Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Samuel 10.1
Bible en Swahili de l’est


Affront des Ammonites

1 Ikawa baadaye, mfalme wa wana wa Amori akafa, akamiliki Hanuni, mwanawe, mahali pake.
Juges 10.7-10.9 Juges 11.12-11.28 1 Samuel 11.1-11.3 1 Chroniques 19.1-19.19
2 Naye Daudi akasema, Nitamtendea wema Hanuni, mwana wa Nahasi, kama babaye alivyonitendea wema mimi. Basi Daudi akatuma kwa mkono wa watumishi wake, ili kumtuliza kwa habari za babaye. Wakaja watumishi wa Daudi katika nchi ya wana wa Amoni.
1 Samuel 11.1 Deutéronome 23.3-23.6 1 Samuel 22.3-22.4 Néhémie 4.3-4.7 Néhémie 13.1-13.3
3 Lakini wakuu wa wana wa Amoni wakamwambia Hanuni, bwana wao, Je! Waona ya kuwa Daudi amemheshimu babayo kwa kutuma kwako wafariji? Je! Daudi hakuwapeleka watumishi wake kwako ili kuuangalia mji, na kuupeleleza, na kuuangamiza?
Genèse 42.9 Genèse 42.16 1 Corinthiens 13.7 1 Corinthiens 13.5
4 Basi Hanuni akawatwaa hao watumishi wa Daudi, akawanyoa nusu ya ndevu zao, akawakatia nguo zao katikati, hata matakoni, akawatoa waende zao.
Esaïe 20.4 Esaïe 15.2 Jérémie 41.5 Lévitique 19.27 Psaumes 109.4-109.5
5 Watu walipomwambia Daudi habari hizo, akatuma watu kuwalaki; kwa sababu watu hao walikuwa wametahayarika sana. Mfalme akasema, Ngojeni Yeriko, hata mtakapoota ndevu zenu, ndipo mrudi.
1 Chroniques 19.5 Josué 6.24-6.26 1 Rois 16.34
6 Na wana wa Amoni walipoona ya kuwa wamekuwa machukizo kwa Daudi, wana wa Amoni wakatuma na kuwaajiri Washami wa Bethrehobu, na Washami wa Soba, askari ishirini elfu, na mfalme wa Maaka mwenye watu elfu, na watu wa Tobu watu kumi na mbili elfu.
2 Samuel 8.5 2 Samuel 8.3 Genèse 34.30 Juges 11.5 1 Samuel 27.12
7 Naye Daudi aliposikia akamtuma Yoabu, na jeshi lote la mashujaa.
2 Samuel 23.8-23.39 1 Chroniques 19.8-19.19
8 Wana wa Amoni wakatoka, wakapanga vita mahali pa kuingilia lango; na Washami wa Soba, na wa Rehobu, na watu wa Tobu, na wa Maaka, walikuwa peke yao uwandani.
2 Samuel 10.6 Josué 19.28 1 Chroniques 19.7 Juges 1.31 Nombres 13.21
9 Basi Yoabu alipoona ya kwamba uso wa vita umekuwa juu yake mbele na nyuma, akachagua baadhi ya wateule wote wa Israeli, akawapanga juu ya Washami;
Josué 8.21-8.22 Juges 20.42-20.43
10 akawatia nguvu watu waliosalia mkononi mwa Abishai, nduguye, akawapanga juu ya wana wa Amoni.
11 Akasema, Wakiwa Washami hodari mno kwangu, ndipo wewe utanisaidia, lakini wana wa Amoni wakiwa ni hodari mno kwako, ndipo mimi nitakuja nikusaidie wewe.
Philippiens 1.27-1.28 Galates 6.2 Luc 22.32 Romains 15.1 Néhémie 4.20
12 Uwe hodari, tukajitie moyo mkuu, kwa ajili ya watu wetu, na kwa ajili ya miji ya Mungu wetu; naye Bwana afanye yaliyo mema machoni pake.
Deutéronome 31.6 1 Corinthiens 16.13 1 Samuel 3.18 Juges 10.15 1 Samuel 4.9
13 Basi Yoabu na watu waliokuwa pamoja naye wakakaribia kupigana na Washami; nao wakakimbia mbele yake.
1 Rois 20.13-20.21 1 Chroniques 19.14-19.15 1 Rois 20.28-20.30 2 Chroniques 13.5-13.16
14 Na wana wa Amoni walipoona ya kwamba Washami wamekimbia, wakakimbia nao mbele ya Abishai, wakaingia mjini. Ndipo Yoabu akarudi kutoka kwa wana wa Amoni, akaja Yerusalemu.
15 Na Washami walipojiona kuwa wameshindwa mbele ya Israeli, wakakusanyika.
Zacharie 14.2-14.3 Apocalypse 19.19-19.21 Michée 4.11-4.12 Psaumes 2.1 Esaïe 8.9-8.10
16 Naye Hadadezeri akatuma na kuwaleta Washami waliokuwako ng’ambo ya Mto; nao wakaja Helamu, naye Shobaki, jemadari wa jeshi la Hadadezeri, akawaongoza.
1 Chroniques 19.16 2 Samuel 8.3-8.8 1 Chroniques 18.3 1 Chroniques 18.5
17 Alipoambiwa Daudi, akakusanya Israeli wote, akavuka Yordani, akaja Helamu. Nao Washami wakajipanga kinyume cha Daudi, wakapigana naye.
1 Chroniques 19.17
18 Wakakimbia Washami mbele ya Israeli; naye Daudi akawaua katika Washami, watu wa magari mia saba, na wapanda farasi arobaini elfu, naye akampiga huyo Shobaki, jemadari wa jeshi lao, hata akafa huko.
1 Chroniques 19.18 Juges 5.26 2 Samuel 8.4 Psaumes 18.38 Juges 4.2
19 Na wafalme wote waliomtumikia Hadadezeri walipojiona kuwa wameshindwa mbele ya Israeli, walifanya amani na Israeli, wakawatumikia. Basi Washami wakaogopa kuwasaidia wana wa Amoni tena.
2 Samuel 8.6 Apocalypse 18.10 Josué 11.10 1 Rois 20.1 Esaïe 26.11

Cette Bible est dans le domaine public.