Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Corinthiens 2.11
Bible en Swahili de l’est


1 Lakini nafsini mwangu nalikusudia hivi, nisije kwenu tena kwa huzuni.
2 Corinthiens 1.23 2 Corinthiens 13.10 1 Corinthiens 4.21 2 Corinthiens 12.20-12.21 2 Corinthiens 2.4
2 Maana mimi nikiwatia huzuni, basi ni nani anifurahishaye mimi ila yeye ahuzunishwaye nami?
2 Corinthiens 7.8 Romains 12.15 2 Corinthiens 1.14 1 Corinthiens 12.26 2 Corinthiens 11.29
3 Nami naliwaandikia neno lilo hilo, ili nijapo nisitiwe huzuni na wale ambao ilinipasa kuwafurahia; nikiwatumaini ninyi nyote kwamba furaha yangu ni yenu nyote pia.
Galates 5.10 2 Corinthiens 8.22 Philémon 1.21 2 Corinthiens 7.12 2 Corinthiens 7.6
4 Maana katika dhiki nyingi na taabu ya moyo niliwaandikia na machozi mengi; si kwamba mhuzunishwe, bali mpate kujua upendo wangu nilio nao kwenu jinsi ulivyo mwingi.
2 Corinthiens 7.12 Proverbes 27.5-27.6 Luc 19.41-19.44 Jérémie 13.15-13.17 2 Corinthiens 11.2
5 Lakini iwapo mtu amehuzunisha, hakunihuzunisha mimi tu, bali kwa sehemu (nisije nikalemea mno), amewahuzunisha ninyi nyote.
1 Corinthiens 5.12-5.13 Galates 4.12 1 Corinthiens 5.1-5.5 Proverbes 17.25 Galates 5.10
6 Yamtosha mtu wa namna hii adhabu ile aliyopewa na walio wengi;
1 Corinthiens 5.4-5.5 2 Corinthiens 13.10 2 Corinthiens 7.11 1 Timothée 5.20
7 hata kinyume cha hayo, ni afadhali mmsamehe na kumfariji, mtu kama huyo asije akamezwa katika huzuni yake ipitayo kiasi.
Ephésiens 4.32 1 Thessaloniciens 4.13 Proverbes 1.12 Hébreux 12.12-12.15 2 Corinthiens 5.4
8 Kwa hiyo nawasihi kumthibitishia upendo wenu.
Jude 1.22-1.23 Galates 6.1-6.2 Galates 5.13 Galates 6.10
9 Maana naliandika kwa sababu hii pia, ili nipate bayana kwenu kwamba mmekuwa wenye kutii katika mambo yote.
2 Corinthiens 10.6 Philippiens 2.22 Exode 16.4 2 Thessaloniciens 3.14 Philémon 1.21
10 Lakini kama mkimsamehe mtu neno lo lote, nami nimemsamehe; kwa maana mimi nami, ikiwa nimemsamehe mtu neno lo lote, nimemsamehe kwa ajili yenu mbele za Kristo,
1 Corinthiens 5.4 Jean 20.23 2 Corinthiens 5.20 Matthieu 18.18
11 Shetani asije akapata kutushinda; kwa maana hatukosi kuzijua fikira zake.
1 Pierre 5.8 Luc 22.31 Apocalypse 12.9-12.11 2 Corinthiens 4.4 Apocalypse 2.24
12 Basi nilipofika Troa kwa ajili ya Injili ya Kristo, nikafunguliwa mlango katika Bwana,
Actes 16.8 Actes 14.27 1 Corinthiens 16.9 Apocalypse 3.7-3.8 Colossiens 4.3
13 sikuona raha nafsini mwangu, kwa sababu sikumwona Tito ndugu yangu, bali niliagana nao, nikaondoka kwenda Makedonia.
2 Corinthiens 12.18 2 Corinthiens 7.5-7.6 2 Corinthiens 8.6 Tite 1.4 Galates 2.1

Le ministère de la nouvelle alliance

14 Ila Mungu ashukuriwe, anayetushangiliza daima katika Kristo, na kuidhihirisha harufu ya kumjua yeye kila mahali kwa kazi yetu.
2 Corinthiens 9.15 Romains 8.37 Ephésiens 5.2 Romains 6.17 2 Corinthiens 2.15-2.16
15 Kwa maana sisi tu manukato ya Kristo, mbele za Mungu, katika wao wanaookolewa, na katika wao wanaopotea;
1 Corinthiens 1.18 Ezéchiel 20.41 Philippiens 4.18 Ephésiens 5.2 2 Thessaloniciens 2.10
16 katika hao wa pili harufu ya mauti iletayo mauti; katika hao wa kwanza harufu ya uzima iletayo uzima. Naye ni nani atoshaye kwa mambo hayo?
Luc 2.34 2 Corinthiens 3.5-3.6 Jean 9.39 1 Pierre 2.7-2.8 1 Corinthiens 15.10
17 Kwa maana sisi si kama walio wengi, walighoshio neno la Mungu; bali kama kwa weupe wa moyo, kama kutoka kwa Mungu, mbele za Mungu, twanena katika Kristo.
2 Corinthiens 4.2 2 Corinthiens 1.12 Apocalypse 19.20 1 Timothée 4.1-4.3 Tite 1.11

Cette Bible est dans le domaine public.