Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Timothée 4.15
Bible en Swahili de l’est


Conseils à propos des fausses doctrines

1 Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani;
2 Timothée 3.1-3.9 2 Pierre 3.3 Jude 1.18 2 Thessaloniciens 2.3-2.12 Ezéchiel 38.16
2 kwa unafiki wa watu wasemao uongo, wakichomwa moto dhamiri zao wenyewe;
Ephésiens 4.19 Romains 16.18 1 Rois 13.18 Jérémie 5.21 Ephésiens 4.14
3 wakiwazuia watu wasioe, na kuwaamuru wajiepushe na vyakula, ambavyo Mungu aliviumba vipokewe kwa shukrani na walio na imani wenye kuijua hiyo kweli.
Romains 14.6 Hébreux 13.4 Genèse 9.3 1 Corinthiens 7.28 Colossiens 2.16
4 Kwa maana kila kiumbe cha Mungu ni kizuri, wala hakuna cha kukataliwa, kama kikipokewa kwa shukrani;
1 Timothée 4.3 Romains 14.20 Actes 21.25 Romains 14.14 Deutéronome 32.4
5 kwa kuwa kimetakaswa kwa neno la Mungu na kwa kuomba.
1 Corinthiens 7.14 Luc 11.41 Genèse 1.25 Luc 4.4 Genèse 1.31
6 Uwakumbushe ndugu mambo hayo, nawe utakuwa mtumishi mwema wa Kristo Yesu, na mzoevu wa maneno ya imani, na mafundisho mazuri yale uliyoyafuata.
Colossiens 3.16 1 Timothée 1.10 Colossiens 4.7 2 Timothée 3.14-3.17 2 Timothée 3.10
7 Bali hadithi za kizee, zisizokuwa za dini, uzikatae; nawe ujizoeze kupata utauwa.
1 Timothée 1.4 2 Timothée 2.16 Tite 2.12 Hébreux 5.14 Tite 3.9
8 Kwa maana kujizoeza kupata nguvu za mwili kwafaa kidogo, lakini utauwa hufaa kwa mambo yote; yaani, unayo ahadi ya uzima wa sasa, na ya ule utakaokuwapo baadaye.
Matthieu 6.33 1 Timothée 6.6 Job 5.19-5.26 Psaumes 84.11 Psaumes 145.19
9 Ni neno la kuaminiwa, tena lastahili kukubalika kabisa;
1 Timothée 1.15
10 kwa maana twajitaabisha na kujitahidi kwa kusudi hili, kwa sababu tunamtumaini Mungu aliye hai, aliye Mwokozi wa watu wote, hasa wa waaminio.
1 Timothée 2.4 1 Jean 4.14 1 Jean 2.2 1 Timothée 2.6 2 Corinthiens 11.23-11.27
11 Mambo hayo uyaagize na kuyafundisha.
1 Timothée 6.2 1 Timothée 5.7 Tite 2.15 Tite 3.8 2 Timothée 4.2
12 Mtu awaye yote asiudharau ujana wako, bali uwe kielelezo kwao waaminio, katika usemi na mwenendo, na katika upendo na imani na usafi.
Tite 2.7 2 Timothée 2.22 1 Pierre 5.3 2 Timothée 2.15 1 Corinthiens 11.1
13 Hata nitakapokuja, ufanye bidii katika kusoma na kuonya na kufundisha.
1 Timothée 4.6 1 Timothée 4.16 1 Timothée 3.14-3.15 Josué 1.8 1 Corinthiens 14.6
14 Usiache kuitumia karama ile iliyomo ndani yako, uliyopewa kwa unabii na kwa kuwekewa mikono ya wazee.
2 Timothée 1.6 1 Timothée 1.18 Actes 6.6 1 Thessaloniciens 5.19 1 Timothée 5.22
15 Uyatafakari hayo; ukae katika hayo; ili kuendelea kwako kuwe dhahiri kwa watu wote.
Matthieu 5.16 Psaumes 119.23 Psaumes 119.48 Psaumes 63.6 Psaumes 143.5
16 Jitunze nafsi yako, na mafundisho yako. Dumu katika mambo hayo; maana kwa kufanya hivyo utajiokoa nafsi yako na wale wakusikiao pia.
Ezéchiel 33.7-33.9 Actes 20.26-20.28 Tite 2.7 Tite 1.9 Hébreux 12.15

Cette Bible est dans le domaine public.