Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Corinthiens 2.13
Bible en Swahili de l’est


1 Lakini nafsini mwangu nalikusudia hivi, nisije kwenu tena kwa huzuni.
2 Corinthiens 1.23 2 Corinthiens 12.20-12.21 2 Corinthiens 13.10 1 Corinthiens 4.21 1 Corinthiens 2.2
2 Maana mimi nikiwatia huzuni, basi ni nani anifurahishaye mimi ila yeye ahuzunishwaye nami?
2 Corinthiens 7.8 Romains 12.15 2 Corinthiens 1.14 1 Corinthiens 12.26 2 Corinthiens 11.29
3 Nami naliwaandikia neno lilo hilo, ili nijapo nisitiwe huzuni na wale ambao ilinipasa kuwafurahia; nikiwatumaini ninyi nyote kwamba furaha yangu ni yenu nyote pia.
Galates 5.10 2 Corinthiens 8.22 Philémon 1.21 2 Corinthiens 7.8 1 Corinthiens 4.21-5.13
4 Maana katika dhiki nyingi na taabu ya moyo niliwaandikia na machozi mengi; si kwamba mhuzunishwe, bali mpate kujua upendo wangu nilio nao kwenu jinsi ulivyo mwingi.
2 Corinthiens 7.12 Philippiens 3.18 Romains 9.2-9.3 Proverbes 27.5-27.6 Luc 19.41-19.44
5 Lakini iwapo mtu amehuzunisha, hakunihuzunisha mimi tu, bali kwa sehemu (nisije nikalemea mno), amewahuzunisha ninyi nyote.
1 Corinthiens 5.12-5.13 Galates 4.12 1 Corinthiens 5.1-5.5 Proverbes 17.25 Galates 5.10
6 Yamtosha mtu wa namna hii adhabu ile aliyopewa na walio wengi;
1 Corinthiens 5.4-5.5 2 Corinthiens 13.10 2 Corinthiens 7.11 1 Timothée 5.20
7 hata kinyume cha hayo, ni afadhali mmsamehe na kumfariji, mtu kama huyo asije akamezwa katika huzuni yake ipitayo kiasi.
Ephésiens 4.32 Psaumes 56.1-56.2 2 Corinthiens 7.10 Colossiens 3.13 Philippiens 2.27
8 Kwa hiyo nawasihi kumthibitishia upendo wenu.
Jude 1.22-1.23 Galates 6.1-6.2 Galates 5.13 Galates 6.10
9 Maana naliandika kwa sababu hii pia, ili nipate bayana kwenu kwamba mmekuwa wenye kutii katika mambo yote.
2 Corinthiens 10.6 Philippiens 2.22 Deutéronome 8.2 2 Corinthiens 8.24 Deutéronome 8.16
10 Lakini kama mkimsamehe mtu neno lo lote, nami nimemsamehe; kwa maana mimi nami, ikiwa nimemsamehe mtu neno lo lote, nimemsamehe kwa ajili yenu mbele za Kristo,
1 Corinthiens 5.4 Jean 20.23 2 Corinthiens 5.20 Matthieu 18.18
11 Shetani asije akapata kutushinda; kwa maana hatukosi kuzijua fikira zake.
1 Pierre 5.8 Luc 22.31 2 Corinthiens 4.4 Apocalypse 12.9-12.11 Zacharie 3.1-3.4
12 Basi nilipofika Troa kwa ajili ya Injili ya Kristo, nikafunguliwa mlango katika Bwana,
Actes 16.8 Actes 14.27 1 Corinthiens 16.9 Apocalypse 3.7-3.8 Colossiens 4.3
13 sikuona raha nafsini mwangu, kwa sababu sikumwona Tito ndugu yangu, bali niliagana nao, nikaondoka kwenda Makedonia.
2 Corinthiens 7.5-7.6 2 Corinthiens 12.18 2 Corinthiens 8.23 Galates 2.3 2 Corinthiens 8.6

Le ministère de la nouvelle alliance

14 Ila Mungu ashukuriwe, anayetushangiliza daima katika Kristo, na kuidhihirisha harufu ya kumjua yeye kila mahali kwa kazi yetu.
2 Corinthiens 9.15 Romains 8.37 Ephésiens 5.2 Cantique 1.3 2 Corinthiens 8.16
15 Kwa maana sisi tu manukato ya Kristo, mbele za Mungu, katika wao wanaookolewa, na katika wao wanaopotea;
1 Corinthiens 1.18 Ezéchiel 20.41 Ephésiens 5.2 Philippiens 4.18 Esaïe 49.5-49.6
16 katika hao wa pili harufu ya mauti iletayo mauti; katika hao wa kwanza harufu ya uzima iletayo uzima. Naye ni nani atoshaye kwa mambo hayo?
Luc 2.34 2 Corinthiens 3.5-3.6 Jean 9.39 1 Pierre 2.7-2.8 1 Corinthiens 15.10
17 Kwa maana sisi si kama walio wengi, walighoshio neno la Mungu; bali kama kwa weupe wa moyo, kama kutoka kwa Mungu, mbele za Mungu, twanena katika Kristo.
2 Corinthiens 4.2 2 Corinthiens 1.12 Apocalypse 12.9 Matthieu 24.24 Actes 20.20

Cette Bible est dans le domaine public.