Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 22.7
Bible en Swahili de l’est


Mise à l’épreuve d’Abraham

1 Ikawa baada ya mambo hayo Mungu alimjaribu Ibrahimu, akamwambia, Ee Ibrahimu! Naye akasema, Mimi hapa.
Hébreux 11.17 Deutéronome 8.2 Genèse 22.11 Jacques 2.21 Esaïe 6.8
2 Akasema, Umchukue mwanao, mwana wako wa pekee, umpendaye, Isaka, ukaende zako mpaka nchi ya Moria, ukamtoe sadaka ya kuteketezwa huko juu ya mlima mmojawapo nitakaokuambia.
Hébreux 11.17 Jean 3.16 1 Jean 4.9-4.10 2 Chroniques 3.1 Romains 8.32
3 Ibrahimu akaondoka alfajiri, akatandika punda wake, akachukua vijana wawili pamoja naye, na Isaka mwanawe, akachanja kuni kwa ajili ya hiyo sadaka ya kuteketezwa, akaondoka, akaenda mpaka mahali alipoambiwa na Mungu.
Psaumes 119.60 Luc 14.26 Hébreux 11.17-11.19 Ecclésiaste 9.10 Hébreux 11.8
4 Siku ya tatu Ibrahimu akainua macho yake, akapaona mahali pakali mbali.
Nombres 19.19 Nombres 10.33 Esther 5.1 Exode 5.3 Exode 15.22
5 Ibrahimu akawaambia vijana wake, Kaeni ninyi hapa pamoja na punda, na mimi na kijana tutakwenda kule, tukaabudu, na kuwarudia tena.
Hébreux 12.1 Hébreux 11.19
6 Basi Ibrahimu akazitwaa kuni za hiyo sadaka, akamtwika Isaka mwanawe; akatwaa moto na kisu mkononi mwake, wakaenda wote wawili pamoja.
Jean 19.17 Luc 24.26-24.27 Esaïe 53.6 1 Pierre 2.24 Matthieu 8.17
7 Isaka akasema na Ibrahimu baba yake, akinena, Babangu! Naye akasema, Mimi hapa, mwanangu. Akasema, Tazama! Moto upo, na kuni zipo, lakini yuko wapi mwana-kondoo kwa sadaka ya kuteketezwa?
Romains 8.15 Matthieu 26.42 Exode 12.3 Genèse 8.20 Matthieu 26.39
8 Ibrahimu akasema, Mungu atajipatia mwana-kondoo kwa hiyo sadaka, mwanangu. Basi wakaendelea wote wawili pamoja.
Jean 1.36 Jean 1.29 Apocalypse 5.12 Apocalypse 13.8 Genèse 18.14
9 Wakafika mahali pale alipoambiwa na Mungu, Ibrahimu akajenga madhabahu huko, akaziweka tayari kuni, kisha akamfunga Isaka mwanawe, akamweka juu ya madhabahu, juu ya zile kuni.
Jacques 2.21 Philippiens 2.7-2.8 Matthieu 27.2 Matthieu 21.1-21.46 Actes 8.32
10 Ibrahimu akanyosha mkono wake, akakitwaa kisu ili amchinje mwanawe.
Esaïe 53.6-53.12 Jacques 2.21-2.23 Hébreux 11.17-11.19
11 Ndipo malaika wa Bwana akamwita kutoka mbinguni, akasema, Ibrahimu! Ibrahimu! Naye akasema, Mimi hapa.
Exode 3.4 Genèse 16.9-16.10 1 Samuel 3.10 Genèse 16.7 Actes 9.4
12 Akasema, Usimnyoshee kijana mkono wako, wala usimtendee neno; kwa maana sasa ninajua ya kuwa unamcha Mungu, iwapo hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee.
1 Samuel 15.22 Jacques 2.21-2.22 Jacques 2.18 Genèse 26.5 Genèse 20.11
13 Ibrahimu akainua macho yake, akaangalia, na tazama, kondoo mume yuko nyuma yake, amenaswa pembe zake katika kichaka. Basi Ibrahimu akaenda akamtwaa huyo kondoo, akamtoa awe sadaka ya kuteketezwa badala ya mwanawe.
1 Corinthiens 10.13 Psaumes 40.6-40.8 Genèse 22.8 1 Pierre 1.19-1.20 Esaïe 30.21
14 Ibrahimu akapaita mahali hapo Yehova-yire,kama watu wasemavyo hata leo,Katika mlima wa BWANA itapatikana.
Genèse 22.8 Exode 17.15 Genèse 16.13-16.14 Ezéchiel 48.35 Psaumes 22.4-22.5
15 Malaika wa Bwana akamwita Ibrahimu mara ya pili kutoka mbinguni
16 akasema, Nimeapa kwa nafsi yangu asema Bwana, kwa kuwa umetenda neno hili, wala hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee,
Psaumes 105.9 Luc 1.73 Jérémie 49.13 Genèse 12.2 Romains 4.13-4.14
17 katika kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha nitauzidisha uzao wako kama nyota za mbinguni, na kama mchanga ulioko pwani; na uzao wako utamiliki mlango wa adui zao;
Genèse 15.5 Genèse 24.60 Genèse 13.16 Genèse 26.4 Jérémie 33.22
18 na katika uzao wako mataifa yote ya dunia watajibarikia; kwa sababu umetii sauti yangu.
Actes 3.25 Genèse 12.3 Genèse 18.18 Galates 3.16 Genèse 26.4-26.5
19 Basi Ibrahimu akawarudia vijana wake, wakaondoka, wakaenda zao pamoja mpaka Beer-sheba; Ibrahimu akakaa huko Beer-sheba.
Genèse 21.31 Juges 20.1 Josué 15.28
20 Ikawa baada ya mambo hayo, Ibrahimu akaambiwa ya kwamba, Tazama, Milka naye amemzalia Nahori ndugu yako wana;
Genèse 11.29 Genèse 24.24 Genèse 24.10 Genèse 31.53 Genèse 24.15
21 Usi, mzaliwa wa kwanza wake, na Buzi nduguye, na Kemueli, baba wa Aramu;
Job 1.1 Genèse 24.10 Job 32.2 Nombres 23.7 Psaumes 60.1-60.12
22 na Kesedi, na Hazo, na Pildashi, na Yidlafu, na Bethueli.
23 Bethueli akamzaa Rebeka; hao wanane Milka alimzalia Nahori ndugu wa Ibrahimu.
Genèse 24.15 Genèse 25.20 Genèse 24.60 Genèse 24.67 Genèse 24.51
24 Na suria wake Reuma naye alizaa Teba na Gahamu na Tahashi na Maaka.
Proverbes 15.25 Genèse 25.6 Genèse 16.3

Cette Bible est dans le domaine public.