Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 17.15
Bible en Swahili de l’est


Alliance de Dieu avec Abraham

1 Abramu alipokuwa mtu wa miaka tisini na kenda, Bwana akamtokea Abramu, akamwambia, Mimi ni Mungu Mwenyezi, uende mbele yangu, ukawe mkamilifu.
Deutéronome 18.13 Genèse 6.9 Job 1.1 Matthieu 5.48 Luc 1.6
2 Nami nitafanya agano langu kati ya mimi na wewe, nami nitakuzidisha sana sana.
Genèse 15.18 Genèse 13.16 Genèse 12.2 Genèse 17.4-17.6 Genèse 22.17
3 Abramu akaanguka kifudifudi. Mungu akamwambia, akasema,
Genèse 17.17 Exode 3.6 Josué 5.14 Nombres 16.45 Nombres 14.5
4 Mimi, agano langu nimefanya nawe, nawe utakuwa baba wa mataifa mengi,
Genèse 35.11 Genèse 12.2 Nombres 1.1-1.54 Genèse 48.19 Romains 4.11-4.18
5 wala jina lako hutaitwa tena Abramu, lakini jina lako litakuwa Ibrahimu, kwani nimekuweka uwe baba wa mataifa mengi.
Néhémie 9.7 Genèse 17.15 Genèse 32.28 Romains 4.17 Esaïe 62.2-62.4
6 Nitakufanya uwe na uzao mwingi sana, nami nitakufanya kuwa mataifa, na wafalme watatoka kwako.
Genèse 35.11 Genèse 17.16 Genèse 17.4 Genèse 17.20 Matthieu 1.6-1.17
7 Agano langu nitalifanya imara kati ya mimi na wewe, na uzao wako baada yako, na vizazi vyao, kuwa agano la milele, kwamba nitakuwa Mungu kwako na kwa uzao wako baada yako.
Genèse 26.24 Hébreux 11.16 Genèse 28.13 Lévitique 26.12 Genèse 15.18
8 Nami nitakupa wewe na uzao wako baada yako nchi hii unayoikaa ugeni, nchi yote ya Kanaani, kuwa milki ya milele; nami nitakuwa Mungu wao.
Genèse 12.7 Lévitique 26.12 Genèse 13.15 Psaumes 105.11 Deutéronome 29.13
9 Mungu akamwambia Ibrahimu, Nawe ulishike agano langu, wewe na uzao wako kwa vizazi vyao baada yako.
Psaumes 103.18 Psaumes 25.10 Esaïe 56.4-56.5
10 Hili ndilo agano langu utakalolishika, kati ya mimi na wewe, na uzao wako baada yako, Kila mwanamume wa kwenu atatahiriwa.
Actes 7.8 Colossiens 2.11-2.12 Genèse 17.11 Josué 5.2 Galates 5.3-5.6
11 Mtatahiriwa nyama ya magovi yenu, na jambo hilo litakuwa ishara ya agano kati ya mimi na ninyi.
Romains 4.11 Actes 7.8 Deutéronome 10.16 Exode 4.25 Josué 5.3
12 Mtoto wa siku nane atatahiriwa kwenu, kila mwanamume katika vizazi vyenu, mzaliwa nyumbani, na mnunuliwa kwa fedha, kila mgeni asiyekuwa wa uzao wako.
Lévitique 12.3 Luc 2.21 Luc 1.59 Exode 12.48-12.49 Philippiens 3.5
13 Mzaliwa nyumbani mwako, na mnunuliwa kwa fedha yako, lazima atahiriwe; na agano langu litakuwa katika mwili wenu, kuwa agano la milele.
Exode 12.44 Néhémie 5.5 Exode 21.16 Matthieu 18.25 Genèse 39.1
14 Na mwanamume mwenye govi asiyetahiriwa nyama ya govi lake, mtu yule atatengwa na watu wake; amelivunja agano langu.
Exode 4.24-4.26 Lévitique 19.8 Psaumes 55.20 Josué 5.2-5.12 Lévitique 18.29
15 Mungu akamwambia Ibrahimu, Sarai mkeo, hutamwita jina lake Sarai, kwa kuwa jina lake litakuwa Sara.
2 Samuel 12.25 Genèse 17.5 Genèse 32.28
16 Nami nitambariki, na tena nitakupa mwana kwake, naam, nitambariki, naye atakuwa mama wa mataifa, na wafalme wa kabila za watu watatoka kwake.
Genèse 35.11 Genèse 17.6 Genèse 1.28 Romains 9.9 Esaïe 49.23
17 Ndipo Ibrahimu akaanguka kifudifudi akacheka, akasema moyoni, Je! Mtu wa umri wa miaka mia, kwake atazaliwa mtoto? Naye Sara mwenye umri wa miaka tisini atazaa?
Genèse 21.6 Genèse 18.12 Genèse 17.3 Jean 8.56 Ezéchiel 1.28
18 Ibrahimu akamwambia Mungu, Lau kwamba Ishmaeli angeishi mbele yako.
Psaumes 41.12 Actes 2.39 Jérémie 32.39 Esaïe 59.2 Psaumes 4.6
19 Mungu akasema, Sivyo, lakini Sara mkeo atakuzalia mwana wa kiume, nawe utamwita jina lake Isaka. Nami nitafanya agano langu imara kwake kuwa agano la milele kwa ajili ya uzao wake baada yake.
Genèse 21.2-21.3 Genèse 21.6 Romains 9.6-9.9 Luc 1.13-1.20 Galates 4.28-4.31
20 Na kwa habari za Ishmaeli nimekusikia, nimembariki, nitamzidisha, nami nitamwongeza sana sana. Atazaa maseyidi kumi na wawili, nami nitamfanya awe taifa kuu.
Genèse 21.18 Genèse 21.13 Genèse 16.10-16.12 Genèse 25.12-25.18
21 Bali agano langu nitalifanya imara kwa Isaka, ambaye Sara atakuzalia majira kama haya mwaka ujao.
Genèse 26.2-26.5 Genèse 18.10 Genèse 21.10-21.12 Genèse 21.2-21.3 Genèse 48.15
22 Mungu akaacha kusema naye, akapanda kutoka kwa Ibrahimu.
Genèse 18.33 Jean 1.18 Exode 20.22 Genèse 17.3 Jean 10.30
23 Ibrahimu akamtwaa Ishmaeli mwanawe, na wote waliozaliwa nyumbani mwake, na wote walionunuliwa kwa fedha yake, wanaume wote wa watu wa nyumba ya Ibrahimu, akawatahiri nyama ya magovi yao siku ile ile, kama Mungu alivyomwambia.
Genèse 17.10-17.14 Proverbes 27.1 Galates 5.6 Galates 6.15 Genèse 34.24
24 Naye Ibrahimu alikuwa mwenye umri wa miaka tisini na kenda alipotahiriwa nyama ya govi lake.
Romains 4.11 Genèse 12.4 Genèse 17.1 Genèse 17.17 Romains 4.19-4.20
25 Na Ishmaeli mwanawe alikuwa mtu wa miaka kumi na mitatu, alipotahiriwa nyama ya govi lake.
26 Siku ile ile akatahiriwa Ibrahimu na Ishmaeli mwanawe.
Genèse 22.3-22.4 Genèse 12.4 Psaumes 119.60
27 Na watu wote wa nyumba yake, wazaliwa nyumbani, na wanunuliwa kwa fedha katika mkono wa mgeni, wakatahiriwa pamoja naye.
Genèse 18.19

Cette Bible est dans le domaine public.