Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Thessaloniciens 2.17
Bible en Swahili de l’est


Retour du Seigneur

1 Basi, ndugu, tunakusihini, kwa habari ya kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo, na kukusanyika kwetu mbele zake,
Marc 13.27 Matthieu 24.31 1 Thessaloniciens 4.14-4.17 1 Thessaloniciens 2.19 Romains 12.1
2 kwamba msifadhaishwe upesi hata kuiacha nia yenu, wala msisitushwe, kwa roho, wala kwa neno, wala kwa waraka unaodhaniwa kuwa ni wetu, kana kwamba siku ya Bwana imekwisha kuwapo.
1 Jean 4.1-4.2 1 Corinthiens 1.8 Marc 13.7 Jérémie 23.25-23.27 1 Thessaloniciens 3.3
3 Mtu awaye yote asiwadanganye kwa njia yo yote; maana haiji, usipokuja kwanza ule ukengeufu; akafunuliwa yule mtu wa kuasi, mwana wa uharibifu;
Ephésiens 5.6 Daniel 7.25 Matthieu 24.4-24.6 Jean 17.12 1 Timothée 4.1-4.3
4 yule mpingamizi, ajiinuaye nafsi yake juu ya kila kiitwacho Mungu ama kuabudiwa; hata yeye mwenyewe kuketi katika hekalu la Mungu, akijionyesha nafsi yake kana kwamba yeye ndiye Mungu.
Ezéchiel 28.2 1 Corinthiens 8.5 Apocalypse 13.6-13.7 Esaïe 14.13-14.14 Daniel 8.9-8.14
5 Je! Hamkumbuki ya kuwa wakati nilipokuwapo pamoja nanyi naliwaambieni hayo?
2 Thessaloniciens 3.10 Actes 20.31 Luc 24.6-24.7 2 Pierre 1.15 Matthieu 16.9
6 Na sasa lizuialo mwalijua, yule apate kufunuliwa wakati wake.
2 Thessaloniciens 2.3 2 Thessaloniciens 2.8
7 Maana ile siri ya kuasi hivi sasa inatenda kazi; lakini yuko azuiaye sasa, hata atakapoondolewa.
1 Jean 2.18 Apocalypse 17.7 Apocalypse 17.5 1 Jean 4.3 Colossiens 2.18-2.23
8 Hapo ndipo atakapofunuliwa yule asi, ambaye Bwana Yesu atamwua kwa pumzi ya kinywa chake, na kumwangamiza kwa ufunuo wa kuwapo kwake;
Esaïe 11.4 Apocalypse 19.15 2 Thessaloniciens 2.3 Daniel 7.10-7.11 Apocalypse 2.16
9 yule ambaye kuja kwake ni kwa mfano wa kutenda kwake Shetani, kwa uwezo wote, na ishara na ajabu za uongo;
Matthieu 24.24 Apocalypse 18.23 Apocalypse 19.20 Deutéronome 13.1-13.2 2 Timothée 3.8
10 na katika madanganyo yote ya udhalimu kwa hao wanaopotea; kwa sababu hawakukubali kuipenda ile kweli, wapate kuokolewa.
Proverbes 1.7 1 Corinthiens 1.18 2 Corinthiens 4.2-4.3 1 Corinthiens 16.22 2 Pierre 2.12
11 Kwa hiyo Mungu awaletea nguvu ya upotevu, wauamini uongo;
Romains 1.28 Ezéchiel 14.9 Jérémie 27.10 Ezéchiel 21.29 Esaïe 6.9-6.10
12 ili wahukumiwe wote ambao hawakuiamini kweli, bali walikuwa wakijifurahisha katika udhalimu.
Romains 1.32 Romains 2.8 Romains 8.7-8.8 Marc 16.16 Psaumes 50.16-50.21

Appel à la fermeté, à la prière et au travail

13 Lakini imetupasa sisi kumshukuru Mungu sikuzote kwa ajili yenu, ndugu mliopendwa na Bwana, kwa kuwa Mungu amewachagua tangu mwanzo mpate wokovu, katika kutakaswa na Roho, na kuiamini kweli;
2 Timothée 1.9 1 Thessaloniciens 1.4 Actes 13.48 2 Thessaloniciens 1.3 1 Thessaloniciens 5.9
14 aliyowaitia ninyi kwa injili yetu, ili kuupata utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristo.
1 Thessaloniciens 2.12 1 Pierre 5.10 1 Thessaloniciens 1.5 Romains 8.28-8.30 Matthieu 25.21
15 Basi, ndugu, simameni imara, mkayashike mapokeo mliyofundishwa, ama kwa maneno, ama kwa waraka wetu.
1 Corinthiens 11.2 2 Thessaloniciens 2.2 2 Thessaloniciens 3.6 1 Corinthiens 16.13 Jude 1.3
16 Na Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe, na Mungu Baba yetu, aliyetupenda akatupa faraja ya milele na tumaini jema, katika neema,
Jean 3.16 1 Pierre 1.3-1.8 Ephésiens 5.25 1 Thessaloniciens 3.11 Jean 14.16-14.18
17 awafariji mioyo yenu, na kuwafanya imara katika kila neno na tendo jema.
2 Thessaloniciens 3.3 1 Thessaloniciens 3.2 1 Thessaloniciens 3.13 2 Corinthiens 1.3-1.6 2 Thessaloniciens 2.16

Cette Bible est dans le domaine public.