Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Hébreux 2.3
Bible en Swahili de l’est


1 Kwa hiyo imetupasa kuyaangalia zaidi hayo yaliyosikiwa tusije tukayakosa.
Hébreux 1.1-1.2 Luc 8.15 2 Pierre 3.1 2 Pierre 1.12-1.13 2 Pierre 1.15
2 Kwa maana, ikiwa lile neno lililonenwa na malaika lilikuwa imara, na kila kosa na uasi ulipata ujira wa haki,
Actes 7.53 Galates 3.19 Hébreux 10.35 Hébreux 10.28 Deutéronome 27.26
3 sisi je! Tutapataje kupona, tusipojali wokovu mkuu namna hii? Ambao kwanza ulinenwa na Bwana, kisha ukathibitika kwetu na wale waliosikia;
Luc 1.2 Hébreux 12.25 Hébreux 1.2 Hébreux 5.9 Ezéchiel 17.15
4 Mungu naye akishuhudu pamoja nao kwa ishara na ajabu na nguvu za namna nyingi, na kwa magawanyo ya Roho Mtakatifu, kama alivyopenda mwenyewe.
1 Corinthiens 12.4-12.11 Ephésiens 4.8-4.11 Ephésiens 1.5 Ephésiens 1.9 Marc 16.20
5 Maana hakuuweka chini ya malaika ulimwengu ule ujao tunaounena, ila mtu mmoja ameshuhudia hivi mahali fulani, akisema,
Hébreux 6.5 Apocalypse 11.15 2 Pierre 3.13
6 Mwanadamu ni nini hata umkumbuke, Ama mwana wa binadamu, hata umwangalie?
Psaumes 144.3 Psaumes 8.4-8.8 Job 7.17-7.18 Job 25.6 Esaïe 51.12
7 Umemfanya mdogo punde kuliko malaika, Umemvika taji ya utukufu na heshima, Umemtawaza juu ya kazi za mikono yako;
Psaumes 8.5
8 Umeweka vitu vyote chini ya nyayo zake. Kwa maana katika kuweka vitu vyote chini yake hakusaza kitu kisichowekwa chini yake. Lakini sasa bado hatujaona vitu vyote kutiwa chini yake.
Psaumes 8.6 1 Corinthiens 15.27 Jean 13.3 Ephésiens 1.21-1.22 Jean 3.35
9 ila twamwona yeye aliyefanywa mdogo punde kuliko malaika, yaani, Yesu, kwa sababu ya maumivu ya mauti, amevikwa taji ya utukufu na heshima, ili kwa neema ya Mungu aionje mauti kwa ajili ya kila mtu.
Philippiens 2.7-2.9 Actes 2.33 Jean 3.16 Jean 8.52 Jean 12.32
10 Kwa kuwa ilimpasa yeye, ambaye kwa ajili yake na kwa njia yake vitu vyote vimekuwapo, akileta wana wengi waufikilie utukufu, kumkamilisha kiongozi mkuu wa wokovu wao kwa njia ya mateso.
Luc 24.26 Romains 11.36 Luc 24.46 Actes 5.31 Hébreux 6.20
11 Maana yeye atakasaye na hao wanaotakaswa wote pia watoka kwa mmoja. Kwa ajili hii haoni haya kuwaita ndugu zake;
Hébreux 10.10 Hébreux 13.12 Matthieu 25.40 Jean 20.17 Hébreux 10.14
12 akisema, Nitalihubiri jina lako kwa ndugu zangu; Katikati ya kanisa nitakuimbia sifa.
Psaumes 22.22 Psaumes 111.1 Psaumes 40.10 Jean 18.20 Psaumes 22.25
13 Na tena, Nitakuwa nimemtumaini yeye. Na tena, Tazama,mimi nipo hapa na watoto niliopewa na Mungu.
Esaïe 8.17-8.18 Esaïe 12.2 Jean 10.29 Psaumes 18.2 Esaïe 50.7-50.9
14 Basi, kwa kuwa watoto wameshiriki damu na mwili, yeye naye vivyo hivyo alishiriki yayo hayo, ili kwa njia ya mauti amharibu yeye aliyekuwa na nguvu za mauti, yaani, Ibilisi,
2 Timothée 1.10 Jean 1.14 Romains 8.3 Osée 13.14 Colossiens 2.15
15 awaache huru wale ambao kwamba maisha yao yote kwa hofu ya mauti walikuwa katika hali ya utumwa.
Romains 8.15 2 Timothée 1.7 1 Corinthiens 15.50-15.57 Psaumes 55.4 2 Corinthiens 1.10
16 Maana ni hakika, hatwai asili ya malaika, ila atwaa asili ya mzao wa Ibrahimu.
Romains 4.16-4.25 Romains 2.25 Galates 3.16 Hébreux 12.10 Galates 3.29
17 Hivyo ilimpasa kufananishwa na ndugu zake katika mambo yote, apate kuwa kuhani mkuu mwenye rehema, mwaminifu katika mambo ya Mungu, ili afanye suluhu kwa dhambi za watu wake.
Hébreux 4.14-5.2 Philippiens 2.7-2.8 Daniel 9.24 Hébreux 2.14 Hébreux 7.26
18 Na kwa kuwa mwenyewe aliteswa alipojaribiwa, aweza kuwasaidia wao wanaojaribiwa.
Hébreux 5.2 Jean 10.29 Hébreux 4.15-4.16 Apocalypse 3.10 Hébreux 7.25-7.26

Cette Bible est dans le domaine public.