Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Apocalypse 21.17
Bible en Swahili de l’est


Un nouveau ciel et une nouvelle terre

1 Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya; kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza zimekwisha kupita, wala hapana bahari tena.
2 Pierre 3.13 Esaïe 66.22 Esaïe 65.17-65.19 2 Pierre 3.10 Apocalypse 20.11
2 Nami nikauona mji ule mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, umewekwa tayari, kama bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa mumewe.
Hébreux 11.10 Apocalypse 3.12 Apocalypse 21.10 Esaïe 61.10 Apocalypse 19.7-19.8
3 Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao.
2 Corinthiens 6.16 Lévitique 26.11-26.12 Zacharie 8.8 Apocalypse 7.15 Ezéchiel 37.27
4 Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita.
Esaïe 25.8 Apocalypse 7.17 1 Corinthiens 15.26 Esaïe 35.10 Apocalypse 20.14
5 Na yeye aketiye juu ya kile kiti cha enzi akasema, Tazama, nayafanya yote kuwa mapya. Akaniambia, Andika ya kwamba maneno hayo ni amini na kweli.
2 Corinthiens 5.17 Esaïe 42.9 Esaïe 43.19 Apocalypse 19.9 Apocalypse 20.11
6 Akaniambia, Imekwisha kuwa. Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Mimi nitampa yeye mwenye kiu, ya chemchemi ya maji ya uzima, bure.
Apocalypse 22.13 Apocalypse 1.8 Jean 4.10 Esaïe 55.1-55.3 Apocalypse 22.17
7 Yeye ashindaye atayarithi haya, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu.
Apocalypse 21.3 Matthieu 25.34 1 Jean 3.1-3.3 Hébreux 8.10 Apocalypse 2.17
8 Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.
1 Corinthiens 6.9-6.10 Apocalypse 20.14-20.15 Apocalypse 2.11 Apocalypse 22.15 Ephésiens 5.5-5.6

La nouvelle Jérusalem

9 Akaja mmoja wa wale malaika saba waliokuwa na vile vitasa saba vilivyojaa yale mapigo saba ya mwisho, naye akanena nami, akisema, Njoo huku, nami nitakuonyesha yule Bibi-arusi, mke wa Mwana-Kondoo.
Apocalypse 19.7 Apocalypse 21.2 Apocalypse 17.1 Apocalypse 16.1-16.17 Apocalypse 15.1-15.7
10 Akanichukua katika Roho mpaka mlima mkubwa, mrefu, akanionyesha ule mji mtakatifu, Yerusalemu, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mwenyezi Mungu;
Apocalypse 17.3 Apocalypse 1.10 Apocalypse 4.2 Ezéchiel 11.24 Actes 8.39
11 wenye utukufu wa Mungu, na mwangaza wake ulikuwa mfano wa kito chenye thamani nyingi kama kito cha yaspi, safi kama bilauri;
Apocalypse 4.6 Apocalypse 22.5 Ezéchiel 1.22 Apocalypse 21.18-21.19 Ezéchiel 1.26
12 ulikuwa na ukuta mkubwa, mrefu, wenye milango kumi na miwili, na katika ile milango malaika kumi na wawili; na majina yameandikwa ambayo ni majina ya kabila kumi na mbili za Waisraeli.
Ezéchiel 48.31-48.34 Apocalypse 7.4-7.8 Apocalypse 21.25 Nombres 2.2-2.32 Esaïe 60.18
13 Upande wa mashariki milango mitatu; na upande wa kaskazini milango mitatu; na upande wa kusini milango mitatu; na upande wa magharibi milango mitatu.
Ezéchiel 48.31-48.34
14 Na ukuta wa mji ulikuwa na misingi kumi na miwili, na katika ile misingi majina kumi na mawili ya wale mitume kumi na wawili wa Mwana-Kondoo.
Hébreux 11.10 Ephésiens 2.20 Apocalypse 18.20 Apocalypse 21.19-21.21 Jude 1.17
15 Na yeye aliyesema nami alikuwa na mwanzi wa dhahabu, apate kuupima huo mji, na milango yake, na ukuta wake.
Zacharie 2.1 Ezéchiel 41.1-41.5 Apocalypse 11.1-11.2 Exode 40.3-40.5
16 Na ule mji ni wa mraba, na marefu yake sawasawa na mapana yake. Akaupima mji kwa ule mwanzi; ulikuwa kama maili elfu na mia tano; marefu yake na mapana yake na kwenda juu kwake ni sawasawa.
Ezéchiel 48.8-48.20 Ezéchiel 48.35
17 Akaupima ukuta wake, ukapata dhiraa mia na arobaini na nne, kwa kipimo cha kibinadamu, maana yake, cha malaika.
Deutéronome 3.11 Apocalypse 7.4 Apocalypse 13.18 Apocalypse 14.3 Apocalypse 21.9
18 Na majenzi ya ule ukuta wake yalikuwa ya yaspi, na mji ule ulikuwa wa dhahabu safi, mfano wa kioo safi.
Apocalypse 21.11 Apocalypse 21.21 Apocalypse 21.19
19 Na misingi ya ukuta wa mji ilikuwa imepambwa kwa vito vya thamani vya kila namna. Msingi wa kwanza ulikuwa yaspi; wa pili yakuti samawi; wa tatu kalkedoni; wa nne zumaridi;
Esaïe 54.11-54.12 Exode 28.17-28.21 Exode 29.10-29.14 Proverbes 3.15 Job 28.16-28.19
20 wa tano sardoniki; wa sita akiki; wa saba krisolitho; wa nane zabarajadi; wa kenda yakuti ya manjano; wa kumi krisopraso; wa kumi na moja hiakintho; wa kumi na mbili amethisto.
Apocalypse 4.3
21 Na ile milango kumi na miwili ni lulu kumi na mbili; kila mlango ni lulu moja. Na njia ya mji ni dhahabu safi kama kioo kiangavu.
Apocalypse 21.18 Apocalypse 17.4 Apocalypse 22.2 Apocalypse 21.11-21.12 Apocalypse 18.16
22 Nami sikuona hekalu ndani yake; kwa maana Bwana Mungu Mwenyezi na Mwana-Kondoo, ndio hekalu lake.
Apocalypse 1.8 Jean 4.23 Colossiens 2.9 2 Chroniques 6.18 Jean 10.30
23 Na mji ule hauhitaji jua wala mwezi kuuangaza, kwa maana utukufu wa Mungu huutia nuru, na taa yake ni Mwana-Kondoo.
Esaïe 60.19-60.20 Apocalypse 21.11 Apocalypse 22.5 Esaïe 24.23 Habakuk 3.3
24 Na mataifa watatembea katika nuru yake. Na wafalme wa nchi huleta utukufu wao ndani yake.
Romains 15.10-15.12 Esaïe 60.16 Zacharie 2.11 Apocalypse 22.2 Esaïe 66.18
25 Na milango yake haitafungwa kamwe mchana; kwa maana humo hamna usiku.
Esaïe 60.11 Zacharie 14.7 Apocalypse 22.5 Esaïe 60.20 Apocalypse 21.23
26 Nao wataleta utukufu na heshima ya mataifa ndani yake.
Apocalypse 21.24
27 Na ndani yake hakitaingia kamwe cho chote kilicho kinyonge, wala yeye afanyaye machukizo na uongo, bali wale walioandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo.
Esaïe 52.1 Apocalypse 22.14-22.15 Esaïe 35.8 Apocalypse 3.5 Joël 3.17

Cette Bible est dans le domaine public.