1 Aliyejeruhika konde, au aliyekatika tupu yake, asiingie mtu huyo katika mkutano wa Bwana.
Galates 3.28  Néhémie 13.1-13.3  Esaïe 56.3-56.4  Deutéronome 23.2-23.3  Deutéronome 23.8  
Cas d’exclusion de l’assemblée
 2  Mwana wa haramu asiingie katika mkutano wa Bwana; hata kizazi cha kumi asiingie aliye wake katika mkutano wa Bwana.Zacharie 9.6  Esaïe 57.3  Hébreux 12.8  Jean 8.41  
 3 Mwamoni wala Mmoabi wasiingie katika mkutano wa Bwana; wala hata kizazi cha kumi mtu wao asiingie katika mkutano wa Bwana milele;
Néhémie 13.1-13.2  Esaïe 56.3  Ruth 4.6  Néhémie 4.3  Ruth 4.10-4.22  
 4 kwa sababu hapo mlipotoka Misri hawakuwalaki na chakula wala maji njiani; na kwa kuwa walimwajiri juu yako Balaamu mwana wa Beori kutoka Pethori iliyo Mesopotamia, aje akuapize.
2 Pierre 2.15  Néhémie 13.2  Nombres 22.17  Genèse 14.17-14.18  Actes 9.4  
 5 Lakini Bwana, Mungu wako, hakukubali kumsikiza huyo Balaamu; Bwana, Mungu wako, aliyageuza yale maapizo kuwa ni baraka, kwa vile alivyokupenda Bwana, Mungu wako.
Deutéronome 7.7-7.8  Romains 8.31  Ephésiens 2.4-2.5  2 Corinthiens 4.17  Nombres 23.5-23.12  
 6 Usitafute amani yao wala heri yao siku zako zote, milele.
Esdras 9.12  Néhémie 13.23-13.25  2 Samuel 8.2  2 Samuel 12.31  
 7 Usimchukie Mwedomi; kwa kuwa ni ndugu yako; usimchukie Mmisri, kwa kuwa ulikuwa mgeni katika nchi yake.
Deutéronome 10.19  Exode 22.21  Lévitique 19.34  Exode 23.9  Genèse 25.24-25.26  
 8 Wana wao watakaozaliwa kizazi cha tatu na waingie katika mkutano wa Bwana.
Deutéronome 23.1-23.3  Exode 20.5-20.6  Romains 3.29-3.30  Ephésiens 2.12-2.13  
 9 Utakapotoka kwenda juu ya adui zako nawe u katika marago, jilinde na kila neno baya.
Josué 6.18  Juges 20.26  2 Chroniques 31.20-32.22  Josué 7.11-7.13  2 Chroniques 19.4  
Règles liées à la pureté
 10 Akiwa kwenu mtu awaye yote asiyekuwa ni tohara kwa ajili ya yaliyomtukia usiku, na atoke nje ya kituo, wala asiingie ndani ya kituo;
Lévitique 15.16  Nombres 5.2-5.3  1 Corinthiens 5.11-5.13  
 11 lakini na iwe ikaribiapo jioni, yeye ataoga maji; na jua likiisha kuchwa ataingia ndani ya kituo.
Ephésiens 5.26-5.27  Lévitique 14.9  Lévitique 15.5  Hébreux 10.22  Luc 11.38-11.39  
 12 Tena uwe na mahali nje ya kituo, kwa kutokea nje; 
13 nawe uwe na jembe dogo katika silaha zako; napo uotamapo nje uchimbe kwa lile jembe, na kugeuka na kukifunika kikutokacho;
Ezéchiel 24.6-24.8  
 14 kwa kuwa Bwana. Mungu wako, yuatembea katika kituo akuokoe, na kukutolea adui zako mbele yako; kwa hiyo na kiwe kitakatifu kituo chako; asije akaona kitu kwako kisichokuwa safi, akageuka na kukuacha.
Lévitique 26.12  Genèse 17.1  2 Corinthiens 6.16  Exode 3.5  
 15 Usimrudishe kwa bwana wake mtumwa aliyejiponya kutoka kwa bwana wake kuja kwako;
1 Samuel 30.15  Abdias 1.14  
 16 na akae nawe, katikati yako, ndani ya malango yako mojawapo, mahali atakapochagua palipo pema machoni pake; usimwonee.
Exode 22.21  Exode 23.9  Luc 15.15-15.24  Malachie 3.5  Jérémie 7.6  
 17 Pasiwe na kahaba katika binti za Israeli, wala pasiwe na hanithi katika wana wa Israeli wanaume.
2 Rois 23.7  Lévitique 19.29  1 Rois 14.24  1 Timothée 1.10  Deutéronome 22.21  
 18 Usilete ujira wa kahaba, wala mshahara wa mbwa, katika nyumba ya Bwana, Mungu wako, kwa ajili ya nadhiri yo yote; kwani haya ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako, yote mawili.
Deutéronome 23.21  Apocalypse 22.15  Lévitique 18.22  Matthieu 7.6  Philippiens 3.2  
 19 Usimkopeshe ndugu yako kwa riba; riba ya fedha, riba ya vyakula, riba ya kitu cho chote kikopeshwacho kwa riba;
Exode 22.25  Psaumes 15.5  Lévitique 25.35-25.37  Luc 6.34-6.35  Néhémie 5.1-5.7  
 20 mgeni waweza kumkopesha kwa riba, ila usimkopeshe ndugu yako kwa riba; ili Bwana, Mungu wako, apate kukubarikia katika yote utiayo mkono wako, katika nchi uingiayo kuimiliki.
Deutéronome 15.10  Deutéronome 15.3  Deutéronome 14.21  1 Corinthiens 15.58  Deutéronome 28.12  
 21 Utakapoweka nadhiri kwa Bwana, Mungu wako, usiwe mlegevu katika kuiondoa; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, hataacha kuitaka kwako; nayo hivi itakuwa dhambi kwako.
Ecclésiaste 5.4-5.5  Deutéronome 23.18  Psaumes 76.11  Psaumes 66.13-66.14  Jonas 1.16  
Les vœux
 22 Lakini ukijizuia usiweke nadhiri, haitakuwa dhambi kwako. 
23 Yaliyotoka midomoni mwako yashike kuyafanya; kwa mfano wa ulivyomwekea nadhiri Bwana, Mungu wako, ni sadaka ya hiari uliyoahidi kwa kinywa chako.
Juges 11.35  Ecclésiaste 5.4-5.5  1 Samuel 14.24  Jérémie 44.25-44.27  Actes 23.21  
 24 Uingiapo katika shamba la mizabibu la jirani yako, utaweza kula zabibu za kukushibisha, kama upendavyo; ila usitie katika chombo chako.
1 Corinthiens 10.26  Hébreux 13.5  Romains 12.13  
 25 Uingiapo katika mmea wa jirani yako waweza kuyapurura masuke kwa mkono wako; ila usisongeze mundu katika mmea wa jirani yako.
Marc 2.23  Luc 6.1-6.2  Matthieu 12.1-12.2