema, na kuwarithisha wana wenu baada yenu hata milele.
Deutéronome 4.1 Proverbes 13.22 Deutéronome 29.10 Actes 10.33 Hébreux 12.1-12.2
9 Nawe, Sulemani mwanangu, mjue Mungu wa baba yako, ukamtumikie kwa moyo mkamilifu, na kwa nia ya kumkubali; kwa kuwa Bwana hutafuta-tafuta mioyo yote, na kuyatambua mawazo yote ya fikira; ukimtafuta, ataonekana nawe; ukimwacha, atakutupa milele.
Jérémie 29.13 1 Rois 8.61 Jacques 4.8-4.11 1 Samuel 16.7 2 Chroniques 15.2
10 Jihadhari basi; kwani Bwana amekuchagua wewe ili ujenge nyumba itakayokuwa mahali patakatifu; uwe hodari ukatende hivyo.
1 Chroniques 28.6 1 Chroniques 22.16-22.19 1 Timothée 4.16
11 Ndipo Daudi akampa Sulemani mwanawe mfano wa ukumbi wa hekalu, na nyumba zake, na hazina zake, na orofa zake, na vyumba vyake vya ndani, na mahali pa kiti cha rehema;
1 Chroniques 28.19 1 Rois 6.3 Exode 25.40 Hébreux 8.5 Exode 25.17-25.22
12 na mfano wa yote aliyokuwa nayo kwa roho, katika habari ya nyua za nyumba ya Bwana, na ya vyumba vyote vilivyoizunguka, ya hazina za nyumba ya Mungu, na ya hazina za vitu vilivyowekwa wakfu;
1 Chroniques 26.20 1 Rois 14.26 2 Rois 16.8 1 Rois 15.18 1 Chroniques 26.26-26.28
13 tena katika habari ya zamu za makuhani na Walawi, na ya kazi yote ya huo utumishi wa nyumba ya Bwana, na ya vyombo vyote vya utumishi nyumbani mwa Bwana;
1 Chroniques 24.1-24.19 Esdras 8.25-8.30 1 Chroniques 9.29 Esdras 8.33 1 Chroniques 23.6
14 ya dhahabu kwa uzani kwa vyombo vya dhahabu, kwa vyombo vyote vya utumishi wa kila namna; ya fedha kwa uzani kwa vyombo vyote vya fedha, kwa vyombo vyote vya utumishi wa kila namna;
15 kwa uzani tena kwa vinara vya dhahabu, na kwa taa zake za dhahabu, kwa uzani, kwa kila kinara, na kwa taa zake; na kwa vinara vya fedha, kwa uzani kwa kila kinara na kwa taa zake, kwa kadiri ya matumizi ya kila kinara;
Exode 25.31-25.39 Zacharie 4.11-4.14 Apocalypse 1.12-1.13 Apocalypse 1.20-2.1 2 Chroniques 4.7
16 na dhahabu kwa uzani kwa meza za mikate ya wonyesho, kwa kila meza; na fedha kwa meza za fedha;
Exode 25.23-25.30 2 Chroniques 4.8 1 Rois 7.48 2 Chroniques 4.19
17 na nyuma, na mabakuli, na vikombe vya dhahabu safi; na kwa matasa ya dhahabu, kwa uzani kwa kila tasa; na kwa matasa ya fedha, kwa uzani kwa kila tasa;
Nombres 7.13-7.14 1 Rois 10.21 1 Samuel 2.13-2.14 2 Chroniques 4.20-4.22 1 Rois 7.48-7.50
18 na kwa madhabahu ya kufukizia, dhahabu iliyosafika sana kwa uzani; na dhahabu kwa mfano wa gari, yaani, makerubi, yenye kutandaza mabawa, na kulifunika sanduku la agano la Bwana.
Exode 25.18-25.22 Exode 30.1-30.10 Ezéchiel 10.2-10.22 Psaumes 68.17 1 Rois 6.23-6.30
19 Hayo yote, akasema Daudi, yamenielea kwa maandiko kutoka kwa mkono wa Bwana, naam, kazi zote za mfano huu.
Exode 25.40 1 Chroniques 28.11-28.12 Ezéchiel 1.3 Ezéchiel 3.14 Exode 26.30
20 Kisha Daudi akamwambia Sulemani mwanawe, Uwe hodari, mwenye moyo mkuu, ukatende hivyo; usiogope wala usifadhaike; kwa kuwa Bwana, Mungu, Mungu wangu, yu pamoja nawe; yeye hatakupungukia wala kukuacha, hata itakapomalizika kazi yote ya huo utumishi wa nyumba ya Bwana.
1 Chroniques 22.13 Hébreux 13.5 Psaumes 27.1-27.2 Esaïe 41.13 1 Corinthiens 16.13
21 Na tazama, hizo zamu za makuhani na Walawi ziko, kwa utumishi wote wa nyumba ya Mungu; nao watakuwapo pamoja nawe kwa kazi ya kila namna, kila mtu mwenye hiari, aliye stadi kwa utumishi wo wote; tena maakida na watu wote watakuwa chini ya amri yako kabisa.
1 Chroniques 24.1-24.26 Exode 35.25-36.4 Romains 13.1 Exode 31.3 Psaumes 110.3

Cette Bible est dans le domaine public.