Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Rois 23.27
Bible en Swahili de l’est


1 Kisha, mfalme akatuma wajumbe, nao wakamkusanyia wazee wote wa Yuda na wa Yerusalemu.
2 Chroniques 29.20 2 Chroniques 34.29-34.33 Deutéronome 31.28 2 Chroniques 30.2 2 Samuel 6.1
2 Mfalme akapanda kwenda nyumbani kwa Bwana, na watu wote wa Yuda, nao wote waliokaa Yerusalemu, pamoja naye, na makuhani, na manabii, na watu wote, wadogo kwa wakubwa; akasoma masikioni mwao maneno yote ya kitabu cha agano kilichoonekana katika nyumba ya Bwana.
2 Rois 22.8 Apocalypse 20.12 Deutéronome 31.10-31.13 Psaumes 115.13 1 Samuel 30.2
3 Mfalme akasimama karibu na nguzo, akafanya agano mbele za Bwana, kumfuata Bwana, na kuyashika maagizo yake, na shuhuda zake, na amri zake, kwa moyo wake wote, na kwa roho yake yote, na kuyathibitisha maneno ya agano hilo yaliyoandikwa katika kitabu hicho; nao watu wote wakalikubali agano lile.
2 Rois 11.14 2 Rois 11.17 Deutéronome 13.4 Deutéronome 29.1 Néhémie 10.28-10.39
4 Kisha, mfalme akamwamuru Hilkia, kuhani mkuu, na makuhani wa daraja ya pili, na walinzi wa mlango, kwamba watoe katika hekalu la Bwana vyombo vyote vilivyofanywa kwa ajili ya Baali, na kwa ajili ya Ashera, na kwa ajili ya jeshi lote la mbinguni; akavipiga moto nje ya Yerusalemu, katika mashamba ya Ridroni, akayachukua majivu yake mpaka Betheli.
2 Rois 21.3 2 Rois 21.7 2 Rois 25.18 2 Chroniques 33.3 1 Rois 18.26
5 Akawaondosha wale makuhuni walioabudu sanamu, ambao wafalme wa Yuda waliwaweka ili kufukiza uvumba katika mahali pa juu, ndani ya miji ya Yuda, na katika kila mahali, pande zote za Yerusalemu; na hao pia waliomfukizia uvumba Baali, na jua, na mwezi, na sayari, na jeshi lote la mbinguni.
Osée 10.5 Jérémie 44.17-44.19 2 Rois 21.3-21.4 Jérémie 8.1-8.2
6 Naye akaiondoa Ashera katika nyumba ya Bwana, nje ya Yerusalemu, mpaka Kidroni, akaipiga moto penye kijito cha Kidroni, na kuiponda-ponda iwe mavumbi, akayatupa mavumbi yake juu ya makaburi ya watu.
2 Chroniques 34.4 2 Rois 23.15 Jérémie 17.2 Exode 32.20 2 Rois 10.27
7 Akaziangusha nyumba za mahanithi, waliokuwamo nyumbani mwa Bwana, wanawake walipofuma mapazia ya Ashera.
Ezéchiel 16.16 1 Rois 15.12 1 Rois 14.24 Exode 35.25-35.26 Osée 2.13
8 Akawatoa makuhani wote katika miji ya Yuda, akapanajisi mahali pa juu, makuhani walipokuwa wamefukiza uvumba, tangu Geba hata Beer-sheba; akapavunja mahali pa juu pa malango, palipokuwapo penye kuingia lango la Yoshua, liwali wa mji, palipokuwa upande wa kushoto wa mtu langoni pa mji.
1 Rois 15.22 Josué 21.17 1 Chroniques 6.60 1 Rois 19.3 Zacharie 14.10
9 Walakini hao makuhani wa mahali pa juu hawakupanda madhabahuni kwa Bwana katika Yerusalemu, bali wakala mikate isiyo na chachu katikati ya ndugu zao.
Ezéchiel 44.10-44.14 Malachie 2.8-2.9 1 Samuel 2.36 Ezéchiel 44.29-44.31
10 Naye akainajisi Tofethi, iliyomo katika bonde la wana wa Hinomu, ili mtu asipitishe mwana wake au binti yake motoni kwa Moleki.
Esaïe 30.33 Jérémie 7.31-7.32 Jérémie 19.6 Lévitique 18.21 Josué 15.8
11 Akawaondoa farasi ambao wafalme wa Yuda waliwatoa kwa jua, hapo pa kuingia nyumbani mwa Bwana, karibu na chumba cha Nathan-Meleki, towashi, kilichohuwako kiungani; akayapiga moto magari ya jua.
Ezéchiel 8.16 2 Chroniques 14.5 2 Rois 23.5 Deutéronome 4.19 2 Chroniques 34.4
12 Nazo madhabahu zilizokuwako darini juu ya chumba cha juu cha Ahazi, wafalme wa Yuda walizozifanya, nazo madhabahu alizozifanya Manase katika behewa mbili za nyumba ya Bwana, mfalme akazivunja, akazitelemsha huko nje, na kuyatupa mavumbi yake katika kijito cha Kidroni.
2 Rois 21.5 Sophonie 1.5 Jérémie 19.13 2 Chroniques 33.5 Deutéronome 22.8
13 Na mahali pa juu palipokuwapo mbele ya Yerusalemu, palipokuwa upande wa kuume wa mlima wa uharibifu, alipopajenga Sulemani, mfalme wa Israeli, kwa Ashtorethi, chukizo la Wasidoni, na Kemoshi, chukizo la Moabu, na Milkomu, chukizo la wana wa Amoni, mfalme akapanajisi.
1 Rois 11.5 1 Rois 11.7 Nombres 21.29 Juges 10.6 1 Samuel 12.10
14 Akazivunja-vunja nguzo, akayakata-kata maashera, akapajaza mahali pake mifupa ya watu.
Exode 23.24 Deutéronome 7.5 2 Rois 23.16 Michée 1.7 Jérémie 8.1-8.2
15 Tena zaidi ya hayo, ile madhabahu iliyokuwako Betheli, na mahali pa juu alipopafanya Yeroboamu, mwana wa Nebati, aliyewakosesha Israeli, madhabahu hiyo aliibomoa; na mahali pa juu alipateketeza, akapaponda-ponda hata pakawa mavumbi, akaiteketeza ile Ashera.
1 Rois 14.16 2 Rois 10.31 1 Rois 15.30 2 Rois 23.6 1 Rois 12.28-13.1
16 Naye Yosia alipogeuka, aliyaona makaburi yale yaliyokuwako huko, juu ya mlima; akatuma watu, akaitoa ile mifupa katika yale makaburi, akaiteketeza juu ya madhabahu, akainajisi, sawasawa na lile neno la Bwana, alilolinena yule mtu wa Mungu, aliyetamka mambo hayo.
1 Rois 13.32 Jean 10.35 1 Rois 13.1-13.2 Matthieu 24.35
17 Kisha akasema, Ni kumbukumbu la nani, hili ninaloliona? Na watu wa mji wakamwambia, Ni kaburi la yule mtu wa Mungu, aliyetoka Yuda, akayanena mambo hayo uliyoyatenda wewe juu ya madhabahu ya Betheli.
1 Rois 13.1 1 Rois 13.30-13.31
18 Akasema, Mwacheni; mtu awaye yote asiiondoe mifupa yake. Basi wakaiacha mifupa yake, pamoja na mifupa ya yule nabii aliyetoka Samaria.
1 Rois 13.31 1 Rois 13.1-13.22
19 Na nyumba zote pia za mahali pa juu palipokuwa katika miji ya Samaria, wafalme wa Israeli walizozifanya, ili kumkasirisha Bwana, Yosia aliziondoa, akazitenda kwa mfano wa mambo yote aliyoyatenda katika Betheli.
2 Chroniques 34.6-34.7 1 Rois 16.33 2 Chroniques 31.1 2 Rois 17.16-17.18 1 Rois 13.32
20 Akawaua na makuhani wote wa mahali pa juu waliokuwako huko, juu ya madhabahu, akateketeza mifupa ya watu juu yake; kisha akarejea Yerusalemu.
2 Rois 11.18 2 Rois 10.25 Exode 22.20 1 Rois 18.40 2 Chroniques 34.5
21 Naye mfalme akawaamuru watu wote, akasema, Mfanyieni Bwana, Mungu wenu, pasaka, kama ilivyoandikwa katika kitabu hiki cha agano.
Deutéronome 16.1-16.8 Lévitique 23.5-23.8 2 Chroniques 35.1-35.19 Nombres 9.2-9.5 Exode 12.3-12.20
22 Hakika yake haikufanyika pasaka kama hiyo, tangu zamani za waamuzi waliowaamua Israeli, wala katika zamani za wafalme wa Israeli, wala za wafalme wa Yuda.
2 Chroniques 30.1-30.3 2 Chroniques 35.3-35.19 2 Chroniques 30.13-30.20
23 Bali katika mwaka wa kumi na nane wa mfalme Yosia ilifanyika pasaka hii kwa Bwana ndani ya Yerusalemu.
24 Tena wenye pepo wa utambuzi, na wachawi, na vinyago, na sanamu, na machukizo yote yaliyoonekana katika nchi ya Yuda na katika Yerusalemu, Yosia akayaondoa yote, ili apate kuyathibitisha maneno ya torati yaliyoandikwa katika kile kitabu alichokiona Hilkia kuhani ndani ya nyumba ya Bwana.
Lévitique 19.31 Genèse 31.19 2 Rois 21.6 Deutéronome 18.10-18.12 Lévitique 20.27
25 Kabla ya huyo hapakuwa na mfalme mfano wake, aliyemwelekea Bwana kwa moyo wake wote, na kwa roho yake yote, na kwa nguvu zake zote, sawasawa na sheria zote za Musa; wala baada yake hakuinuka mmoja mfano wake yeye.
2 Rois 18.5 Jean 1.17 Jean 7.19 1 Rois 15.5 Jérémie 29.13
26 Walakini Bwana hakuuacha ukali wa ghadhabu yake nyingi, ambayo kwayo hasira yake iliwaka juu ya Yuda, kwa sababu ya machukizo yote ambayo Manase amemchukiza.
2 Rois 21.11-21.13 2 Rois 24.4 2 Chroniques 36.16 Jérémie 15.1-15.4 2 Rois 22.16-22.17
27 Bwana akasema Nitawahamisha Yuda pia mbali nami, kama nilivyowahamisha Israeli, nami nitautupa mji huu niliouchagua, naam, Yerusalemu, na nyumba ile niliyoinena, Jina langu litakuwa humo.
2 Rois 18.11 2 Rois 21.13 2 Rois 17.18 2 Rois 21.4 2 Rois 17.20
28 Basi mambo yote ya Yosia yaliyosalia, na yote aliyoyafanya, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Yuda?
2 Rois 20.20
29 Katika siku zake, Farao-neko, mfalme wa Misri, akakwea ili kupigana na mfalme wa Ashuru, akafika mto Frati; naye mfalme Yosia akaenda kupigana naye; naye mfalme wa Misri akamwua huko Megido, hapo alipoonana naye.
Jérémie 46.2 Zacharie 12.11 2 Chroniques 35.20-35.24 Juges 5.19 2 Rois 9.27
30 Watumishi wake wakamchukua garini, amekwisha kufa, kutoka Megido, wakamleta Yerusalemu, wakamzika katika kaburi lake mwenyewe. Watu wa nchi wakamtwaa Yehoahazi mwana wa Yosia, wakamtia mafuta, wakamtawaza awe mfalme badala ya baba yake.
2 Rois 9.28 2 Chroniques 36.1-36.4 2 Rois 21.24 1 Rois 22.33-22.38 2 Rois 14.21

Règne de Joachaz sur Juda

31 Yehoahazi alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitatu alipoanza kutawala; akatawala miezi mitatu katika Yerusalemu; na jina la mamaye aliitwa Hamutali binti Yeremia wa Libna.
1 Chroniques 3.15 Jérémie 22.11 2 Rois 24.18
32 Akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, sawasawa na yote waliyoyafanya baba zake.
2 Rois 21.2-21.7 2 Rois 21.21-21.22
33 Naye Farao-neko akamfunga huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, ili asitawale huko Yerusalemu. Akaitoza nchi kodi talanta mia za fedha na talanta ya dhahabu.
2 Rois 25.6 1 Rois 8.65 Jérémie 39.5-39.6 Jérémie 52.26-52.27 Jérémie 52.9-52.10
34 Farao-neko akamfanya Eliakimu mwana wa Yosia awe mfalme mahali pa Yosia babaye, akambadilisha jina lake kuwa Yehoyakimu, lakini akamwondoa Yehoahazi; akaenda naye Misri, naye akafa huko.
Ezéchiel 19.3-19.4 1 Chroniques 3.15 Jérémie 22.11-22.12 2 Rois 24.17 Daniel 1.7
35 Na Yehoyakimu akampa Farao dhahabu na fedha; lakini akaitoza nchi kodi, ili apate kutoa zile fedha kwa amri yake Farao; akawatoza fedha na dhahabu watu wa nchi, kila mtu kwa kodi yake, ili ampe Farao-neko.
2 Rois 23.33 2 Rois 15.19-15.20

Règne de Jojakim sur Juda

36 Yehoyakimu alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala; akatawala miaka kumi na mmoja huko Yerusalemu; na jina la mamaye aliitwa Zebida binti Pedaya wa Ruma.
2 Chroniques 36.5 Jérémie 1.3 Jérémie 26.1 1 Chroniques 3.15
37 Akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, sawasawa na yote waliyoyafanya baba zake.
Jérémie 36.23-36.26 Jérémie 22.13-22.17 2 Chroniques 28.22-28.25 Ezéchiel 19.5-19.9 Jérémie 26.20-26.23

Cette Bible est dans le domaine public.