Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Deutéronome 23.22
Bible en Swahili de l’est


1 Aliyejeruhika konde, au aliyekatika tupu yake, asiingie mtu huyo katika mkutano wa Bwana.
Lévitique 22.22-22.24 Lévitique 21.17-21.21 Lamentations 1.10 Galates 3.28 Néhémie 13.1-13.3

Cas d’exclusion de l’assemblée

2 Mwana wa haramu asiingie katika mkutano wa Bwana; hata kizazi cha kumi asiingie aliye wake katika mkutano wa Bwana.
Zacharie 9.6 Esaïe 57.3 Hébreux 12.8 Jean 8.41
3 Mwamoni wala Mmoabi wasiingie katika mkutano wa Bwana; wala hata kizazi cha kumi mtu wao asiingie katika mkutano wa Bwana milele;
Néhémie 13.1-13.2 Ruth 4.10-4.22 Néhémie 13.23 Néhémie 4.7 Esaïe 56.3
4 kwa sababu hapo mlipotoka Misri hawakuwalaki na chakula wala maji njiani; na kwa kuwa walimwajiri juu yako Balaamu mwana wa Beori kutoka Pethori iliyo Mesopotamia, aje akuapize.
2 Pierre 2.15 Néhémie 13.2 Zacharie 2.8 Nombres 23.7 1 Rois 18.4
5 Lakini Bwana, Mungu wako, hakukubali kumsikiza huyo Balaamu; Bwana, Mungu wako, aliyageuza yale maapizo kuwa ni baraka, kwa vile alivyokupenda Bwana, Mungu wako.
Deutéronome 7.7-7.8 Romains 8.31 Ephésiens 2.4-2.5 2 Corinthiens 4.17 Nombres 23.5-23.12
6 Usitafute amani yao wala heri yao siku zako zote, milele.
Esdras 9.12 2 Samuel 8.2 2 Samuel 12.31 Néhémie 13.23-13.25
7 Usimchukie Mwedomi; kwa kuwa ni ndugu yako; usimchukie Mmisri, kwa kuwa ulikuwa mgeni katika nchi yake.
Exode 22.21 Deutéronome 10.19 Lévitique 19.34 Exode 23.9 Genèse 25.24-25.26
8 Wana wao watakaozaliwa kizazi cha tatu na waingie katika mkutano wa Bwana.
Deutéronome 23.1-23.3 Exode 20.5-20.6 Romains 3.29-3.30 Ephésiens 2.12-2.13
9 Utakapotoka kwenda juu ya adui zako nawe u katika marago, jilinde na kila neno baya.
Josué 6.18 2 Chroniques 19.4 Juges 20.26 2 Chroniques 31.20-32.22 Josué 7.11-7.13

Règles liées à la pureté

10 Akiwa kwenu mtu awaye yote asiyekuwa ni tohara kwa ajili ya yaliyomtukia usiku, na atoke nje ya kituo, wala asiingie ndani ya kituo;
Lévitique 15.16 Nombres 5.2-5.3 1 Corinthiens 5.11-5.13
11 lakini na iwe ikaribiapo jioni, yeye ataoga maji; na jua likiisha kuchwa ataingia ndani ya kituo.
Ephésiens 5.26-5.27 Lévitique 14.9 Lévitique 15.5 Hébreux 10.22 Luc 11.38-11.39
12 Tena uwe na mahali nje ya kituo, kwa kutokea nje;
13 nawe uwe na jembe dogo katika silaha zako; napo uotamapo nje uchimbe kwa lile jembe, na kugeuka na kukifunika kikutokacho;
Ezéchiel 24.6-24.8
14 kwa kuwa Bwana. Mungu wako, yuatembea katika kituo akuokoe, na kukutolea adui zako mbele yako; kwa hiyo na kiwe kitakatifu kituo chako; asije akaona kitu kwako kisichokuwa safi, akageuka na kukuacha.
Lévitique 26.12 Genèse 17.1 2 Corinthiens 6.16 Exode 3.5
15 Usimrudishe kwa bwana wake mtumwa aliyejiponya kutoka kwa bwana wake kuja kwako;
1 Samuel 30.15 Abdias 1.14
16 na akae nawe, katikati yako, ndani ya malango yako mojawapo, mahali atakapochagua palipo pema machoni pake; usimwonee.
Exode 22.21 Exode 23.9 Esaïe 16.3-16.4 Jacques 2.6 Tite 3.2-3.3
17 Pasiwe na kahaba katika binti za Israeli, wala pasiwe na hanithi katika wana wa Israeli wanaume.
Lévitique 19.29 2 Rois 23.7 1 Rois 14.24 1 Rois 15.12 1 Rois 22.46
18 Usilete ujira wa kahaba, wala mshahara wa mbwa, katika nyumba ya Bwana, Mungu wako, kwa ajili ya nadhiri yo yote; kwani haya ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako, yote mawili.
Matthieu 7.6 Philippiens 3.2 Deutéronome 23.21 Apocalypse 22.15 Lévitique 18.22
19 Usimkopeshe ndugu yako kwa riba; riba ya fedha, riba ya vyakula, riba ya kitu cho chote kikopeshwacho kwa riba;
Exode 22.25 Lévitique 25.35-25.37 Psaumes 15.5 Ezéchiel 18.16-18.18 Ezéchiel 18.13
20 mgeni waweza kumkopesha kwa riba, ila usimkopeshe ndugu yako kwa riba; ili Bwana, Mungu wako, apate kukubarikia katika yote utiayo mkono wako, katika nchi uingiayo kuimiliki.
Deutéronome 15.10 Deutéronome 15.3 Deutéronome 14.21 Luc 14.14 Esaïe 1.19
21 Utakapoweka nadhiri kwa Bwana, Mungu wako, usiwe mlegevu katika kuiondoa; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, hataacha kuitaka kwako; nayo hivi itakuwa dhambi kwako.
Ecclésiaste 5.4-5.5 Deutéronome 23.18 Psaumes 76.11 Psaumes 66.13-66.14 Genèse 28.20

Les vœux

22 Lakini ukijizuia usiweke nadhiri, haitakuwa dhambi kwako.
23 Yaliyotoka midomoni mwako yashike kuyafanya; kwa mfano wa ulivyomwekea nadhiri Bwana, Mungu wako, ni sadaka ya hiari uliyoahidi kwa kinywa chako.
Proverbes 20.25 Actes 23.12 Nombres 30.2 Marc 6.22-6.23 Psaumes 66.13-66.14
24 Uingiapo katika shamba la mizabibu la jirani yako, utaweza kula zabibu za kukushibisha, kama upendavyo; ila usitie katika chombo chako.
1 Corinthiens 10.26 Hébreux 13.5 Romains 12.13
25 Uingiapo katika mmea wa jirani yako waweza kuyapurura masuke kwa mkono wako; ila usisongeze mundu katika mmea wa jirani yako.
Marc 2.23 Luc 6.1-6.2 Matthieu 12.1-12.2

Cette Bible est dans le domaine public.