Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Deutéronome 12.7
Bible en Swahili de l’est


Répétition des prescriptions et règles

Ordre de servir l’Éternel à l’endroit choisi par lui

1 Hizi ndizo amri na hukumu mtakazotunza kuzifanya katika nchi aliyokupa Bwana, Mungu wa baba zako, uimiliki, siku zote mtakazoishi juu ya nchi.
1 Rois 8.40 Job 7.1 Deutéronome 12.19 Deutéronome 4.19 Deutéronome 6.1-6.2
2 Vunjeni kabisa mahali pote walipokuwa wakiitumikia miungu yao mataifa mtakayoyamiliki, juu ya milima mirefu, na juu ya vilima, na chini ya kila mti wenye majani mabichi;
2 Rois 16.4 2 Rois 17.10-17.11 Jérémie 3.6 Deutéronome 7.25-7.26 Deutéronome 7.5
3 nanyi zivunjeni madhabahu zao, zibomoeni nguzo zao, na maashera yao yateketezeni kwa moto, na sanamu za kuchonga za miungu yao zikateni; na jina lao lifutilieni mbali na mahali hapo.
Zacharie 13.2 Juges 2.2 Nombres 33.52 Psaumes 16.4 Exode 23.13
4 Wala msimfanyie hivyo Bwana, Mungu wenu.
Deutéronome 16.21-16.22 Deutéronome 12.30-12.31 Lévitique 20.23 Deutéronome 20.18
5 Lakini mahali atakapochagua Bwana, Mungu wenu, katika kabila zenu zote, apaweke jina lake, maana, ni makao yake, elekezeni nyuso zenu hapo, nawe wende huko;
Deutéronome 12.11 2 Chroniques 7.12 Deutéronome 16.2 1 Rois 8.29 Deutéronome 26.2
6 pelekeni huko sadaka zenu za kuteketezwa, na dhabihu zenu, na zaka zenu, na sadaka ya kuinuliwa ya mikono yenu, na nadhiri zenu, na sadaka zenu za hiari, na wazaliwa wa kwanza wa makundi yenu ya ng’ombe na ya kondoo;
Deutéronome 15.19-15.20 Lévitique 17.3-17.9 Nombres 18.15-18.17 Ezéchiel 20.40 Deutéronome 14.22-14.26
7 na huko mtakula mbele za Bwana, Mungu wenu, nanyi furahini katika yote mtakayotia mikono yenu, ninyi na wa nyumbani mwenu, aliyokubarikia Bwana, Mungu wako.
Deutéronome 12.18 Deutéronome 14.26 Lévitique 23.40 Deutéronome 12.12 Philippiens 4.4
8 Msifanye kwa kufuata mambo yote tuyafanyayo hapa leo, kila mtu kama aonavyo vema machoni pake;
Juges 21.25 Juges 17.6 Proverbes 21.2 Amos 5.25 Nombres 15.39
9 kwani hamjafikilia bado katika raha na urithi akupao Bwana, Mungu wako.
1 Rois 8.56 Deutéronome 25.19 Michée 2.10 Psaumes 95.11 1 Pierre 1.3-1.4
10 Lakini mtakapovuka Yordani na kukaa katika nchi anayowarithisha Bwana, Mungu wenu, akawapeni raha, akiwaokoa na adui zenu pande zote, mkakaa salama;
Deutéronome 11.31 Josué 3.17-4.1 Jérémie 32.37 Jérémie 23.6 Ezéchiel 34.25
11 wakati huo itakuwa kwamba mahali pale atakapopachagua Bwana, Mungu wenu, alikalishe jina lake, hapo ndipo mtakapoleta kila kitu ninachowaamuru; sadaka zenu za kuteketezwa, na dhabihu zenu, na zaka zenu, na sadaka ya kuinuliwa ya mikono yenu, na nadhiri zenu zote teule mtakazoweka kwa Bwana.
Deutéronome 12.5 Deutéronome 15.20 Deutéronome 17.8 Deutéronome 18.6 Jean 4.20-4.23
12 Nanyi mtafurahi mbele za Bwana, Mungu wenu, ninyi, na wana wenu, na binti zenu, na watumishi wenu wanawaume na wanawake, na Mlawi aliyemo malangoni mwenu; kwa kuwa hana sehemu wala urithi kwenu.
Deutéronome 12.7 Deutéronome 26.12 Nombres 18.20 Deutéronome 10.9 Deutéronome 12.19
13 Ujihadhari usitoe sadaka zako za kuteketezwa katika kila mahali upaonapo;
Lévitique 17.2-17.5 1 Rois 15.34 1 Rois 12.28-12.32 2 Chroniques 15.17 Deutéronome 12.6
14 bali katika mahali atakapopachagua Bwana katika kabila zako mojawapo, ndipo utakapotoa sadaka zako za kuteketezwa, ndipo utakapotenda yote nikuamuruyo.
Deutéronome 12.11 Deutéronome 12.5 Psaumes 5.7 Hébreux 10.19-10.22 Hébreux 13.15
15 Pamoja na haya waweza kuchinja nyama na kula ndani ya malango yako yote, kwa kufuata yote yatamaniwayo na roho yako, kwa mfano wa baraka ya Bwana, Mungu wako, aliyokupa; aliye tohara na asiye tohara ana ruhusa kula katika nyama hiyo, kama ya paa na ya kulungu.
Deutéronome 14.5 Deutéronome 15.22-15.23 Deutéronome 14.26 Deutéronome 12.20-12.23 Lévitique 17.3-17.5
16 Lakini msiile damu; imwageni juu ya nchi kama maji.
Genèse 9.4 Deutéronome 15.23 Actes 15.29 Deutéronome 12.23-12.24 1 Timothée 4.4
17 Usile ndani ya malango yako zaka ya nafaka zako, wala ya divai yako, wala ya mafuta yako, wala wazaliwa wa kwanza wa makundi yako, ya ng’ombe wala ya kondoo, wala nadhiri zako uwekazo zo zote, wala sadaka zako za hiari, wala sadaka ya kuinuliwa ya mkono wako;
Deutéronome 26.14 Deutéronome 12.6 Deutéronome 26.12 Nombres 18.21-18.24 Lévitique 27.30-27.32
18 lakini hivyo mtakula mbele za Bwana, Mungu wako, mahali atakapochagua Bwana, Mungu wako, wewe, na mwanao mume na mke, na mtumwa wako mume na mke, na Mlawi aliye ndani ya malango yako; nawe furahi mbele za Bwana, Mungu wako, katika yote utakayotia mkono wako.
Deutéronome 12.7 Deutéronome 14.23 Deutéronome 12.5 Actes 2.46 Psaumes 68.3
19 Jilinde nafsi yako usimwache Mlawi siku zote uishizo katika nchi yako.
Néhémie 10.34-10.39 2 Chroniques 31.4-31.21 2 Chroniques 11.13-11.14 1 Corinthiens 9.10-9.14 Deutéronome 14.27-14.29
20 Bwana, Mungu wako, atakapoongeza mpaka wako, kama alivyokuahidi, nawe utakaposema, Nataka kula nyama, kwa kuwa roho yako yatamani kula nyama; waweza kula nyama, kwa kufuata yote inayotamani roho yako.
Deutéronome 19.8 Deutéronome 11.24 Exode 34.24 Genèse 28.14 Philippiens 1.8
21 Na mahali atakapochagua Bwana, Mungu wako, apaweke jina lake, pakiwa mbali nawe mno, ndipo utakapochinja katika kundi lako la ng’ombe na kondoo alilokupa Bwana kama nilivyokuagiza, nawe utakula ndani ya malango yako, kwa kufuata yote inayotamani roho yako.
Deutéronome 12.5 Deutéronome 16.11 Exode 20.24 1 Rois 14.21 Deutéronome 16.6
22 Kama vile aliwavyo paa na kulungu, ndivyo utakavyoila nyama hii; asiyekuwa tohara na aliye tohara wataila pia.
Deutéronome 12.15-12.16
23 Ila ujihadhari kwamba usile damu, kwani ile damu ndiyo uhai; na uhai usile pamoja na nyama.
Lévitique 17.11 Genèse 9.4 Lévitique 17.13-17.14 Lévitique 3.16-3.17 Deutéronome 12.16
24 Usiile; imwage juu ya nchi kama maji.
Deutéronome 15.23 Deutéronome 12.16
25 Usiile; ili upate kufanikiwa, na watoto wako baada yako utakapofanya yaliyoelekea machoni pa Bwana.
1 Rois 11.38 Esaïe 3.10 Deutéronome 4.40 Exode 15.26 Deutéronome 13.18
26 Ila vitu vyako vitakatifu ulivyo navyo, na nadhiri zako, uvitwae ukaende mahali atakapochagua Bwana;
Nombres 5.9-5.10 Nombres 18.19 1 Samuel 1.21-1.24 Deutéronome 12.11 Deutéronome 12.17-12.18
27 nawe zisongeze sadaka zako za kuteketezwa, nyama na damu, juu ya madhabahu ya Bwana, Mungu wako; na damu ya dhabihu zako uimwage juu ya madhabahu ya Bwana, Mungu wako, na wewe utakula nyama yake.
Lévitique 17.11 Lévitique 1.13 Lévitique 1.9 Lévitique 1.5 Lévitique 4.30
28 Maneno haya nikuagizayo yote yatunze na kuyasikiza, ili upate kufanikiwa na watoto wako baada yako milele, hapo uyafanyapo yaliyo mema na kuelekea machoni pa Bwana, Mungu wako.
Deutéronome 4.40 Jean 15.10 Ezéchiel 37.24 Lévitique 19.37 2 Chroniques 7.17
29 Bwana, Mungu wako, atakapoyakatilia mbali hayo mataifa mbele yako, huko uingiako kuyamiliki, nawe ukawatwaa, na kuketi katika nchi yao;
Josué 23.4 Deutéronome 19.1 Exode 23.23 Deutéronome 9.3 Psaumes 78.55
30 ujiangalie, usije ukanaswa ukawafuata, wakiisha kuangamizwa mbele yako; wala usije ukauliza habari za miungu yao, ukisema, Mataifa haya waitumikiaje miungu yao? Nami nifanye vivyo.
Deutéronome 7.16 Ephésiens 4.17 2 Rois 17.15 Ezéchiel 20.28 Ezéchiel 20.32
31 Usimtende kama haya Bwana, Mungu wako; kwani kila yaliyo machukizo kwa Bwana, ayachukiayo yeye, wameifanyia miungu yao; kwa maana hata wana wao na binti zao huiteketezea hiyo miungu yao ndani ya moto.
Jérémie 32.35 Deutéronome 12.4 Lévitique 18.3 Jérémie 7.31 Exode 23.2
32 Neno niwaagizalo lo lote liangalieni kulifanya; usiliongeze, wala usilipunguze.
Deutéronome 4.2 Josué 1.7 Proverbes 30.6 Apocalypse 22.18-22.19 Deutéronome 13.18

Cette Bible est dans le domaine public.