Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Corinthiens 1.8
Bible en Swahili de l’est


Paul et les Corinthiens

Salutation et louange

1 Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na Timotheo ndugu yetu; kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, pamoja na watakatifu wote walioko katika nchi yote ya Akaya.
Ephésiens 1.1 2 Timothée 1.1 Actes 16.1 1 Corinthiens 16.10 1 Timothée 1.1
2 Neema na iwe kwenu na amani, zitokazo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
Romains 1.7 1 Chroniques 12.18 Ephésiens 6.23 Colossiens 1.2 2 Thessaloniciens 1.2
3 Na ahimidiwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa rehema, Mungu wa faraja yote;
Ephésiens 1.3 1 Pierre 1.3 Jean 10.30 Romains 15.5-15.6 Michée 7.18
4 atufarijiye katika dhiki zetu zote ili nasi tupate kuwafariji wale walio katika dhiki za namna zote, kwa faraja hizo, tunazofarijiwa na Mungu.
2 Corinthiens 7.6-7.7 Esaïe 51.12 Hébreux 12.12 1 Thessaloniciens 5.11 Esaïe 52.9
5 Kwa kuwa kama vile mateso ya Kristo yanavyozidi kwetu, vivyo hivyo faraja yetu inazidi kwa njia ya Kristo.
Colossiens 1.24 Philippiens 3.10 1 Corinthiens 4.10-4.13 Luc 2.25 2 Thessaloniciens 2.16-2.17
6 Lakini ikiwa sisi tu katika dhiki, ni kwa ajili ya faraja yenu na wokovu wenu; au ikiwa twafarijiwa, ni kwa ajili ya faraja yenu; ambayo hutenda kazi yake kwa kustahimili mateso yale yale tuteswayo na sisi.
2 Timothée 2.10 2 Corinthiens 4.15-4.18 2 Corinthiens 1.4 Romains 5.3-5.5 1 Corinthiens 3.21-3.23
7 Na tumaini letu kwa ajili yenu ni imara, tukijua ya kuwa kama vile mlivyo washiriki wa yale mateso, vivyo hivyo mmekuwa washiriki wa zile faraja.
Romains 8.17-8.18 1 Corinthiens 10.13 2 Corinthiens 7.9 2 Thessaloniciens 1.4-1.7 Luc 22.28-22.30
8 Maana ndugu, hatupendi, msijue habari ya dhiki ile iliyotupata katika Asia, ya kwamba tulilemewa mno kuliko nguvu zetu, hata tukakata tamaa ya kuishi.
1 Corinthiens 15.32 Actes 19.23-19.35 1 Corinthiens 16.9 2 Corinthiens 4.7-4.12 1 Corinthiens 4.8
9 Naam, sisi wenyewe tulikuwa na hukumu ya mauti katika nafsi zetu ili tusijitumainie nafsi zetu, bali tumtumaini Mungu, awafufuaye wafu,
Romains 4.17-4.25 2 Corinthiens 3.5 2 Corinthiens 12.7-12.10 Proverbes 28.26 Psaumes 44.5-44.7
10 aliyetuokoa sisi katika mauti kuu namna ile; tena atatuokoa; ambaye tumemtumaini kwamba atazidi kutuokoa;
Romains 15.31 1 Samuel 7.12 Job 5.17-5.22 1 Timothée 4.10 2 Pierre 2.9
11 ninyi nanyi mkisaidiana nasi kwa ajili yetu katika kuomba, ili, kwa sababu ya ile karama tupewayo sisi kwa msaada wa watu wengi, watu wengi watoe shukrani kwa ajili yetu.
Philippiens 1.19 2 Corinthiens 4.15 Philémon 1.22 Actes 12.5 2 Corinthiens 9.11-9.12

Motivations et projets de Paul

12 Kwa maana kujisifu kwetu ni huku, ushuhuda wa dhamiri yetu, ya kwamba kwa utakatifu na weupe wa moyo utokao kwa Mungu; si kwa hekima ya mwili, bali kwa neema ya Mungu; tulienenda katika dunia, na hasa kwenu ninyi.
2 Corinthiens 2.17 1 Corinthiens 2.13 Actes 24.16 Hébreux 13.18 2 Corinthiens 4.2
13 Maana hatuwaandikii ninyi neno, ila yale msomayo, au kuyakiri; nami nataraji ya kuwa mtayakiri hayo hata mwisho;
Philémon 1.6 2 Corinthiens 4.2 2 Corinthiens 5.11 2 Corinthiens 13.6
14 vile vile kama mlivyotukiri kwa sehemu, ya kwamba sisi tu sababu ya kujisifu kwenu, kama ninyi mlivyo kwetu sisi, katika siku ile ya Bwana wetu Yesu.
1 Corinthiens 1.8 2 Corinthiens 2.5 Philippiens 4.1 Philippiens 2.16 2 Corinthiens 5.12
15 Nami nikiwa na tumaini hilo nalitaka kufika kwenu hapo kwanza, ili mpate karama ya pili;
Romains 1.11 1 Corinthiens 4.19 Romains 15.29 1 Corinthiens 11.34 Philippiens 1.25-1.26
16 na kupita kwenu na kuendelea mpaka Makedonia; na tena toka Makedonia kurudi kwenu na kusafirishwa nanyi kwenda Uyahudi.
1 Corinthiens 16.5-16.7 Actes 19.21-19.22 Actes 21.5
17 Basi, nilipokusudia hayo, je! Nalitumia kigeugeu? Au hayo niyakusudiayo, nayakusudia kwa jinsi ya mwili kwamba iwe hivi kwangu, kusema Ndiyo, ndiyo, na Siyo, siyo?
2 Corinthiens 10.2-10.3 Matthieu 5.37 2 Corinthiens 1.18-1.20 2 Corinthiens 1.12 Galates 1.16
18 Lakini kama Mungu alivyo mwaminifu, neno letu kwenu si Ndiyo na siyo.
1 Corinthiens 1.9 Jean 7.28 2 Corinthiens 1.23 2 Corinthiens 2.17 1 Jean 5.20
19 Maana Mwana wa Mungu, Kristo Yesu, aliyehubiriwa katikati yenu na sisi, yaani, mimi na Silwano na Timotheo, hakuwa Ndiyo na siyo; bali katika yeye ni Ndiyo.
Hébreux 13.8 Actes 18.5 Apocalypse 1.17 1 Jean 5.20 1 Jean 1.3
20 Maana ahadi zote za Mungu zilizopo katika yeye ni Ndiyo; tena kwa hiyo katika yeye ni Amin; Mungu apate kutukuzwa kwa sisi.
Apocalypse 3.14 Hébreux 13.8 1 Corinthiens 14.16 Genèse 49.10 Ephésiens 3.8-3.10
21 Basi Yeye atufanyaye imara pamoja nanyi katika Kristo, na kututia mafuta, ni Mungu,
1 Jean 2.27 1 Jean 2.20 2 Corinthiens 5.5 Esaïe 49.8 Psaumes 37.23-37.24
22 naye ndiye aliyetutia muhuri akatupa arabuni ya Roho mioyoni mwetu.
2 Corinthiens 5.5 Ephésiens 4.30 Ephésiens 1.13-1.14 Jean 6.27 Romains 8.14-8.16
23 Lakini mimi namwita Mungu awe shahidi juu ya roho yangu, ya kwamba, kwa kuwahurumia sijafika Korintho.
Romains 1.9 1 Corinthiens 4.21 Galates 1.20 2 Corinthiens 13.10 2 Corinthiens 13.2
24 Si kwamba tunatawala imani yenu; bali tu wasaidizi wa furaha yenu; maana kwa imani yenu mnasimama.
1 Corinthiens 15.1 Romains 11.20 1 Pierre 5.3 Matthieu 23.8-23.10 2 Timothée 2.24-2.26

Cette Bible est dans le domaine public.