Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Samuel 11.9
Bible en Swahili de l’est


Adultère et crime de David

1 Hata ikawa, mwanzo wa mwaka mpya, wakati watokapo wafalme kwenda vitani, Daudi akampeleka Yoabu, na watumishi wake pamoja naye, na Israeli wote; wakawaangamiza wana wa Amoni, wakauhusuru Raba. Lakini Daudi mwenyewe akakaa Yerusalemu.
1 Chroniques 20.1 1 Rois 20.26 1 Rois 20.22 2 Chroniques 36.10 Deutéronome 3.11
2 Ikawa wakati wa jioni, Daudi akaondoka kitandani, akatembea juu ya dari ya jumba la mfalme; na alipokuwa juu ya dari aliona mwanamke anaoga; naye huyo mwanamke alikuwa mzuri sana, wa kupendeza macho.
Deutéronome 22.8 Matthieu 5.28 Job 31.1 Actes 10.9 Proverbes 24.33-24.34
3 Naye Daudi akapeleka, akauliza habari za yule mwanamke. Mtu mmoja akasema, Je! Huyu siye Bath-sheba, binti Eliamu, mkewe Uria, Mhiti?
2 Samuel 23.39 1 Chroniques 3.5 Jérémie 5.8 Osée 7.6-7.7 1 Chroniques 11.41
4 Basi Daudi akapeleka wajumbe, akamtwaa; naye akaingia kwake; naye akalala naye; (maana yule mwanamke amekwisha kutakasika unajisi wake); kisha akarudi nyumbani kwake.
Lévitique 18.19 Jacques 1.14-1.15 Lévitique 12.2-12.5 Psaumes 51.1-51.19 Lévitique 15.19-15.33
5 Yule mwanamke akachukua mimba; basi akapeleka na kumwambia Daudi, akasema, Ni mja-mzito.
Deutéronome 22.22 Proverbes 6.34
6 Ndipo Daudi akapeleka kwa Yoabu, akisema, Unipelekee Uria, Mhiti. Naye Yoabu akampeleka Uria kwa Daudi.
Proverbes 28.13 Genèse 4.7 Job 20.12-20.14 Genèse 38.18-38.23 Matthieu 26.70
7 Uria alipomwendea Daudi, Daudi alimwuliza habari za Yoabu, na habari za watu, na habari za vita.
1 Samuel 17.22 Genèse 37.14 Genèse 29.6
8 Daudi akamwambia Uria, Haya, shuka nyumbani kwako, ukanawe miguu yako. Basi Uria akatoka katika nyumba ya mfalme, na tunu ya vyakula ikamfuata, iliyotoka kwa mfalme.
Genèse 18.4 Genèse 43.24 Hébreux 4.13 Genèse 43.34 Esaïe 29.15
9 Lakini Uria akalala mlangoni pa nyumba ya mfalme, pamoja na watumishi wote wa bwana wake, wala hakushuka nyumbani kwake.
Job 5.12-5.14 Proverbes 21.30
10 Watu walipomwambia Daudi ya kwamba, Uria hakushuka nyumbani kwake, Daudi akamwambia Uria, Je! Hukutoka safarini? Mbona hukushuka nyumbani kwako?
11 Naye Uria akamwambia Daudi, Sanduku, na Israeli, na Yuda, wanakaa vibandani; na bwana wangu Yoabu, na watumishi wa bwana wangu, wamepiga kambi waziwazi uwandani; nami niende nyumbani kwangu, kula na kunywa, na kulala na mke wangu? Uishivyo, na kama roho yako iishivyo, mimi sitafanya jambo hili.
2 Samuel 7.2 2 Samuel 20.6 2 Samuel 7.6 1 Samuel 1.26 1 Samuel 14.18
12 Basi Daudi akamwambia Uria, Ngoja hapa leo tena, na kesho nitakuacha kwenda zako. Basi Uria akakaa Yerusalemu siku ile, na siku ya pili yake.
Jérémie 2.37 Jérémie 2.22-2.23
13 Naye Daudi akamwalika, akala, akanywa mbele yake; naye akamlevya; hata wakati wa jioni akatoka kwenda kulala kitandani mwake pamoja na watumishi wa bwana wake, lakini hakushuka nyumbani kwake.
Habakuk 2.15 Exode 32.21 Genèse 19.32-19.35 Proverbes 20.1
14 Hata ikawa asubuhi, Daudi akamwandikia Yoabu waraka, akaupeleka kwa mkono wa Uria.
1 Rois 21.8-21.10 Jérémie 17.9 Jérémie 9.1-9.4 Michée 7.3-7.5 Psaumes 52.2
15 Akaandika katika waraka huo, kusema, Mwekeni Uria mbele ya watu penye vita vikali, kisha ondokeni, mmwache, ili apigwe akafe.
2 Samuel 12.9 Jérémie 20.13 Psaumes 51.4 1 Samuel 18.25 1 Samuel 18.17
16 Ikawa, Yoabu alipokuwa akiuhusuru mji, akamweka Uria mahali alipojua ya kuwa pana mashujaa.
1 Rois 2.5 2 Samuel 20.9-20.10 Actes 5.29 Proverbes 29.12 1 Samuel 22.17-22.19
17 Watu wa mji wakatoka, wakapigana na Yoabu; na baadhi ya watu, watumishi wa Daudi, wakaanguka; Uria Mhiti naye akafa.
Psaumes 51.14 2 Samuel 12.9
18 Ndipo Yoabu akapeleka na kumwarifu Daudi habari zote za vita;
19 akamwagiza yule mjumbe, akisema, Ukiisha kumpa mfalme habari zote za vita,
20 itakuwa, hasira ya mfalme ikiwaka, akakuambia, Kwani mliukaribia mji namna ile ili kuupiga? Je! Hamkujua ya kuwa watapiga mishale toka ukutani?
21 Ni nani aliyempiga Ahimeleki, mwana wa Yeru-beshethi? Je! Si mwanamke aliyemtupia jiwe la kusagia la juu kutoka ukutani? Hata akafa huko Thebesi? Kwani kuukaribia ukuta namna ile? Ndipo utakaposema, Mtumishi wako Uria, Mhiti, amekufa naye.
Psaumes 39.8 Ezéchiel 16.51-16.52 Esaïe 14.10 2 Samuel 3.27 Juges 9.50-9.54
22 Basi yule mjumbe akaenda, akafika na kumwonyesha Daudi yote aliyomtuma Yoabu.
23 Yule mjumbe akamwambia Daudi, Watu hao walitushinda, wakatutokea nje hata uwandani, tukashindana nao hata mahali pa kuingilia langoni.
24 Wapiga mishale wakatupiga sisi, watumishi wako, toka juu ya ukuta; na baadhi ya watumishi wa mfalme wamekufa, na Uria, Mhiti, mtumishi wako, amekufa naye.
25 Basi Daudi akamwambia yule mjumbe, Basi, mwambie Yoabu maneno haya, Jambo hili lisiwe baya machoni pako, maana upanga hula huyu kama unavyomla huyu; zidi kutia nguvu vita vyako juu ya mji ukauangushe; nawe mtie moyo.
1 Samuel 6.9 Ecclésiaste 9.11-9.12 Josué 7.8-7.9 2 Samuel 12.26 Ecclésiaste 9.1-9.3
26 Na yule mke wa Uria alipopata habari ya kuwa Uria mumewe amekufa, akamwombolezea mumewe.
Genèse 27.41 2 Samuel 14.2 2 Samuel 3.31
27 Hata maombolezo hayo yalipokwisha, Daudi akatuma mtu, akamtwaa, akamtia nyumbani mwake; naye akawa mkewe, akamzalia mwana. Lakini jambo lile alilolitenda Daudi likamchukiza Bwana.
2 Samuel 12.9 Psaumes 51.4-51.5 2 Samuel 5.13-5.16 1 Chroniques 21.7 Hébreux 13.4

Cette Bible est dans le domaine public.