Paul et les Corinthiens
Salutation et louange
1 Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na Timotheo ndugu yetu; kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, pamoja na watakatifu wote walioko katika nchi yote ya Akaya.
2 Timothée 1.1 Ephésiens 1.1 1 Timothée 1.1 Colossiens 1.1-1.2 Philippiens 1.1
2 Neema na iwe kwenu na amani, zitokazo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
Romains 1.7 1 Chroniques 12.18 2 Samuel 15.20 1 Corinthiens 1.3 1 Thessaloniciens 1.1
3 Na ahimidiwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa rehema, Mungu wa faraja yote;
Ephésiens 1.3 1 Pierre 1.3 Jean 10.30 Romains 15.5-15.6 Philippiens 2.11
4 atufarijiye katika dhiki zetu zote ili nasi tupate kuwafariji wale walio katika dhiki za namna zote, kwa faraja hizo, tunazofarijiwa na Mungu.
2 Corinthiens 7.6-7.7 Esaïe 51.12 Hébreux 12.12 1 Thessaloniciens 5.11 2 Thessaloniciens 2.16-2.17
5 Kwa kuwa kama vile mateso ya Kristo yanavyozidi kwetu, vivyo hivyo faraja yetu inazidi kwa njia ya Kristo.
Colossiens 1.24 Philippiens 3.10 Philippiens 1.20 2 Corinthiens 4.10-4.11 1 Corinthiens 4.10-4.13
6 Lakini ikiwa sisi tu katika dhiki, ni kwa ajili ya faraja yenu na wokovu wenu; au ikiwa twafarijiwa, ni kwa ajili ya faraja yenu; ambayo hutenda kazi yake kwa kustahimili mateso yale yale tuteswayo na sisi.
2 Timothée 2.10 2 Corinthiens 1.4 2 Corinthiens 4.15-4.18 2 Corinthiens 5.5 Romains 8.28
7 Na tumaini letu kwa ajili yenu ni imara, tukijua ya kuwa kama vile mlivyo washiriki wa yale mateso, vivyo hivyo mmekuwa washiriki wa zile faraja.
Romains 8.17-8.18 1 Corinthiens 10.13 Jacques 1.12 1 Thessaloniciens 1.3-1.4 2 Corinthiens 1.14
8 Maana ndugu, hatupendi, msijue habari ya dhiki ile iliyotupata katika Asia, ya kwamba tulilemewa mno kuliko nguvu zetu, hata tukakata tamaa ya kuishi.
1 Corinthiens 15.32 1 Corinthiens 4.8 Actes 19.23-19.35 1 Corinthiens 16.9 2 Corinthiens 4.7-4.12
9 Naam, sisi wenyewe tulikuwa na hukumu ya mauti katika nafsi zetu ili tusijitumainie nafsi zetu, bali tumtumaini Mungu, awafufuaye wafu,
Romains 4.17-4.25 2 Corinthiens 3.5 Luc 18.9 2 Corinthiens 4.7 2 Corinthiens 12.7-12.10
10 aliyetuokoa sisi katika mauti kuu namna ile; tena atatuokoa; ambaye tumemtumaini kwamba atazidi kutuokoa;
Romains 15.31 Actes 26.21 Psaumes 34.19 1 Samuel 7.12 Job 5.17-5.22
11 ninyi nanyi mkisaidiana nasi kwa ajili yetu katika kuomba, ili, kwa sababu ya ile karama tupewayo sisi kwa msaada wa watu wengi, watu wengi watoe shukrani kwa ajili yetu.Philippiens 1.19 2 Corinthiens 4.15 Philémon 1.22 Actes 12.5 2 Corinthiens 9.11-9.12
Motivations et projets de Paul
12 Kwa maana kujisifu kwetu ni huku, ushuhuda wa dhamiri yetu, ya kwamba kwa utakatifu na weupe wa moyo utokao kwa Mungu; si kwa hekima ya mwili, bali kwa neema ya Mungu; tulienenda katika dunia, na hasa kwenu ninyi.
2 Corinthiens 2.17 1 Corinthiens 2.13 Actes 23.1 Jacques 3.13-3.18 Job 23.10-23.12
13 Maana hatuwaandikii ninyi neno, ila yale msomayo, au kuyakiri; nami nataraji ya kuwa mtayakiri hayo hata mwisho;
2 Corinthiens 13.6 Philémon 1.6 2 Corinthiens 4.2 2 Corinthiens 5.11
14 vile vile kama mlivyotukiri kwa sehemu, ya kwamba sisi tu sababu ya kujisifu kwenu, kama ninyi mlivyo kwetu sisi, katika siku ile ya Bwana wetu Yesu.
1 Corinthiens 1.8 Philippiens 4.1 Philippiens 2.16 2 Corinthiens 5.12 1 Thessaloniciens 2.19-2.20
15 Nami nikiwa na tumaini hilo nalitaka kufika kwenu hapo kwanza, ili mpate karama ya pili;
Romains 1.11 1 Corinthiens 4.19 Romains 15.29 2 Corinthiens 6.1 1 Corinthiens 11.34
16 na kupita kwenu na kuendelea mpaka Makedonia; na tena toka Makedonia kurudi kwenu na kusafirishwa nanyi kwenda Uyahudi.
1 Corinthiens 16.5-16.7 Actes 21.5 Actes 19.21-19.22
17 Basi, nilipokusudia hayo, je! Nalitumia kigeugeu? Au hayo niyakusudiayo, nayakusudia kwa jinsi ya mwili kwamba iwe hivi kwangu, kusema Ndiyo, ndiyo, na Siyo, siyo?
2 Corinthiens 10.2-10.3 Matthieu 5.37 Jérémie 23.32 Jean 8.15 Juges 9.4
18 Lakini kama Mungu alivyo mwaminifu, neno letu kwenu si Ndiyo na siyo.
1 Corinthiens 1.9 2 Corinthiens 11.31 Jean 7.28 2 Corinthiens 1.23 2 Corinthiens 2.17
19 Maana Mwana wa Mungu, Kristo Yesu, aliyehubiriwa katikati yenu na sisi, yaani, mimi na Silwano na Timotheo, hakuwa Ndiyo na siyo; bali katika yeye ni Ndiyo.
Hébreux 13.8 Apocalypse 1.17 Actes 18.5 Marc 1.1 Romains 1.3-1.4
20 Maana ahadi zote za Mungu zilizopo katika yeye ni Ndiyo; tena kwa hiyo katika yeye ni Amin; Mungu apate kutukuzwa kwa sisi.
Apocalypse 3.14 1 Corinthiens 14.16 Hébreux 13.8 1 Pierre 1.12 Galates 3.22
21 Basi Yeye atufanyaye imara pamoja nanyi katika Kristo, na kututia mafuta, ni Mungu,
1 Jean 2.27 1 Jean 2.20 Esaïe 62.7 2 Thessaloniciens 2.17 Apocalypse 3.18
22 naye ndiye aliyetutia muhuri akatupa arabuni ya Roho mioyoni mwetu.
2 Corinthiens 5.5 Ephésiens 4.30 Ephésiens 1.13-1.14 Romains 8.14-8.16 Jean 6.27
23 Lakini mimi namwita Mungu awe shahidi juu ya roho yangu, ya kwamba, kwa kuwahurumia sijafika Korintho.
Romains 1.9 1 Corinthiens 4.21 Galates 1.20 2 Corinthiens 13.10 2 Corinthiens 13.2
24 Si kwamba tunatawala imani yenu; bali tu wasaidizi wa furaha yenu; maana kwa imani yenu mnasimama.
Romains 11.20 1 Pierre 5.3 1 Corinthiens 15.1 Matthieu 23.8-23.10 2 Corinthiens 5.7