Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Rois 2.18
Bible en Swahili de l’est


Derniers instants et mort de David

1 Basi siku ya kufa kwake Daudi ikakaribia, akamwusia Sulemani mwanawe, akasema,
Genèse 47.29 Deutéronome 31.14 Actes 20.28-20.31 Nombres 27.19 1 Timothée 1.18
2 Mimi naenda njia ya ulimwengu wote; basi uwe hodari, ujionyeshe kuwa mwanamume;
Josué 23.14 Josué 1.6-1.7 Ecclésiaste 12.13 2 Samuel 10.12 Deutéronome 31.6-31.7
3 uyashike mausia ya Bwana, Mungu wako, uende katika njia zake, uzishike sheria zake, na amri zake, na hukumu zake, na shuhuda zake, sawasawa na ilivyoandikwa katika torati ya Musa, upate kufanikiwa katika kila ufanyalo, na kila utazamako;
Deutéronome 29.9 1 Chroniques 22.12-22.13 Deutéronome 17.18-17.20 Malachie 4.4 2 Chroniques 31.20-31.21
4 ili Bwana afanye imara neno lake alilonena kwa habari yangu, akisema, Ikiwa watoto wako wataiangalia njia yao, wakienda mbele zangu kwa kweli, kwa moyo wao wote, na kwa roho yao yote, (akasema), hutakosa mtu katika kiti cha enzi cha Israeli.
2 Rois 20.3 1 Rois 8.25 2 Samuel 7.25 Jude 1.20-1.21 1 Chroniques 28.5-28.7
5 Na zaidi ya hayo, umejua alivyonitenda Yoabu, mwana wa Seruya, yaani, alivyowatenda majemadari wawili wa majeshi ya Israeli, Abneri, mwana wa Neri, na Amasa, mwana wa Yetheri, ambao aliwaua, na kuimwaga damu ya vita wakati wa amani, akautia damu ya vita mshipi uliokuwa viunoni mwake, na viatu vilivyokuwa miguuni mwake.
2 Samuel 3.27 2 Samuel 20.10 2 Samuel 18.12 2 Samuel 18.5 2 Samuel 3.39
6 Kwa hiyo ufanye kama ilivyo hekima yako, wala usimwachie mvi zake kushukia Ahera kwa amani.
1 Rois 2.9 Nombres 35.33 1 Rois 2.28-2.34 Genèse 9.6 2 Rois 22.20
7 Lakini uwafanyie mema wana wa Barzilai Mgileadi, wawe miongoni mwao walao mezani pako; kwa jinsi walivyonijilia nilipokuwa nimekimbia mbele ya Absalomu, ndugu yako.
2 Samuel 9.7 2 Samuel 9.10 2 Samuel 17.27-17.29 Proverbes 27.10 Luc 22.28-22.30
8 Hata, angalia, yuko pamoja nawe Shimei, mwana wa Gera, Mbenyamini, wa Bahurimu, ndiye aliyenilaani kwa laana kuu siku ile nilipokwenda Mahanaimu; lakini akashuka kunilaki kule Yordani, nami nikamwapia kwa Bwana, nikamwambia, Mimi sitakuua kwa upanga.
2 Samuel 16.5-16.8 2 Samuel 19.16-19.23 Jérémie 4.2 1 Rois 2.36-2.46
9 Basi kwa hiyo usimwachilie, kwa kuwa wewe u mtu wa akili; nawe utajua ikupasayo umtendee, na mvi zake utazishusha Ahera pamoja na damu.
1 Rois 2.6 Genèse 42.38 Genèse 44.31 Exode 20.7 1 Rois 3.28
10 Basi Daudi akalala na babaze, akazikwa mjini mwa Daudi.
2 Samuel 5.7 1 Rois 3.1 Actes 2.29 Actes 13.36 1 Rois 1.21
11 Na siku alizotawala Daudi juu ya Israeli zilikuwa miaka arobaini; huko Hebroni alitawala miaka saba, na katika Yerusalemu akatawala miaka thelathini na mitatu.
1 Chroniques 29.26-29.27 2 Samuel 5.4-5.5
12 Basi Sulemani akaketi katika kiti cha enzi cha Daudi baba yake; na ufalme wake ukawa imara sana.
2 Chroniques 1.1 Psaumes 72.8-72.20 2 Samuel 7.12-7.13 2 Samuel 7.29 Psaumes 132.12

Premières décisions du roi Salomon

13 Ndipo Adonia mwana wa Hagithi akaja kwa Bath-sheba mamaye Sulemani. Naye akasema, Je! Umekuja kwa amani?
2 Rois 9.18-9.22 1 Rois 1.50-1.53 1 Chroniques 12.17-12.18 1 Rois 1.5-1.10 1 Samuel 16.4-16.5
14 Naye akajibu, Kwa amani. Tena akasema, Nina shauri ninalotaka kukuambia. Naye akamwambia, Sema.
2 Samuel 14.12 Luc 7.40
15 Basi akasema, Wajua ya kwamba ufalme ulikuwa wangu, na Israeli wote wakaniwekea nyuso zao ili nimiliki mimi; walakini sasa ufalme umegeuka kuwa wake ndugu yangu; kwa maana ulikuwa wake kutoka kwa Bwana.
1 Chroniques 28.5-28.7 1 Chroniques 22.9-22.10 1 Rois 1.5 1 Rois 1.25 Jérémie 27.5-27.8
16 Basi sasa nina haja moja ninayokuomba, usinikataze hiyo. Naye akamwambia, Sema.
Psaumes 132.10 Proverbes 30.7
17 Akasema, Nena, nakusihi, na Sulemani, mfalme, (kwa kuwa hawezi kukukataza neno), kwamba anioze Abishagi, Mshunami.
1 Rois 1.2-1.4 2 Samuel 3.7 2 Samuel 12.8
18 Naye Bath-sheba akasema, Vema; nitasema na mfalme kwa ajili yako.
Proverbes 14.15
19 Basi Bath-sheba akaingia kwa mfalme Sulemani, aseme naye kwa ajili ya Adonia. Naye mfalme akainuka kwenda kumlaki, akamwinamia, akaketi katika kiti chake cha enzi; kisha akaagiza awekewe kiti cha enzi mamaye mfalme; naye akaketi mkono wake wa kuume.
Psaumes 45.9 Matthieu 25.33 Exode 20.12 Psaumes 110.1 Lévitique 19.3
20 Ndipo akasema, Haja moja ndogo nakuomba; usinikataze. Mfalme akamwambia, Omba, mama; kwa kuwa siwezi kukukataza neno.
Jean 15.16 Matthieu 18.19 Matthieu 11.24 Matthieu 10.35-10.36 Jean 14.13-14.14
21 Naye akasema, Nataka Adonia, ndugu yako, aozwe Abishagi, Mshunami.
1 Rois 1.3 2 Samuel 16.21-16.22
22 Akajibu mfalme Sulemani akamwambia mamaye, Na mbona wamtakia Adonia Abishagi, Mshunami? Umtakie na ufalme pia; kwa kuwa yeye ni ndugu yangu mkubwa; naam, umtakie yeye, na Abiathari kuhani, na Yoabu mwana wa Seruya.
1 Chroniques 3.2 1 Rois 1.5-1.7 Jacques 4.3 1 Chroniques 3.5 Marc 10.38
23 Ndipo mfalme Sulemani akaapa kwa Bwana, akasema, Mungu anifanyie hivyo, na kuzidi, isipokuwa Adonia amenena neno hili juu ya uhai wake mwenyewe.
Ruth 1.17 Luc 19.22 Proverbes 18.6-18.7 2 Samuel 3.9 1 Rois 20.10
24 Basi kwa hiyo, Bwana aishivyo, aliyenithibitisha na kunikalisha katika kiti cha enzi cha Daudi baba yangu, akanifanyia nyumba, kama alivyoahidi, hakika atauawa leo hivi Adonia.
1 Chroniques 22.10 Ecclésiaste 8.11-8.13 2 Chroniques 1.8-1.9 1 Chroniques 29.23 1 Chroniques 17.23
25 Mfalme Sulemani akatuma kwa mkono wa Benaya mwana wa Yehoyada: naye akampiga, hata akafa.
2 Samuel 8.18 1 Rois 2.34 Juges 8.20-8.21 2 Samuel 1.15 1 Samuel 15.33
26 Tena, mfalme akamwambia Abiathari kuhani, Enenda Anathothi mashambani kwako; kwa kuwa wastahili kufa; ila leo sikuui, kwa sababu wewe ulichukua sanduku la Bwana mbele ya Daudi baba yangu, na kwa sababu wewe uliteswa kwa mateso yote ya baba yangu.
Josué 21.18 1 Samuel 22.20-22.23 Jérémie 1.1 2 Samuel 15.24-15.29 Matthieu 10.42
27 Hivyo Sulemani akamtoa Abiathari asiwe kuhani wa Bwana; ili alitimize neno la Bwana, alilonena juu ya nyumba ya Eli katika Shilo.
1 Samuel 2.27-2.36 Psaumes 78.60 Jean 19.24 Josué 18.1 Jérémie 7.12-7.14
28 Tena, habari zikamfikia Yoabu; kwa maana Yoabu alikuwa amemfuata Adonia, ingawa hakumfuata Absalomu. Yoabu akakimbilia Hemani kwa Bwana, akazishika pembe za madhabahu.
1 Rois 1.50 1 Rois 1.7 2 Samuel 18.2 Exode 27.2 Deutéronome 32.35
29 Akaambiwa mfalme Sulemani ya kwamba, Yoabu amekimbilia Hemani kwa Bwana, naye, tazama, yuko madhabahuni. Ndipo Sulemani akamtuma Benaya, mwana wa Yehoyada, akisema, Enenda, umpige.
1 Rois 2.25 Exode 21.14 1 Pierre 4.17 Ezéchiel 9.6 1 Rois 2.46
30 Basi Benaya akaja Hemani kwa Bwana, akamwambia, Mfalme asema hivi, Njoo utoke. Naye akajibu, La, sivyo; ila nitakufa papa hapa. Naye Benaya akamletea mfalme habari, akisema, Hivi ndivyo alivyonena Yoabu, na ndivyo alivyonijibu.
31 Mfalme akamwambia, Fanya alivyonena, umpige, ukamzike; ili uniondolee mimi na nyumba ya babangu damu aliyoimwaga Yoabu bure.
Deutéronome 21.8-21.9 Nombres 35.33 Exode 21.14 Actes 28.4 2 Rois 9.26
32 Naye Bwana atamrudishia damu yake kichwani pake mwenyewe, kwa kuwa aliwapiga watu wawili wenye haki, na wema kuliko yeye, akawaua kwa upanga, wala babangu Daudi hakujua habari hiyo; yaani Abneri, mwana wa Neri, jemadari wa jeshi la Israeli, na Amasa, mwana wa Yetheri, jemadari wa jeshi la Yuda.
Juges 9.24 2 Chroniques 21.13 Juges 9.57 Psaumes 7.16 1 Rois 2.5
33 Hivyo damu yao itarudi kichwani pa Yoabu, na kichwani pa wazao wake hata milele; ila kwa Daudi, na kwa wazao wake, na kwa nyumba yake, na kwa kiti chake cha enzi, kutakuwa na amani hata milele kutoka kwa Bwana.
1 Rois 2.32 Psaumes 89.36-89.37 Psaumes 109.6-109.15 Psaumes 132.12 Psaumes 101.8
34 Ndipo Benaya, mwana wa Yehoyada, akapanda, akampiga, akamwua; naye akazikwa katika nyumba yake mwenyewe iliyoko nyikani.
1 Rois 2.25 Josué 15.61 Matthieu 3.1 2 Chroniques 33.20 2 Rois 21.18
35 Kisha mfalme akamweka Benaya, mwana wa Yehoyada, mahali pake juu ya jeshi; na Sadoki, kuhani, mfalme akamweka mahali pa Abiathari.
1 Rois 2.27 1 Rois 4.4 1 Chroniques 29.22 1 Chroniques 24.3 1 Chroniques 6.4-6.15
36 Tena, mfalme akatuma watu akamwita Shimei, akamwambia, Ujijengee nyumba humu Yerusalemu, ukae ndani yake, wala usitoke humo kwenda mahali po pote.
Proverbes 20.26 2 Samuel 16.5-16.9 2 Samuel 14.28 1 Rois 1.53 2 Samuel 14.24
37 Kwa kuwa siku ile ya kutoka kwako, na kuvuka kijito Kidroni, ujue hakika ya kwamba kufa utakufa; damu yako itakuwa juu ya kichwa chako mwenyewe.
2 Samuel 1.16 2 Samuel 15.23 Josué 2.19 Ezéchiel 18.13 Lévitique 20.9
38 Naye Shimei akamwambia mfalme, Neno hili ni jema; kama alivyosema bwana wangu mfalme, ndivyo atakavyofanya mtumwa wako. Basi Shimei akakaa Yerusalemu siku nyingi.
1 Rois 20.4 2 Rois 20.19
39 Ikawa miaka mitatu ilipokwisha, watumwa wawili wa Shimei wakatoroka kwenda kwa Akishi, mwana wa Maaka, mfalme wa Gathi. Wakamwambia Shimei, wakasema, Angalia, watumwa wako wako huko Gathi.
1 Samuel 21.10 1 Samuel 27.2-27.3
40 Shimei akaondoka, akatandika punda wake, akaenda Gathi kwa Akishi, ili kuwatafuta watumwa wake. Akaenda Shimei, akawaleta watumwa wake toka Gathi.
Luc 12.15 1 Timothée 6.10 Proverbes 15.27
41 Naye Sulemani akaambiwa, ya kwamba Shimei alikuwa ametoka Yerusalemu kwenda Gathi, na kurudi tena.
42 Basi, mfalme akatuma watu, akamwita Shimei, akamwambia, Je! Sikukuapisha kwa Bwana, na kukushuhudia, kusema, Siku ile ya kutoka kwako ukienda mahali po pote, ujue hakika ya kwamba kufa utakufa? Nawe ukaniambia, Neno hili nililolisikia ni jema?
Luc 19.22 1 Rois 2.36-2.38 Luc 15.22 Psaumes 15.4
43 Mbona basi hukukishika kiapo cha Bwana, na amri niliyokuagiza?
Romains 13.5 Ezéchiel 17.18-17.19 Ecclésiaste 8.2 2 Samuel 21.2 2 Chroniques 30.12
44 Tena, mfalme akamwambia Shimei, Umejua uovu wote uliouona moyoni mwako, uliomtenda Daudi baba yangu; basi kwa hiyo Bwana atakurudishia uovu wako kichwani pako mwenyewe.
2 Samuel 16.5-16.13 Ezéchiel 17.19 Psaumes 7.16 1 Samuel 25.39 Jean 8.9
45 Ila mfalme Sulemani atakuwa amebarikiwa, na kiti cha enzi cha Daudi kitathibitika mbele za Bwana hata milele.
Proverbes 25.5 Psaumes 21.6 1 Rois 2.24 1 Rois 2.33-2.34 Esaïe 9.6-9.7
46 Basi mfalme akamwamuru Benaya, mwana wa Yehoyada; naye akatoka, akampiga, hata akafa. Nao ufalme ukawa imara mkononi mwa Sulemani.
1 Rois 2.12 2 Chroniques 1.1 Proverbes 29.4 1 Rois 2.45

Cette Bible est dans le domaine public.