Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Corinthiens 6.5
Bible en Swahili de l’est


1 Nasi tukitenda kazi pamoja naye twawasihi msiipokee neema ya Mungu bure.
1 Corinthiens 3.9 Hébreux 12.15 1 Pierre 4.10 Tite 2.11 Matthieu 23.37
2 (Kwa maana asema, Wakati uliokubalika nalikusikia, Siku ya wokovu nalikusaidia;tazama,wakati uliokubalika ndiyo sasa; tazama siku ya wokovu ni sasa)
Esaïe 49.8 Hébreux 4.7 Hébreux 3.13 Hébreux 3.7 Luc 4.19
3 Tusiwe kwazo la namna yo yote katika jambo lo lote, ili utumishi wetu usilaumiwe;
Romains 14.13 1 Corinthiens 9.12 Matthieu 17.27 Matthieu 18.6 1 Corinthiens 9.22
4 bali katika kila neno tujipatie sifa njema, kama watumishi wa Mungu; katika saburi nyingi, katika dhiki, katika misiba, katika shida;
2 Corinthiens 4.8 2 Corinthiens 12.12 1 Corinthiens 3.5 2 Corinthiens 3.6 2 Corinthiens 12.10
5 katika mapigo, katika vifungo, katika fitina, katika taabu, katika kukesha, katika kufunga;
2 Corinthiens 11.23-11.25 Actes 19.23-19.34 Actes 17.5 2 Corinthiens 11.27 Actes 14.23
6 katika kuwa safi, katika elimu, katika uvumilivu, katika utu wema, katika Roho Mtakatifu, katika upendo usio unafiki;
2 Corinthiens 11.6 Romains 12.9 Romains 15.19 1 Thessaloniciens 2.10 1 Corinthiens 2.4
7 katika neno la kweli, katika nguvu ya Mungu; kwa silaha za haki za mkono wa kuume na za mkono wa kushoto;
2 Corinthiens 4.2 Ephésiens 1.13 Colossiens 1.5 Ephésiens 6.11-6.20 2 Timothée 4.7
8 kwa utukufu na aibu; kwa kunenwa vibaya na kunenwa vema; kama wadanganyao, bali tu watu wa kweli;
Matthieu 27.63 Romains 3.8 1 Corinthiens 4.10-4.13 Apocalypse 3.9 1 Timothée 3.7
9 kama wasiojulikana, bali wajulikanao sana; kama wanaokufa, kumbe tu hai; kama wanaorudiwa, bali wasiouawa;
1 Corinthiens 4.9 Romains 8.36 2 Corinthiens 4.10-4.11 2 Corinthiens 11.6 2 Corinthiens 1.8-1.10
10 kama wenye huzuni, bali siku zote tu wenye furaha; kama maskini, bali tukitajirisha wengi; kama wasio na kitu, bali tu wenye vitu vyote.
2 Corinthiens 8.9 Jean 16.22 Philippiens 4.4 1 Timothée 6.18 Romains 15.13

Appel à la sainteté

11 Vinywa vyetu vimefumbuliwa kwenu, enyi Wakorintho; mioyo yetu imekunjuliwa.
2 Corinthiens 12.15 Psaumes 119.32 Job 32.20 Philippiens 1.8 Galates 3.1
12 Hamsongwi ndani yetu, bali mwasongwa katika mioyo yenu.
Michée 2.7 1 Jean 3.17 2 Corinthiens 7.2 Job 36.16 Ecclésiaste 6.9
13 Basi, ili mlipe kadiri ile mliyopewa (nasema nanyi kama na watoto), nanyi pia mkunjuliwe mioyo.
Galates 4.12 Hébreux 12.5-12.6 Matthieu 17.19-17.20 1 Jean 5.14-5.15 3 Jean 1.4
14 Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza?
1 Corinthiens 15.33 1 Corinthiens 10.21 Ephésiens 5.6-5.14 Deutéronome 22.9-22.11 Jacques 4.4
15 Tena pana ulinganifu gani kati ya Kristo na Beliari? Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na yeye asiyeamini?
Actes 5.14 1 Rois 18.21 1 Corinthiens 10.20-10.21 1 Jean 5.11-5.13 Esdras 4.3
16 Tena pana mapatano gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa maana sisi tu hekalu la Mungu aliye hai; kama Mungu alivyosema, ya kwamba, Nitakaa ndani yao, na kati yao nitatembea, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.
Exode 29.45 Apocalypse 21.3 Jérémie 32.38 Lévitique 26.12 Hébreux 8.10
17 Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha.
Esaïe 52.11 Apocalypse 18.4 2 Corinthiens 7.1 Nombres 16.26 Proverbes 9.6
18 Nitakuwa Baba kwenu, Nanyi mtakuwa kwangu wanangu wa kiume na wa kike,
Jean 1.12 Apocalypse 21.7 Esaïe 43.6 Jérémie 31.9 Galates 4.5-4.7

Cette Bible est dans le domaine public.