Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Matthieu 28.7
Bible en Swahili de l’est


Résurrection de Jésus

1 Hata sabato ilipokwisha, ikipambazuka siku ya kwanza ya juma, Mariamu Magdalene, na Mariamu yule wa pili, walikwenda kulitazama kaburi.
Matthieu 27.61 Matthieu 27.56 Luc 24.22 Jean 20.1-20.10 Luc 23.56-24.10
2 Na tazama, palikuwa na tetemeko kubwa la nchi; kwa sababu malaika wa Bwana alishuka kutoka mbinguni, akaja akalivingirisha lile jiwe akalikalia.
Actes 16.26 Jean 20.12-20.13 1 Pierre 1.12 Jean 20.1 Luc 24.2-24.5
3 Na sura yake ilikuwa kama umeme, na mavazi yake meupe kama theluji.
Marc 9.3 Actes 1.10 Marc 16.5 Jean 20.12 Apocalypse 1.14-1.16
4 Na kwa kumwogopa, wale walinzi wakatetemeka, wakawa kama wafu.
Apocalypse 1.17 Actes 9.3-9.7 Psaumes 48.6 Matthieu 27.65-27.66 Actes 16.29
5 Malaika akajibu, akawaambia wale wanawake, Msiogope ninyi; kwa maana najua ya kuwa mnamtafuta Yesu aliyesulibiwa.
Hébreux 1.14 Jean 20.13-20.15 Psaumes 105.3-105.4 Esaïe 35.4 Matthieu 28.10
6 Hayupo hapa; kwani amefufuka kama alivyosema. Njoni, mpatazame mahali alipolazwa.
Matthieu 16.21 Matthieu 27.63 Matthieu 17.9 Luc 24.23 Luc 24.12
7 Nanyi nendeni upesi, mkawaambie wanafunzi wake, Amefufuka katika wafu. Tazama, awatangulia kwenda Galilaya; ndiko mtakakomwona. Haya, nimekwisha waambia.
Matthieu 28.10 Matthieu 26.32 Matthieu 28.16-28.17 Marc 16.10 Jean 14.29
8 Wakaondoka upesi kutoka kaburini, kwa hofu na furaha nyingi, wakaenda mbio kuwapasha wanafunzi wake habari.
Psaumes 2.11 Jean 16.22 Esdras 3.12-3.13 Jean 20.20-20.21 Marc 16.8
9 Na tazama, Yesu akakutana nao, akisema, Salamu! Wakakaribia wakamshika miguu, wakamsujudia.
Luc 24.52 Jean 20.28 Jean 20.14-20.17 Matthieu 28.17 Marc 16.9-16.10
10 Kisha Yesu akawaambia, Msiogope; enendeni, mkawaambie ndugu zangu waende Galilaya, ndiko watakakoniona.
Jean 20.17 Romains 8.29 Matthieu 28.5 Matthieu 14.27 Matthieu 28.7
11 Nao wale walipokuwa wakienda, tazama, baadhi ya askari waliingia mjini, wakawapasha wakuu wa makuhani habari za mambo yote yaliyotendeka.
Matthieu 27.65-27.66 Matthieu 28.4
12 Wakakusanyika pamoja na wazee, wakafanya shauri, wakawapa askari fedha nyingi,
Psaumes 2.1-2.7 Matthieu 27.1-27.2 Actes 4.5-4.22 Matthieu 26.3-26.4 Matthieu 27.62-27.64
13 wakisema, Semeni, ya kwamba wanafunzi wake walikuja usiku, wakamwiba, sisi tulipokuwa tumelala.
Matthieu 26.64
14 Na neno hili likisikilikana kwa liwali, sisi tutasema naye, nanyi tutawaondolea wasiwasi.
Matthieu 27.2 Actes 12.19
15 Basi wakazitwaa zile fedha, wakafanya kama walivyofundishwa. Na neno hilo likaenea kati ya Wayahudi hata leo.
Matthieu 27.8 Matthieu 26.15 1 Timothée 6.10

Mission confiée aux disciples

16 Na wale wanafunzi kumi na mmoja wakaenda Galilaya mpaka mlima ule aliowaagiza Yesu.
Matthieu 26.32 Matthieu 28.10 Matthieu 28.7 Actes 1.13-1.26 Marc 16.14
17 Nao walipomwona, walimsujudia; lakini baadhi yao waliona shaka.
Matthieu 28.9 Jean 5.23 Psaumes 45.11 Psaumes 2.12 Matthieu 16.28
18 Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.
1 Pierre 3.22 Ephésiens 1.20-1.22 Jean 3.35 Matthieu 11.27 1 Corinthiens 15.27
19 Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;
Marc 16.15-16.16 Actes 13.46-13.47 Actes 2.38-2.39 Actes 1.8 Actes 2.41
20 na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.
Esaïe 41.10 Actes 18.9-18.10 Josué 1.5 Genèse 39.2-39.3 Matthieu 18.20

Cette Bible est dans le domaine public.