Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 10.2
Bible en Swahili de l’est


Descendance des fils de Noé

1 Hivi ndivyo vizazi vya wana wa Nuhu, Shemu, na Hamu, na Yafethi. Na kwao walizaliwa wana wa kiume baada ya gharika.
Genèse 2.4 Matthieu 1.1 Genèse 9.19 Genèse 5.1 Genèse 6.9
2 Wana wa Yafethi ni Gomeri, na Magogu, na Madai, na Yavani, na Tubali, na Mesheki, na Tirasi.
Ezéchiel 38.2 Ezéchiel 38.6 Apocalypse 20.8 Esaïe 66.19 1 Chroniques 1.5-1.7
3 Na wana wa Gomeri ni Ashkenazi, na Rifathi, na Togama.
Jérémie 51.27 Ezéchiel 27.14
4 Na wana wa Yavani ni Elisha, Tarshishi, Kitimu, na Warodani.
Esaïe 23.12 Esaïe 23.1 Nombres 24.24 Daniel 11.30 Ezéchiel 27.12
5 Kwa hao nchi za pwani za mataifa ziligawanyikana kuwa nchi zao, kila moja kwa lugha yake, kwa jamaa zao, kufuata mataifa yao.
Genèse 10.20 Jérémie 2.10 Jérémie 25.22 Sophonie 2.11 Psaumes 72.10
6 Na wana wa Hamu ni Kushi, na Misri, na Putu, na Kanaani.
1 Chroniques 1.8-1.16 Psaumes 106.22 Psaumes 105.23 Psaumes 78.51 Jérémie 46.9
7 Na wana wa Kushi ni Seba, na Havila, na Sabta, na Raama, na Sabteka. Na wana wa Raama ni Sheba, na Dedani.
Ezéchiel 27.22 Ezéchiel 27.15 1 Rois 10.1 Genèse 2.11 Psaumes 72.10
8 Kushi akamzaa Nimrodi, akaanza kuwa mtu hodari katika nchi.
Michée 5.6
9 Alikuwa hodari kuwinda wanyama mbele za Bwana. Kwa hiyo watu hunena, Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda wanyama mbele za Bwana.
Genèse 27.30 Genèse 6.11 Ezéchiel 13.18 Genèse 6.4 Genèse 13.13
10 Mwanzo wa ufalme wake ulikuwa Babeli na Ereku, na Akadi, na Kalne, katika nchi ya Shinari.
Genèse 11.9 Genèse 11.2 Genèse 14.1 Esaïe 39.1 Esaïe 11.11
11 Akatoka katika nchi ile akaenda mpaka Ashuru, akajenga Ninawi, na Rehoboth-iri, na Kala;
Michée 5.6 Nahum 1.1 Psaumes 83.8 Jonas 1.2 Esaïe 37.37
12 na Reseni, kati ya Ninawi na Kala, nao ni mji mkubwa.
13 Misri akazaa Waludi, na Waanami, na Walehabi, na Wanaftuhi,
1 Chroniques 1.11-1.12 Jérémie 46.9 Ezéchiel 30.5
14 na Wapathrusi, na Wakasluhi; huko ndiko walikotoka Wafilisti na Wakaftori.
Jérémie 47.4 1 Chroniques 1.12 Deutéronome 2.23 Amos 9.7 Jérémie 44.1
15 Kanaani akamzaa Sidoni, mwanawe wa kwanza, na Hethi,
1 Chroniques 1.13 Genèse 15.18-15.21 Genèse 28.3-28.20 Esaïe 23.4 Nombres 34.2-34.15
16 na Myebusi, na Mwamori, na Mgirgashi,
Zacharie 9.7 Juges 1.21 2 Samuel 24.18
17 na Mhivi, na Mwarki, na Msini,
Genèse 34.2
18 na Mwarvadi, na Msemari, na Mhamathi. Baadaye jamaa za Wakanaani walitawanyikana.
Nombres 34.8 Ezéchiel 47.16-47.17 2 Chroniques 13.4 Ezéchiel 27.8 2 Rois 17.30
19 Na mpaka wa Wakanaani ulianza kutoka Sidoni kwa njia ya Gerari hata Gaza; tena kwa njia ya Sodoma, na Gomora, na Adma, na Seboimu, hata Lasha.
Genèse 14.2 Genèse 13.10-13.17 Genèse 19.24-19.25 Genèse 26.1 Jérémie 25.20
20 Hao ndio wana wa Hamu, kufuata jamaa zao, kwa lugha zao, katika nchi zao, kufuata mataifa yao.
Genèse 10.6 Genèse 11.1-11.9
21 Naye Shemu ambaye ni baba wa wana wote wa Eberi, na ndugu mkubwa wa Yafethi, akazaliwa wana.
Nombres 24.24 Genèse 11.10-11.26
22 Wana wa Shemu ni Elamu, na Ashuru, na Arfaksadi, na Ludi, na Aramu.
Esaïe 66.19 Actes 2.9 Esaïe 11.11 Nombres 23.7 Jérémie 49.34-49.39
23 Na wana wa Aramu ni Usi, na Huli, na Getheri, na Mashi.
Job 1.1 Jérémie 25.20
24 Arfaksadi akamzaa Sela, Sela akamzaa Eberi.
Luc 3.35 Genèse 11.12-11.15
25 Eberi akazaliwa wana wawili wa kiume; jina la wa kwanza ni Pelegi maana katika siku zake nchi iligawanyika; na jina la nduguye ni Yoktani.
1 Chroniques 1.19 Genèse 11.16-11.19 Genèse 10.32 Actes 17.26 Genèse 10.21
26 Yoktani akamzaa Almodadi, na Shelefu, na Hasarmawethi, na Yera,
1 Chroniques 1.20-1.28
27 na Hadoramu, na Uzali, na Dikla,
1 Chroniques 1.20-1.28
28 na Obali, na Abimaeli, na Seba,
1 Rois 10.1 Genèse 25.3 1 Chroniques 1.20-1.28
29 na Ofiri, na Havila, na Yobabi. Hao wote ndio wana wa Yoktani.
1 Rois 9.28 1 Samuel 15.7 Job 28.16 Genèse 2.11 1 Rois 22.48
30 Makao yao yalikuwa kutoka Mesha kwa njia ya Sefari, mlima wa mashariki.
Nombres 23.7
31 Hao ndio wana wa Shemu, kufuata jamaa zao, na lugha zao, katika nchi zao, kufuata mataifa yao.
Genèse 10.20 Genèse 10.5 Actes 17.26
32 Hizo ndizo jamaa za wana wa Nuhu, kufuata vizazi vyao, katika mataifa yao; na kwa hao mataifa yaligawanyika katika nchi baada ya gharika.
Genèse 9.19 Genèse 10.1 Genèse 5.29-5.31 Genèse 10.25 Genèse 10.20

Cette Bible est dans le domaine public.