Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Juges 2.6
Bible en Swahili de l’est


Constat d’échec et mort de Josué

1 Kisha malaika wa Bwana alikwea juu kutoka Gilgali kwenda Bokimu. Akasema, Mimi nimewaleta ninyi mkwee juu kutoka nchi ya Misri, nami nimewaleta hata nchi niliyowaapia baba zenu; nami nilisema, Mimi milele sitalivunja hilo agano langu nililoagana nanyi;
Lévitique 26.42 Genèse 17.7-17.8 Exode 20.2 Genèse 12.7 Juges 2.5
2 nanyi msifanye agano lo lote na hawa wenyeji wa nchi hii; zipomosheni nchi madhabahu zao; lakini hamkuisikia sauti yangu; je! Mmefanya haya kwa sababu gani?
Deutéronome 7.2-7.4 1 Pierre 4.17 Esdras 9.1-9.3 Psaumes 78.55-78.58 Genèse 4.10
3 Basi kwa ajili ya hayo mimi nilisema zaidi, Mimi sitawafukuza watoke mbele zenu; lakini watakuwa kama miiba mbavuni mwenu, na miungu yao itakuwa ni tanzi kwenu.
Nombres 33.55 Josué 23.13 Psaumes 106.36 Juges 3.6 Juges 2.21
4 Ikawa, hapo huyo malaika wa Bwana alipoyanena maneno haya, kuwaambia wana wa Israeli wote, ndipo hao watu wakainua sauti zao na kulia.
Zacharie 12.10 Jacques 4.9 Jérémie 31.9 Luc 6.21 Luc 7.38
5 Nao wakaliita jina la mahali pale Bokimu; nao wakamchinjia Bwana sadaka huko.
Genèse 35.8 Juges 6.24 Juges 13.19 Josué 7.26 1 Samuel 7.9
6 Basi hapo Yoshua alipowapa watu ruhusa waende zao, wana wa Israeli wakaenda kila mtu kuuendea urithi wake, ili kuimiliki hiyo nchi.
Josué 24.28-24.31 Josué 22.6
7 Watu hao wakamtumikia Bwana siku zote za Yoshua, na siku zote za hao wazee walioendelea siku zao baada ya Yoshua, hao waliokuwa wameiona hiyo kazi kubwa ya Bwana yote, aliyokuwa ameitenda kwa ajili ya Israeli.
Josué 24.31 2 Chroniques 24.2 Philippiens 2.12 2 Rois 12.2 2 Chroniques 24.14-24.22
8 Kisha Yoshua mwana wa Nuni, mtumishi wa Bwana, akafa, naye alipata umri wa miaka mia na kumi.
Josué 24.29-24.30
9 Nao wakamzika katika mpaka wa urithi wake katika Timnath-heresi, katika nchi ya vilima vilima ya Efraimu, upande wa kaskazini wa mlima wa Gaashi.
Josué 19.50 Josué 24.30

Attitude de la nouvelle génération

10 Tena watu wote wa kizazi hicho nao walikusanywa waende kwa baba zao; kikainuka kizazi kingine nyuma yao, ambacho hakikumjua Bwana, wala hawakuijua hiyo kazi ambayo alikuwa ameitenda kwa ajili ya Israeli.
1 Samuel 2.12 Exode 5.2 1 Chroniques 28.9 Deutéronome 31.16 Tite 1.16
11 Wana wa Israeli walifanya yaliyokuwa ni maovu mbele za macho ya Bwana, nao wakawatumikia Mabaali.
Juges 10.6 Juges 6.1 Juges 4.1 Juges 3.7 Juges 8.33
12 Wakamwacha Bwana, Mungu wa baba zao, aliyewaleta kutoka katika nchi ya Misri, wakafuata miungu mingine, baadhi ya miungu ya watu wale waliokaa karibu nao pande zote, wakajiinamisha mbele yao; wakamkasirisha Bwana, akaghadhibika.
Exode 20.5 Deutéronome 29.25 Deutéronome 13.5 Deutéronome 29.18 Deutéronome 6.14-6.15
13 Wakamwacha Bwana, wakamtumikia Baali na Maashtorethi.
Juges 10.6 Juges 3.7 Psaumes 106.36 1 Rois 11.33 1 Samuel 31.10
14 Hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli, naye akawatia katika mikono ya watu waliowateka nyara, akawauza na kuwatia katika mikono ya adui zao pande zote; hata wasiweze tena kusimama mbele ya adui zao.
Deutéronome 32.30 Psaumes 106.40-106.42 Juges 4.2 Lévitique 26.37 Josué 7.12-7.13
15 Kila walikokwenda mkono wa Bwana ulikuwa juu yao kuwatenda mabaya, kama Bwana alivyosema, na kama Bwana alivyowaapia; nao wakafadhaika sana.
Deutéronome 28.15-28.68 Lévitique 26.14-26.46 Michée 2.3 Jérémie 44.27 1 Samuel 14.24
16 Kisha Bwana akawainua waamuzi, waliowaokoa na mikono ya watu hao waliowateka nyara.
Actes 13.20 Juges 3.15 Néhémie 9.27 Psaumes 106.43-106.45 1 Samuel 12.11
17 Lakini hawakuwasikiliza hao waamuzi wao, maana walifanya uasherati kwa kuifuata miungu mingine, wakajiinamisha mbele yao; wakageuka upesi, na kuiacha njia ile waliyoiendea baba zao, waliozitii amri za Bwana bali wao hawakufanya hivyo.
Juges 2.7 Deutéronome 9.12 Psaumes 106.43 Psaumes 106.39 2 Chroniques 36.15-36.16
18 Na wakati Bwana alipowainulia waamuzi, ndipo Bwana alikuwa pamoja na mwamuzi huyo, akawaokoa na mikono ya adui zao siku zote za mwamuzi huyo; maana Bwana alighairi kwa ajili ya kuugua kwao kwa sababu ya watu wale waliowaonea na kuwasumbua.
Josué 1.5 Deutéronome 32.36 Exode 2.24 Psaumes 106.44-106.45 Genèse 6.6
19 Lakini ikawa, wakati alipokufa mwamuzi huyo, wakarudi nyuma wakafanya maovu kuliko baba zao, kwa kuifuata miungu mingine ili kuitumikia, na kuinama mbele yao; hawakuacha matendo yao, wala njia zao za ukaidi.
Juges 4.1 Juges 8.33 Matthieu 23.32 Juges 3.11-3.12 Jérémie 16.12
20 Basi hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli, naye akasema, Kwa kuwa taifa hili wamelihalifu agano langu nililowaamuru baba zao, wala hawakuisikiliza sauti yangu;
Juges 2.14 Josué 23.16 Deutéronome 29.10-29.13 Exode 24.3-24.8 Ezéchiel 20.37
21 mimi nami tokea sasa sitalifukuza taifa mojawapo la hayo aliyoyaacha Yoshua alipokufa;
Josué 23.13 Juges 2.3 Juges 3.3 Ezéchiel 20.24
22 ili kwa njia ya hayo nipate kuwajaribu Israeli, kwamba wataishika njia ya Bwana kwenda katika njia hiyo, au sivyo.
Deutéronome 8.2 Deutéronome 8.16 Deutéronome 13.3 Job 23.10 Malachie 3.2-3.3
23 Basi Bwana akawaacha mataifa yale, wala hakuwafukuza kwa upesi, wala hakuwatia katika mikono ya Yoshua.

Cette Bible est dans le domaine public.