Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 1.26
Bible en Swahili de l’est


La création

Création du ciel et de la terre

1 Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi.
Hébreux 11.3 Esaïe 45.18 Jean 1.1-1.3 Job 38.4 Esaïe 42.5
2 Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.
Jérémie 4.23 Psaumes 104.30 Esaïe 45.18
3 Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru.
2 Corinthiens 4.6 Jean 1.5 Psaumes 33.6 1 Jean 1.5 Esaïe 45.7
4 Mungu akaiona nuru, ya kuwa ni njema; Mungu akatenga nuru na giza.
Genèse 1.18 Genèse 1.12 Ecclésiaste 2.13 Genèse 1.31 Genèse 1.25
5 Mungu akaiita nuru Mchana, na giza akaliita Usiku. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku moja.
Psaumes 74.16 Esaïe 45.7 Psaumes 104.20 Jérémie 33.20 Psaumes 19.2
6 Mungu akasema, Na liwe anga katikati ya maji, likayatenge maji na maji.
Jérémie 51.15 Psaumes 104.2 Job 37.18 Job 26.7-26.8 Psaumes 33.6
7 Mungu akalifanya anga, akayatenga yale maji yaliyo juu ya anga na yale maji yaliyo chini ya anga; ikawa hivyo.
Psaumes 148.4 Proverbes 8.28-8.29 Genèse 1.11 Job 38.8-38.11 Genèse 1.15
8 Mungu akaliita lile anga Mbingu. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya pili.
Genèse 1.5 Genèse 1.19
9 Mungu akasema, Maji yaliyo chini ya mbingu na yakusanyike mahali pamoja, ili pakavu paonekane; ikawa hivyo.
2 Pierre 3.5 Jérémie 5.22 Psaumes 95.5 Psaumes 33.7 Apocalypse 10.6
10 Mungu akapaita pale pakavu Nchi; na makusanyiko ya maji akayaita Bahari; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.
11 Mungu akasema, Nchi na itoe majani, mche utoao mbegu, na mti wa matunda uzaao matunda kwa jinsi yake, ambao mbegu zake zimo ndani yake, juu ya nchi; ikawa hivyo.
Hébreux 6.7 Psaumes 147.8 Psaumes 65.9-65.13 Matthieu 6.30 Psaumes 104.14-104.17
12 Nchi ikatoa majani, mche utoao mbegu kwa jinsi yake, na mti uzaao matunda, ambao mbegu zake zimo ndani yake, kwa jinsi yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.
Marc 4.28 Esaïe 61.11 Esaïe 55.10-55.11 2 Corinthiens 9.10 Luc 6.44
13 Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya tatu.
14 Mungu akasema, Na iwe mianga katika anga la mbingu ili itenge kati ya mchana na usiku; nayo iwe ndiyo dalili na majira na siku na miaka;
Psaumes 136.7-136.9 Psaumes 74.16-74.17 Jérémie 31.35 Esaïe 40.26 Psaumes 8.3-8.4
15 tena iwe ndiyo mianga katika anga la mbingu itie nuru juu ya nchi; ikawa hivyo.
16 Mungu akafanya mianga miwili mikubwa, ule mkubwa utawale mchana, na ule mdogo utawale usiku; akafanya na nyota pia.
Psaumes 8.3 Psaumes 148.5 Esaïe 40.26 Psaumes 136.7-136.9 Deutéronome 4.19
17 Mungu akaiweka katika anga la mbingu, itie nuru juu ya nchi
Psaumes 8.3 Psaumes 8.1 Genèse 9.13 Actes 13.47 Job 38.12
18 na kuutawala mchana na usiku na kutenga nuru na giza; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.
Jérémie 31.35 Psaumes 19.6
19 Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya nne.
20 Mungu akasema, Maji na yajawe kwa wingi na kitu kiendacho chenye uhai, na ndege waruke juu ya nchi katika anga la mbingu.
Genèse 2.19 Psaumes 104.24-104.25 Psaumes 148.10 Genèse 1.22 Genèse 8.17
21 Mungu akaumba nyangumi wakubwa, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho, ambavyo maji yalijawa navyo kwa wingi kwa jinsi zao, na kila ndege arukaye, kwa jinsi yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.
Psaumes 104.24-104.26 Genèse 1.25 Jonas 2.10 Matthieu 12.40 Genèse 6.20
22 Mungu akavibarikia, akisema, Zaeni, mkaongezeke, mkayajaze maji ya baharini, ndege na wazidi katika nchi.
Genèse 8.17 Genèse 1.28 Psaumes 107.38 Job 42.12 Genèse 9.1
23 Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya tano.
24 Mungu akasema, Nchi na izae kiumbe hai kwa jinsi zake, mnyama wa kufugwa, nacho kitambaacho, na wanyama wa mwitu kwa jinsi zake; ikawa hivyo.
Job 40.15 Psaumes 50.9-50.10 Genèse 6.20 Genèse 8.19 Genèse 7.14
25 Mungu akafanya mnyama wa mwitu kwa jinsi zake, na mnyama wa kufugwa kwa jinsi zake, na kila kitu kitambaacho juu ya nchi kwa jinsi yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.
Jérémie 27.5 Job 12.8-12.10 Genèse 2.19-2.20 Job 26.13

Création de l’être humain et repos

26 Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.
Colossiens 3.10 Ephésiens 4.24 Jacques 3.9 Genèse 3.22 2 Corinthiens 3.18
27 Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba.
Matthieu 19.4 Marc 10.6 Ephésiens 2.10 Genèse 5.1-5.2 Esaïe 43.7
28 Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi.
Genèse 9.7 Genèse 9.1 Lévitique 26.9 Esaïe 45.18 1 Chroniques 4.10
29 Mungu akasema, Tazama, nimewapa kila mche utoao mbegu, ulio juu ya uso wa nchi yote pia, na kila mti, ambao matunda yake yana mbegu; vitakuwa ndivyo chakula chenu;
Genèse 9.3 Psaumes 145.15-145.16 Psaumes 136.25 Actes 17.28 Psaumes 104.14-104.15
30 na chakula cha kila mnyama wa nchi, na cha kila ndege wa angani, na cha kila kitu kitambaacho juu ya nchi, chenye uhai; majani yote ya miche, ndiyo chakula chenu; ikawa hivyo.
Psaumes 147.9 Psaumes 104.14 Psaumes 145.15-145.16 Genèse 9.3 Job 38.39-38.41
31 Mungu akaona kila kitu alichokifanya, na tazama, ni chema sana. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya sita.
1 Timothée 4.4 Psaumes 104.24 Exode 20.11 Psaumes 104.31 Genèse 2.2

Cette Bible est dans le domaine public.