Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Rois 9.20
Bible en Swahili de l’est


Accession de Jéhu au trône d’Israël

1 Nabii Elisha akamwita mmojawapo wa wana wa manabii, akamwambia, Jikaze viuno, ukachukue chupa hii ya mafuta mkononi mwako, ukaende Ramoth-Gileadi.
1 Samuel 10.1 2 Rois 4.29 1 Samuel 16.1 1 Rois 1.39 2 Rois 8.28-8.29
2 Utakapofika huko, mtafute Yehu, mwana wa Yehoshafati, mwana wa Nimshi, ukaingie, ukamtoe miongoni mwa ndugu zake, ukamchukue katika chumba cha ndani.
2 Rois 9.14 2 Rois 9.5 2 Rois 9.11 1 Rois 19.16-19.17 1 Rois 22.25
3 Kisha, ukatwae ile chupa ya mafuta, ukayamimine juu ya kichwa chake, ukaseme, Bwana asema hivi, Nimekutia mafuta uwe mfalme juu ya Israeli. Kisha ufungue mlango ukakimbie, wala usikawie.
1 Rois 19.16 1 Samuel 15.17 Psaumes 75.6-75.7 1 Samuel 16.2 Proverbes 8.15-8.16
4 Basi yule kijana, yule nabii kijana, akaenda Ramoth-Gileadi.
5 Naye alipofika, tazama, majemadari wa jeshi walikuwa wamekaa; naye akasema, Nimetumwa na neno kwako, Ee jemadari; Yehu akasema, Kwa yupi miongoni mwetu sote? Akasema, Kwako wewe, Ee jemadari.
Juges 3.19
6 Akainuka akaingia nyumbani; naye akayamimina yale mafuta kichwani mwake, akamwambia, Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Nimekutia mafuta uwe mfalme juu ya watu wa Bwana, yaani, juu ya Israeli.
1 Rois 19.16 2 Chroniques 22.7 2 Rois 9.3 1 Rois 1.34 Actes 23.18-23.19
7 Nawe utawapiga nyumba ya Ahabu, bwana wako, ili nijilipize kisasi cha damu ya watumishi wangu manabii, na damu ya watumishi wote wa Bwana, mkononi mwa Yezebeli.
1 Rois 21.15 1 Rois 18.4 Deutéronome 32.43 1 Rois 21.25 2 Rois 9.32-9.37
8 Kwa maana nyumba yote ya Ahabu wataangamia; nami nitamkatilia mbali kila mwanamume wa nyumba ya Ahabu, yeye aliyefungwa, na yeye asiyefungwa, katika Israeli.
Deutéronome 32.36 1 Samuel 25.22 2 Rois 14.26 2 Rois 10.17 1 Rois 14.10-14.11
9 Nami nitaifanya nyumba ya Ahabu kuwa kama nyumba ya Yeroboamu mwana wa Nebati, na kama nyumba ya Baasha mwana wa Ahiya.
1 Rois 15.29 1 Rois 21.22 1 Rois 16.11-16.12 1 Rois 16.3-16.5 1 Rois 14.10-14.11
10 Na mbwa watamla Yezebeli katika kiwanja cha Yezreeli, wala hapatakuwa na mtu wa kumzika. Akaufungua mlango, akakimbia.
1 Rois 21.23 2 Rois 9.35-9.36 2 Rois 9.3 Juges 3.26 Jérémie 22.19
11 Ndipo Yehu akatoka akawaendea watumishi wa bwana wake. Mmoja wao akamwuliza, Je! Ni amani? Huyu mwenye wazimu amekujia kwa nini? Akawaambia, Ninyi mnamjua mtu huyu na habari ya maneno yake.
Jérémie 29.26 Actes 26.24 Jean 10.20 Osée 9.7 Marc 3.21
12 Wakasema, Ni uongo; haya, tuambie. Akasema, Aliniambia haya na haya, akisema, Bwana asema hivi, Nimekutia mafuta, uwe mfalme juu ya Israeli.
13 Basi wakafanya haraka, kila mtu akalitwaa vazi lake, na kulitia chini yake juu ya madaraja, wakapiga baragumu wakasema, Yehu ni mfalme.
1 Rois 1.34 2 Samuel 15.10 1 Rois 1.39 Matthieu 21.7-21.8 Marc 11.7-11.8
14 Hivyo Yehu, mwana wa Yehoshafati, mwana wa Nimshi, akafanya fitina juu ya Yoramu. Basi Yoramu alikuwa akiulinda Ramoth-Gileadi, yeye na Israeli wote, kwa sababu ya Hazaeli mfalme wa Shamu.
2 Rois 8.28 1 Rois 22.3 1 Rois 16.7 2 Rois 9.31 1 Rois 15.27
15 Lakini mfalme Yoramu mwenyewe alikuwa amerudi, apate kupona jeraha zake alizotiwa na Washami, alipokuwa akipigana na Hazaeli mfalme wa Shamu. Yehu akasema, Kama hii ndiyo nia yenu, basi, msimwache hata mtu mmoja atoke mjini, ili aende kupeleka habari Yezreeli.
2 Rois 8.29 2 Chroniques 22.6 1 Samuel 27.9-27.11
16 Basi Yehu akapanda gari lake kwenda Yezreeli; kwa maana Yoramu alikuwa amelala huko; na Ahazia mfalme wa Yuda alikuwa ameshuka ili kumtazama Yoramu.
2 Chroniques 22.6-22.7 2 Rois 8.28-8.29
17 Basi mlinzi alikuwa anasimama juu ya mnara wa Yezreeli, akaliona lile kundi la watu wa Yehu, alipokuwa akija, akasema, Naona kundi la watu. Yoramu akasema, Haya! Mtwae mpanda farasi mmoja, ukampeleke aende kuwalaki, na kuwauliza, Je! Ni amani?
1 Samuel 16.4 Esaïe 21.11-21.12 2 Rois 7.14 2 Samuel 18.24 Esaïe 62.6
18 Basi mpanda farasi mmoja akatoka awalaki, akasema, Mfalme asema hivi, Je! Ni amani? Yehu akasema, Wewe una nini na amani? Geuka unifuate. Yule mlinzi akatoa habari, akasema, Yule mjumbe amewafikilia, lakini harudi tena.
2 Rois 9.22 2 Rois 9.19 Romains 3.17 Esaïe 48.22 Esaïe 59.8
19 Ndipo akapeleka mpanda farasi wa pili, naye akawafikilia, akasema, Mfalme asema hivi, Je! Ni amani? Yehu akasema, Wewe una nini na amani? Geuka unifuate.
20 Yule mlinzi akatoa habari, akasema, Amewafikilia wala harudi tena; na mwendo huu ni kama mwendo wa Yehu mwana wa Nimshi; maana analiendesha gari kwa kasi.
2 Samuel 18.27 Esaïe 54.16 2 Rois 10.16 Daniel 11.44 1 Rois 19.17
21 Yoramu akasema, Tandika gari. Wakalitandika gari lake. Yoramu mfalme wa Israeli akatoka, na Ahazia mfalme wa Yuda, kila mtu katika gari lake. Wakatoka ili kumlaki Yehu, wakamkuta katika kiwanja cha Nabothi, Myezreeli.
1 Rois 21.1-21.7 2 Chroniques 22.7 Nombres 20.14 1 Rois 21.15-21.19 Michée 1.13
22 Ikawa, Yoramu alipomwona Yehu, akasema, Je! Ni amani, Yehu? Akajibu, Amani gani, maadamu uzinzi wa mama yako Yezebeli na uchawi wake ni mwingi?
1 Rois 16.30-16.33 2 Chroniques 21.13 Esaïe 57.19-57.21 Apocalypse 18.23 Apocalypse 2.20-2.23
23 Yoramu akageuza mikono yake, akakimbia, akamwambia Ahazia, Ni uhaini, Ahazia.
2 Rois 11.14 2 Chroniques 23.13
24 Yehu akavuta upinde wake kwa nguvu zake zote, akampiga Yoramu kati ya mikono yake, hata mshale ukamtoka penye moyo wake, akaanguka katika gari lake.
1 Rois 22.34 Psaumes 50.22 Ecclésiaste 8.12-8.13 1 Thessaloniciens 5.3 Proverbes 21.30
25 Ndipo Yehu akamwambia Bidkari, akida wake, Mtwae ukamtupe katika kiwanja cha Nabothi, Myezreeli; maana kumbuka, hapo mimi na wewe tulipokuwa tumepanda farasi zetu, na kumfuata Anabu baba yake, Bwana alimwekea mzigo huu, akasema;
1 Rois 21.19 Esaïe 13.1 1 Rois 21.24-21.29 Matthieu 11.30 Malachie 1.1
26 Hakika, jana nimeiona damu ya Nabothi, na damu ya wanawe, asema Bwana; nami nitakulipa katika kiwanja hiki, asema Bwana. Basi sasa mtwae huyu ukamtupe katika kiwanja hicho, sawasawa na neno la Bwana.
1 Rois 21.19 2 Chroniques 24.25 Deutéronome 5.9 Deutéronome 24.16 Ezéchiel 18.19
27 Na Ahazia mfalme wa Yuda alipoona hayo, akakimbia kwa njia ya nyumba ya bustanini. Yehu akamfuatia, akasema, Mpigeni huyu naye katika gari lake; wakampiga hapo penye kupandia Guri, karibu na Ibleamu. Akakimbilia Megido, akafa huko.
Juges 1.27 Josué 17.11 2 Rois 23.29-23.30 1 Rois 4.12 Proverbes 13.20
28 Na watumishi wake wakamchukua garini mpaka Yerusalemu, wakamzika katika kaburi lake pamoja na baba zake katika mji wa Daudi.
2 Chroniques 35.24 2 Rois 23.30 2 Rois 23.20 2 Rois 14.19-14.20 2 Rois 12.21
29 Katika mwaka wa kumi na moja wa Yoramu mwana wa Ahabu, Ahazia alianza kutawala juu ya Yuda.
2 Chroniques 21.18-21.19 2 Rois 8.16 2 Chroniques 22.1-22.2 2 Rois 8.24-8.25
30 Hata Yehu alipofika Yezreeli, Yezebeli akapata habari; akatia uwanja machoni mwake, akapamba kichwa chake, akachungulia dirishani.
Jérémie 4.30 Ezéchiel 23.40 Ezéchiel 24.17 1 Pierre 3.3 1 Timothée 2.9-2.10
31 Hata Yehu alipoingia lango la mji, alisema, Je! Ni amani, Ewe Zimri, mwenye kumwua bwana wako?
1 Rois 16.9-16.20
32 Akainua uso wake kulielekea dirisha, akasema, Aliye upande wangu ni nani? Matowashi wawili watatu wakachungulia.
Psaumes 118.6 1 Chroniques 12.18 Esther 2.15 Psaumes 124.1-124.2 2 Chroniques 11.12
33 Akasema, Mtupeni chini. Basi wakamtupa chini; na damu yake ikamwagika nyingine juu ya ukuta, na nyingine juu ya farasi, naye akamkanyaga-kanyaga.
2 Rois 7.20 Hébreux 10.29 Malachie 4.3 Lamentations 1.15 Michée 7.10
34 Alipoingia, akala, na kunywa; kisha akasema, Haya! Mwangalieni mwanamke huyu aliyelaaniwa, mkamzike; kwa maana ni binti mfalme.
1 Rois 16.31 1 Rois 21.25 Esaïe 65.15 Matthieu 25.41 Proverbes 10.7
35 Wakaenda ili kumzika; lakini hawakuona kitu ila kifuvu cha kichwa chake, na miguu yake, na vitanga vya mikono yake.
Ecclésiaste 6.3 Jérémie 22.19 Actes 12.23 Esaïe 14.18-14.20 Job 31.3
36 Basi wakarudi, wakampasha habari. Akasema, Hili ndilo neno la Bwana, alilolinena kwa kinywa cha mtumishi wake Eliya, Mtishbi, kusema, Katika kiwanja cha Yezreeli mbwa wataila nyama ya Yezebeli.
1 Rois 21.23 2 Samuel 12.25 Lévitique 8.36 2 Rois 14.25
37 Na mzoga wa Yezebeli utakuwa kama mavi juu ya uso wa mashamba, katika kiwanja cha Yezreeli; hata wasipate kusema, Huyu ni Yezebeli.
Jérémie 8.2 Jérémie 16.4 Psaumes 83.10 Jérémie 25.33 Jérémie 9.22

Cette Bible est dans le domaine public.