Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

3 Jean 1.15
Bible en Swahili de l’est


Salutation et louange

1 Mzee, kwa Gayo mpenzi, nimpendaye katika kweli.
Romains 16.23 1 Jean 3.18 1 Corinthiens 1.14 Actes 19.29 Actes 20.4
2 Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo.
2 Pierre 1.3-1.9 2 Pierre 3.18 Jacques 5.12 3 Jean 1.3-1.6 Psaumes 20.1-20.5
3 Maana nalifurahi mno walipokuja ndugu na kuishuhudia kweli yako, kama uendavyo katika kweli.
2 Jean 1.4 Ephésiens 1.15-1.16 2 Jean 1.2 Psaumes 119.11 Philippiens 1.4
4 Sina furaha iliyo kuu kuliko hii, kusikia ya kwamba watoto wangu wanakwenda katika kweli.
Philémon 1.10 Galates 4.19 Galates 2.14 2 Rois 20.3 1 Rois 3.6
5 Mpenzi, kazi ile ni ya uaminifu uwatendeayo hao ndugu na hao wageni nao,
Galates 6.10 Colossiens 3.17 Matthieu 24.45 2 Corinthiens 4.1-4.3 Luc 12.42
6 waliokushuhudia upendo wako mbele ya kanisa; utafanya vizuri ukiwasafirisha kama ipasavyo kwa Mungu.
1 Thessaloniciens 2.12 Tite 3.13 Actes 15.3 3 Jean 1.12 Philippiens 4.14
7 Kwa maana, kwa ajili ya Jina hilo, walitoka, wasipokee kitu kwa Mataifa.
1 Corinthiens 9.12-9.15 Colossiens 1.24 Actes 5.41 2 Corinthiens 11.7-11.9 2 Rois 5.15-5.16
8 Basi imetupasa sisi kuwakaribisha watu kama hao, ili tuwe watenda kazi pamoja na kweli.
Matthieu 10.40 2 Corinthiens 7.2-7.3 1 Corinthiens 16.10-16.11 2 Corinthiens 8.23 Philippiens 4.3

Diotrèphe et Démétrius

9 Naliliandikia kanisa neno, lakini Diotrefe, apendaye kuwa wa kwanza kati yao, hatukubali.
Marc 9.34 Marc 10.35-10.45 Matthieu 10.40-10.42 Romains 12.10 Luc 9.48
10 Kwa hiyo, nikija, nitayakumbuka matendo yake atendayo, atoavyo upuzi juu yetu kwa maneno maovu; wala hatoshwi na hayo, ila yeye mwenyewe hawakaribishi hao ndugu, na wale watakao kuwakaribisha, huwazuia, na kuwatoa katika kanisa.
Jean 9.34-9.35 Jean 9.22 Proverbes 10.8 2 Corinthiens 10.1-10.11 1 Corinthiens 5.1-5.5
11 Mpenzi, usiuige ubaya, bali uige wema. Yeye atendaye mema ni wa Mungu, bali yeye atendaye mabaya hakumwona Mungu.
Esaïe 1.16-1.17 Psaumes 37.27 1 Jean 2.29 Jean 3.20 Ephésiens 5.1
12 Demetrio ameshuhudiwa na watu wote, tena na ile kweli yenyewe. Nasi pia twashuhudia, nawe wajua ya kwamba ushuhuda wetu ni kweli.
1 Timothée 3.7 Jean 21.24 Jean 19.35 Actes 10.22 1 Thessaloniciens 4.12
13 Nalikuwa na mambo mengi ya kukuandikia, lakini sipendi kukuandikia kwa wino na kalamu.
2 Jean 1.12
14 Lakini nataraji kukuona karibu, nasi tutasema uso kwa uso. [15] Amani kwako. Rafiki zetu wakusalimu. Wasalimu hao rafiki zetu, kila mtu kwa jina lake.
Ephésiens 6.23 Daniel 4.1 Romains 16.1-16.16 Genèse 43.23 1 Pierre 5.14

Cette Bible est dans le domaine public.