Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jean 15.17
Bible en Swahili de l’est


Le cep et les sarments

1 Mimi ndimi mzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mkulima.
Jérémie 2.21 Esaïe 27.2-27.3 Jean 1.17 Psaumes 80.8-80.19 Esaïe 5.1-5.7
2 Kila tawi ndani yangu lisilozaa huliondoa; na kila tawi lizaalo hulisafisha, ili lizidi kuzaa.
Matthieu 3.10 Matthieu 15.13 Hébreux 12.10-12.11 Apocalypse 3.19 Hébreux 6.7-6.8
3 Ninyi mmekwisha kuwa safi kwa sababu ya lile neno nililowaambia.
Ephésiens 5.26 Jean 17.17 Jean 13.10 1 Pierre 1.22
4 Kaeni ndani yangu, nami ndani yenu. Kama vile tawi lisivyoweza kuzaa peke yake, lisipokaa ndani ya mzabibu; kadhalika nanyi, msipokaa ndani yangu.
Galates 2.20 1 Jean 2.6 2 Jean 1.9 Ezéchiel 15.2-15.5 Jean 6.56
5 Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote.
Philippiens 4.13 Colossiens 1.10 2 Pierre 1.2-1.18 Proverbes 11.30 Jacques 1.17
6 Mtu asipokaa ndani yangu, hutupwa nje kama tawi na kunyauka; watu huyakusanya na kuyatupa motoni yakateketea.
Jean 15.2 Matthieu 7.19 Hébreux 6.7-6.8 Matthieu 13.41 1 Jean 2.19
7 Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa.
Psaumes 37.4 Jean 14.13 1 Jean 5.14 1 Jean 3.22 Jean 15.16
8 Hivyo hutukuzwa Baba yangu, kwa vile mzaavyo sana; nanyi mtakuwa wanafunzi wangu.
Jean 8.31 Matthieu 5.16 2 Corinthiens 9.10-9.15 Philippiens 1.11 1 Pierre 4.11
9 Kama vile Baba alivyonipenda mimi, nami nilivyowapenda ninyi, kaeni katika pendo langu.
Jean 17.26 Jean 17.23-17.24 1 Jean 2.28 Jean 15.11 Ephésiens 3.18
10 Mkizishika amri zangu, mtakaa katika pendo langu; kama vile mimi nilivyozishika amri za Baba yangu na kukaa katika pendo lake.
Jean 14.15 2 Pierre 2.21 Jean 4.34 Apocalypse 22.14 1 Jean 3.21-3.24
11 Hayo nimewaambia, ili furaha yangu iwe ndani yenu, na furaha yenu itimizwe.
Jean 17.13 Jean 16.24 1 Pierre 1.8 Romains 15.13 1 Jean 1.4
12 Amri yangu ndiyo hii, Mpendane, kama nilivyowapenda ninyi.
Jean 13.34 1 Pierre 4.8 1 Jean 4.21 1 Jean 3.23 Romains 12.10
13 Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.
Jean 10.11 Ephésiens 5.2 Jean 10.15 Romains 5.6-5.8 1 Jean 4.7-4.11
14 Ninyi mmekuwa rafiki zangu, mkitenda niwaamuruyo.
Matthieu 12.50 Luc 12.4 1 Jean 5.3 Jean 2.5 Jean 14.15
15 Siwaiti tena watumwa; kwa maana mtumwa hajui atendalo bwana wake; lakini ninyi nimewaita rafiki; kwa kuwa yote niliyoyasikia kwa Baba yangu nimewaarifu.
Psaumes 25.14 Genèse 18.17-18.19 Matthieu 13.11 Colossiens 1.26 1 Corinthiens 2.9-2.12
16 Si ninyi mlionichagua mimi, bali ni mimi niliyewachagua ninyi; nami nikawaweka mwende mkazae matunda; na matunda yenu yapate kukaa; ili kwamba lo lote mmwombalo Baba kwa jina langu awapeni.
2 Timothée 3.15-3.17 Jean 15.19 Jean 6.70 Jean 13.18 Luc 6.13
17 Haya nawaamuru ninyi, mpate kupendana.
Jean 15.12 1 Jean 3.14-3.17 1 Pierre 2.17

L’œuvre du Saint-Esprit et la mort de Jésus

18 Iwapo ulimwengu ukiwachukia, mwajua ya kuwa umenichukia mimi kabla ya kuwachukia ninyi.
1 Jean 3.13 Jean 7.7 Marc 13.13 1 Jean 3.1 1 Rois 22.8
19 Kama mngekuwa wa ulimwengu, ulimwengu ungewapenda walio wake; lakini kwa kuwa ninyi si wa ulimwengu, bali mimi naliwachagua katika ulimwengu, kwa sababu hiyo ulimwengu huwachukia.
Jean 15.16 1 Jean 4.4-4.5 Jean 17.14-17.16 Ephésiens 1.4-1.11 Tite 3.3-3.7
20 Likumbukeni lile neno nililowaambia, Mtumwa si mkubwa kuliko bwana wake. Ikiwa waliniudhi mimi, watawaudhi ninyi; ikiwa walilishika neno langu watalishika na lenu.
2 Timothée 3.12 Ezéchiel 3.7 2 Corinthiens 4.9 1 Thessaloniciens 2.15 Jean 13.16
21 Lakini haya yote watawatenda kwa ajili ya jina langu, kwa kuwa hawamjui yeye aliyenipeleka.
Matthieu 10.22 Jean 16.3 Matthieu 24.9 Jean 8.19 Actes 5.41
22 Kama nisingalikuja na kusema nao, wasingalikuwa na dhambi; lakini sasa hawana udhuru kwa dhambi yao.
Jean 9.41 Romains 1.20 Jacques 4.17 Jean 19.11 1 Pierre 2.16
23 Yeye anichukiaye mimi humchukia na Baba yangu.
Jean 8.40-8.42 1 Jean 2.23 2 Jean 1.9
24 Kama nisingalitenda kwao kazi asizozitenda mtu mwingine, wasingalikuwa na dhambi; lakini sasa wametuona mimi na Baba yangu, na kutuchukia.
Jean 9.32 Jean 14.9 Jean 10.37 Jean 5.36 Jean 7.31
25 Lakini litimie lile neno lililoandikwa katika torati yao, Walinichukia bure.
Psaumes 109.3 Psaumes 69.4 Psaumes 35.19 2 Corinthiens 11.7 Jean 10.34
26 Lakini ajapo huyo Msaidizi, nitakayewapelekea kutoka kwa Baba, huyo Roho wa kweli atokaye kwa Baba, yeye atanishuhudia.
Jean 14.26 Jean 14.16-14.17 Jean 16.13-16.15 Actes 2.32-2.33 Apocalypse 22.1
27 Nanyi pia mnashuhudia, kwa kuwa tangu mwanzo mmekuwapo pamoja nami.
1 Jean 4.14 1 Jean 1.1-1.2 Jean 21.24 Luc 24.48 Actes 23.11

Cette Bible est dans le domaine public.