Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Romains 5.18
Bible en Swahili de l’est


Fruits de la justice obtenue par la foi

1 Basi tukiisha kuhesabiwa haki itokayo katika imani, na mwe na amani kwa Mungu, kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,
Romains 15.13 Romains 6.23 Esaïe 32.17 Actes 13.38-13.39 Romains 14.17
2 ambaye kwa yeye tumepata kwa njia ya imani kuifikia neema hii ambayo mnasimama ndani yake; na kufurahi katika tumaini la utukufu wa Mungu.
Ephésiens 2.18 Ephésiens 3.12 1 Corinthiens 15.1 Jean 5.24 1 Pierre 3.18
3 Wala si hivyo tu, ila na mfurahi katika dhiki pia; mkijua ya kuwa dhiki, kazi yake ni kuleta saburi;
Jacques 1.2-1.3 Jacques 1.12 2 Corinthiens 12.9-12.10 Luc 6.22-6.23 1 Pierre 3.14
4 na kazi ya saburi ni uthabiti wa moyo; na kazi ya uthabiti wa moyo ni tumaini;
Jacques 1.12 Psaumes 42.4-42.5 1 Pierre 5.10 2 Corinthiens 4.8-4.12 Josué 10.24-10.25
5 na tumaini halitahayarishi; kwa maana pendo la Mungu limekwisha kumiminwa katika mioyo yetu na Roho Mtakatifu tuliyepewa sisi.
Philippiens 1.20 Job 27.8 2 Timothée 1.12 Galates 4.6 1 Jean 4.19
6 Kwa maana hapo tulipokuwa hatuna nguvu, wakati ulipotimia, Kristo alikufa kwa ajili ya waovu.
Romains 5.8 Ephésiens 2.1-2.5 Colossiens 2.13 Romains 4.25 Romains 5.10
7 Kwa kuwa ni shida mtu kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki; lakini yawezekana mtu kuthubutu kufa kwa ajili ya mtu aliye mwema.
Psaumes 112.5 Actes 11.24 2 Samuel 23.14-23.17 1 Jean 3.16 2 Samuel 18.3
8 Bali Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi.
Jean 15.13 Jean 3.16 Romains 5.6 1 Pierre 3.18 1 Jean 3.16
9 Basi zaidi sana tukiisha kuhesabiwa haki katika damu yake, tutaokolewa na ghadhabu kwa yeye.
1 Thessaloniciens 1.10 Romains 1.18 Romains 5.1 Hébreux 9.22 Romains 8.1
10 Kwa maana ikiwa tulipokuwa adui tulipatanishwa na Mungu kwa mauti ya Mwana wake; zaidi sana baada ya kupatanishwa tutaokolewa katika uzima wake.
2 Corinthiens 5.18-5.19 Ephésiens 2.16 Romains 8.32 Colossiens 1.20-1.21 2 Corinthiens 4.10-4.11
11 Wala si hivyo tu, ila pia twajifurahisha katika Mungu kwa Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye kwa yeye sasa tumeupokea huo upatanisho.
2 Corinthiens 5.18-5.19 Romains 5.10 Esaïe 61.10 Philippiens 4.4 Habakuk 3.17-3.18
12 Kwa hiyo, kama kwa mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi;
1 Corinthiens 15.21-15.22 Romains 5.19 Romains 6.23 Genèse 2.17 1 Jean 1.8-1.10
13 maana kabla ya sheria dhambi ilikuwamo ulimwenguni, lakini dhambi haihesabiwi isipokuwapo sheria;
Romains 4.15 1 Corinthiens 15.56 Genèse 13.13 Genèse 19.36 Genèse 8.21
14 walakini mauti ilitawala tangu Adamu mpaka Musa, nayo iliwatawala hata wao wasiofanya dhambi ifananayo na kosa la Adamu, aliye mfano wake yeye atakayekuja.
1 Corinthiens 15.45 Exode 12.29-12.30 Romains 8.20 Romains 8.22 Exode 1.22
15 Lakini karama ile haikuwa kama lile kosa; kwa maana ikiwa kwa kukosa kwake yule mmoja wengi walikufa, zaidi sana neema ya Mungu, na kipawa kilicho katika neema yake mwanadamu mmoja Yesu Kristo kimezidi kwa ajili ya wale wengi.
Romains 6.23 Romains 5.12 1 Jean 5.11 Esaïe 53.11 Romains 5.16-5.20
16 Wala kadiri ya yule mtu mmoja aliyefanya dhambi si kadiri ya kile kipawa; kwa maana hukumu ilikuja kwa njia ya mtu mmoja ikaleta adhabu; bali karama ya neema ilikuja kwa ajili ya makosa mengi, ikaleta kuhesabiwa haki.
Actes 13.38-13.39 Jacques 2.10 Genèse 3.6-3.19 Luc 7.47-7.50 Galates 3.10
17 Kwa maana ikiwa kwa kukosa mtu mmoja mauti ilitawala kwa sababu ya yule mmoja, zaidi sana wao wapokeao wingi wa neema, na kile kipawa cha haki, watatawala katika uzima kwa yule mmoja, Yesu Kristo.
Romains 5.12 Apocalypse 22.5 Genèse 3.6 1 Corinthiens 15.21-15.22 Genèse 3.19
18 Basi tena, kama kwa kosa moja watu wote walihukumiwa adhabu, kadhalika kwa tendo moja la haki watu wote walihesabiwa haki yenye uzima.
Romains 5.12 Romains 4.25 1 Timothée 2.4-2.6 Romains 5.19 Romains 5.15
19 Kwa sababu kama kwa kuasi kwake mtu mmoja watu wengi waliingizwa katika hali ya wenye dhambi, kadhalika kwa kutii kwake mmoja watu wengi wameingizwa katika hali ya wenye haki.
2 Corinthiens 5.21 Philippiens 2.8 Ephésiens 1.6 Romains 5.15 Daniel 9.24
20 Lakini sheria iliingia ili kosa lile liwe kubwa sana; na dhambi ilipozidi, neema ilikuwa nyingi zaidi;
Romains 6.1 Psaumes 25.11 Tite 3.3-3.7 Romains 6.14 Galates 3.19-3.25
21 ili kwamba, kama vile dhambi ilivyotawala katika mauti, vivyo hivyo kwa njia ya haki neema itawale hata uzima wa milele kwa Yesu Kristo Bwana wetu.
Romains 5.14 Romains 6.23 Romains 5.12 Tite 2.11 Jean 1.16-1.17

Cette Bible est dans le domaine public.