Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 46.28
Bible en Swahili de l’est


Jacob et sa famille en Égypte

1 Akasafiri Israeli, pamoja na yote aliyokuwa nayo, akaja Beer-sheba, akamchinjia sadaka Mungu wa Isaka babaye.
Genèse 21.33 Genèse 28.13 Genèse 28.10 Genèse 31.42 Genèse 21.31
2 Mungu akanena na Israeli katika ndoto ya usiku, akasema, Yakobo, Yakobo. Akasema, Mimi hapa.
Genèse 15.1 Job 33.14-33.15 Nombres 12.6 Genèse 22.11 Genèse 22.1
3 Akasema, Mimi ni Mungu, Mungu wa baba yako, usiogope kushuka mpaka Misri; maana nitakufanya uwe taifa kubwa huko.
Deutéronome 26.5 Genèse 12.2 Genèse 35.11 Jérémie 40.9 Genèse 47.27
4 Mimi nitashuka pamoja nawe mpaka Misri; nami nitakupandisha tena bila shaka; na Yusufu ataweka mkono wake juu ya macho yako.
Genèse 28.15 Genèse 50.1 Genèse 48.21 Exode 3.8 Genèse 50.5
5 Yakobo akaondoka kutoka Beer-sheba; wana wa Israeli wakamchukua baba yao na watoto wao wadogo, na wake zao katika magari aliyoyapeleka Farao ili kumchukua.
Genèse 45.21 Genèse 45.19 Genèse 45.27 Actes 7.15 Exode 10.24
6 Wakatwaa na wanyama wao, na mali zao walizokuwa wamezipata katika nchi ya Kanaani, wakaja Misri, Yakobo na uzao wake wote pamoja naye.
Josué 24.4 Psaumes 105.23 Esaïe 52.4 Actes 7.15 Deutéronome 26.5
7 Wanawe, na wana wa wanawe, pamoja naye, binti zake na binti za wanawe, na uzao wake wote, aliwaleta pamoja naye mpaka Misri.
8 Haya ndiyo majina ya wana wa Israeli walioingia Misri, Yakobo na wanawe: Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa Yakobo.
1 Chroniques 2.1-2.55 Exode 1.1-1.5 Genèse 29.32 1 Chroniques 8.1-8.40 Genèse 29.1-29.30
9 Na wana wa Reubeni; Hanoki, na Palu, na Hesroni, na Karmi.
10 Na wana wa Simeoni; Yemueli na Yamini, na Ohadi, na Yakini, na Sohari, na Shauli, mwana wa mwanamke Mkanaani.
Exode 6.15 Genèse 29.33 Nombres 2.12-2.13 Nombres 26.12-26.13 Genèse 34.30
11 Na wana wa Lawi; Gershoni, na Kohathi, na Merari.
Genèse 29.34 1 Chroniques 2.11 1 Chroniques 2.1 Deutéronome 33.8-33.11 Nombres 4.1-4.49
12 Na wana wa Yuda; Eri, na Onani, na Shela, na Peresi, na Zera; lakini Eri na Onani walikufa katika nchi ya Kanaani. Na wana wa Peresi, ni Hesroni, na Hamuli.
1 Chroniques 4.21 Genèse 38.10 Genèse 29.35 Genèse 38.7 Juges 1.2
13 Na wana wa Isakari; Tola, na Puva, na Yashubu, na Shimroni.
Nombres 26.23-26.25 Genèse 35.23 Genèse 30.14-30.18 Deutéronome 33.18 1 Chroniques 7.1-7.5
14 Na wana wa Zabuloni; Seredi, na Eloni, na Yaleeli.
Genèse 30.19-30.20 Genèse 49.13 Deutéronome 33.18-33.19 1 Chroniques 2.1 Nombres 1.30-1.31
15 Hao ndio wana wa Lea, aliomzalia Yakobo katika Padan-aramu, na Dina, binti yake. Nafsi zote za wanawe na binti zake walikuwa thelathini na watatu.
Genèse 30.17-30.21 Genèse 29.32-29.35 Nombres 26.1-26.65 Nombres 1.1-1.54 1 Chroniques 2.1
16 Na wana wa Gadi; Sefoni, na Hagi, na Shuni, na Esboni, na Eri, na Arodi, na Areli.
Nombres 26.15-26.17 Genèse 30.11 Genèse 35.26 1 Chroniques 2.2 Nombres 1.11
17 Na wana wa Asheri; Imna, na Ishva, na Ishvi, na Beria, na Sera, umbu lao. Na wana wa Beria ni Heberi, na Malkieli.
Genèse 30.13 Nombres 1.40-1.41 Nombres 26.44-26.46 1 Chroniques 7.30-7.40 1 Chroniques 2.2
18 Hao ndio wana wa Zilpa, ambaye Labani alimpa Lea, binti yake, naye akamzalia Yakobo hao, nafsi kumi na sita.
Genèse 29.24 Genèse 30.9-30.13 Exode 1.4 Genèse 35.26
19 Wana wa Raheli, mkewe Yakobo Yusufu na Benyamini.
Genèse 44.27 Genèse 47.1-47.31 Exode 1.3 Genèse 29.18 Genèse 35.16-35.18
20 Walizaliwa kwake Yusufu katika nchi ya Misri, Manase na Efraimu, aliomzalia Asenathi binti Potifera, kuhani wa Oni.
Genèse 41.50-41.52 Genèse 41.45 Genèse 48.13-48.14 Deutéronome 33.13-33.17 Nombres 26.28-26.37
21 Na wana wa Benyamini; Bela, na Bekeri, na Ashbeli, na Gera, na Naamani, na Ehi, na Roshi, na Mupimu, na Hupimu, na Ardi.
1 Chroniques 7.6-7.12 1 Chroniques 8.1-8.7 Nombres 26.38-26.40 Genèse 49.27 Nombres 1.11
22 Hao ndio wana wa Raheli, aliomzalia Yakobo, nafsi zote walikuwa kumi na wanne.
23 Na wana wa Dani; Hushimu.
Deutéronome 33.22 Nombres 1.38-1.39 1 Chroniques 2.2 Nombres 10.25 1 Chroniques 7.12
24 Na wana wa Naftali; Yaseeli, na Guni, na Yaseri, na Shilemu.
1 Chroniques 7.13 2 Rois 15.29 Nombres 26.48-26.50 Deutéronome 33.23 Nombres 1.42-1.43
25 Hao ndio wana wa Bilha, ambaye Labani alimpa Raheli, binti yake, naye akamzalia Yakobo hao; nafsi zote walikuwa saba.
Genèse 29.29 Exode 1.2 Genèse 35.25 Genèse 30.3-30.8 Genèse 35.22
26 Nafsi zote waliokuja pamoja na Yakobo mpaka Misri waliotoka viunoni mwake, bila wake za wanawe Yakobo, nafsi zote walikuwa sitini na sita.
Exode 1.5 Juges 8.30 Genèse 35.11
27 Na wana wa Yusufu aliozaliwa katika Misri walikuwa nafsi wawili. Nafsi zote za nyumba ya Yakobo walioingia Misri walikuwa sabini.
Actes 7.14 Exode 1.5 Deutéronome 10.22 Exode 24.1
28 Yakobo akampeleka Yuda mbele yake kwa Yusufu, ili amwongoze njia mpaka Gosheni. Wakaja mpaka nchi ya Gosheni.
Genèse 45.10 Genèse 31.21 Genèse 43.8 Genèse 46.34-47.1 Genèse 49.8
29 Yusufu akatandika gari lake, akapanda kwenda kumlaki Israeli, babaye, huko Gosheni; akajionyesha kwake, akamwangukia shingoni, akalia shingoni mwake kitambo kizima.
Luc 15.20 Genèse 41.43 Genèse 45.14-45.15 Genèse 33.4 Genèse 45.19
30 Israeli akamwambia Yusufu, Na nife sasa, kwa kuwa nimekuona uso wako, ya kuwa ungali hai.
Luc 2.29-2.30 Genèse 45.28
31 Yusufu akawaambia ndugu zake na watu wa nyumbani mwa baba yake, Nitapanda mimi nimpashe Farao habari; nitamwambia, Ndugu zangu, na watu wa nyumbani mwa baba yangu, waliokuwa katika nchi ya Kanaani, wamenijia.
Hébreux 2.11 Genèse 45.16-45.20 Genèse 47.1-47.3 Actes 18.3
32 Na watu hao ni wachungaji, maana wamekuwa watu wa kuchunga wanyama, nao wameleta kondoo zao, na ng’ombe zao, na yote waliyo nayo.
Genèse 47.3 Esaïe 40.11 Genèse 9.20 1 Samuel 17.15 Psaumes 78.70-78.72
33 Itakuwa Farao atakapowaita, na kuwauliza, Kazi yenu ni nini?
Genèse 46.32 Jonas 1.8 Genèse 47.2-47.4
34 Semeni, Watumwa wako tumekuwa wachunga wanyama tangu ujana wetu, na hata leo, sisi, na baba zetu; mpate kukaa katika nchi ya Gosheni; maana kila mchunga wanyama ni chukizo kwa Wamisri.
Exode 8.26 Genèse 43.32 Genèse 46.32 Genèse 37.12 Genèse 34.5

Cette Bible est dans le domaine public.