Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Corinthiens 2.3
Bible en Swahili de l’est


L’exemple de Paul

1 Basi, ndugu zangu, mimi nilipokuja kwenu, sikuja niwahubiri siri ya Mungu kwa ufasaha wa maneno, wala kwa hekima.
1 Corinthiens 1.17 1 Corinthiens 2.4 1 Corinthiens 2.13 Exode 4.10 1 Timothée 1.11
2 Maana naliazimu nisijue neno lo lote kwenu ila Yesu Kristo, naye amesulibiwa.
Galates 6.14 Philippiens 3.8-3.10 Galates 3.1 1 Corinthiens 1.22-1.25 Jean 17.3
3 Nami nalikuwako kwenu katika hali ya udhaifu na hofu na matetemeko mengi.
2 Corinthiens 13.4 2 Corinthiens 11.29-11.30 2 Corinthiens 10.10 Actes 17.6-17.12 Actes 20.18-20.19
4 Na neno langu na kuhubiri kwangu hakukuwa kwa maneno ya hekima yenye kushawishi akili za watu, bali kwa dalili za Roho na za nguvu,
Romains 15.19 1 Corinthiens 1.17 1 Corinthiens 2.13 1 Corinthiens 4.20 2 Pierre 1.16
5 ili imani yenu isiwe katika hekima ya wanadamu, bali katika nguvu za Mungu.
2 Corinthiens 4.7 2 Corinthiens 6.7 1 Corinthiens 1.17 2 Corinthiens 12.9
6 Walakini iko hekima tusemayo kati ya wakamilifu; ila si hekima ya dunia hii, wala ya hao wanaoitawala dunia hii, wanaobatilika;
1 Corinthiens 1.28 Hébreux 5.14 Jacques 3.15 2 Corinthiens 4.4 Ephésiens 4.11-4.13
7 bali twanena hekima ya Mungu katika siri, ile hekima iliyofichwa, ambayo Mungu aliiazimu tangu milele, kwa utukufu wetu;
Romains 16.25-16.26 Ephésiens 3.4-3.9 Matthieu 11.25 2 Pierre 1.3 1 Pierre 1.11
8 ambayo wenye kuitawala dunia hii hawaijui hata mmoja; maana kama wangaliijua, wasingalimsulibisha Bwana wa utukufu;
Actes 7.2 Jacques 2.1 Actes 13.27 Jean 15.22-15.25 Psaumes 24.7-24.10
9 lakini, kama ilivyoandikwa, Mambo ambayo jicho halikuyaona wala sikio halikuyasikia, (Wala hayakuingia katika moyo wa mwanadamu,) Mambo ambayo Mungu aliwaandalia wampendao.
Esaïe 64.4 Jacques 1.12 Psaumes 31.19 Esaïe 65.17 Jean 3.16
10 Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho huchunguza yote, hata mafumbo ya Mungu.
Ephésiens 3.3 Ephésiens 3.5 Jean 14.26 Matthieu 13.11 Matthieu 16.17
11 Maana ni nani katika binadamu ayajuaye mambo ya binadamu ila roho ya binadamu iliyo ndani yake? Vivyo hivyo na mambo ya Mungu hakuna ayafahamuye ila Roho wa Mungu.
Proverbes 20.27 Jérémie 17.9 Proverbes 14.10 1 Corinthiens 2.10 Romains 11.33-11.34
12 Lakini sisi hatukuipokea roho ya dunia, bali Roho atokaye kwa Mungu, makusudi tupate kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu.
1 Jean 2.27 1 Jean 5.19-5.20 Romains 8.5-8.6 Jean 16.14-16.15 Romains 8.15-8.16
13 Nayo twayanena, si kwa maneno yanayofundishwa kwa hekima ya kibinadamu, bali yanayofundishwa na Roho, tukiyafasiri mambo ya rohoni kwa maneno ya rohoni.
1 Corinthiens 1.17 1 Corinthiens 2.4 1 Corinthiens 2.14 Colossiens 3.16 1 Pierre 1.12
14 Basi mwanadamu wa tabia ya asili hayapokei mambo ya Roho wa Mungu; maana kwake huyo ni upuzi, wala hawezi kuyafahamu, kwa kuwa yatambulikana kwa jinsi ya rohoni.
1 Corinthiens 1.18 Matthieu 13.11-13.17 Romains 8.5-8.8 Jean 6.44-6.45 1 Jean 2.27
15 Lakini mtu wa rohoni huyatambua yote, wala yeye hatambuliwi na mtu.
Galates 6.1 1 Corinthiens 3.1 1 Jean 4.1 1 Thessaloniciens 5.21 1 Corinthiens 14.37
16 Maana, Ni nani aliyeifahamu nia ya Bwana, amwelimishe? Lakini sisi tunayo nia ya Kristo.
Jean 15.15 Romains 11.34 Jean 16.13-16.16 Esaïe 40.13-40.14 Jean 17.6-17.8

Cette Bible est dans le domaine public.