Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Matthieu 18.35
Bible en Swahili de l’est


Petits et grands dans le royaume des cieux

1 Saa ile wanafunzi wakamwendea Yesu wakisema,
Matthieu 20.20-20.28 Luc 9.46-9.48 Marc 9.33-9.37 Luc 22.24-22.27 Marc 10.14-10.15
2 Ni nani basi aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni? Akaita mtoto mmoja, akamweka katikati yao,
Matthieu 19.13-19.14 Jérémie 1.7 Marc 9.36-9.37 1 Rois 3.7
3 akasema, Amin, nawaambia, Msipoongoka na kuwa kama vitoto, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni.
1 Pierre 2.2 Marc 10.14-10.15 Matthieu 19.14 1 Corinthiens 14.20 Luc 18.16-18.17
4 Basi, ye yote ajinyenyekeshaye mwenyewe kama mtoto huyu, huyo ndiye aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni.
Matthieu 23.11-23.12 Luc 9.48 Matthieu 18.1 Psaumes 131.1-131.2 Marc 10.43
5 Na ye yote atakayempokea mtoto mmoja mfano wa huyu kwa jina langu, anipokea mimi;
Galates 4.14 Matthieu 25.40 Luc 9.48 Luc 17.1-17.2 Matthieu 10.40-10.42
6 bali atakayemkosesha mmojawapo wa wadogo hawa waniaminio, yamfaa afungiwe shingoni jiwe kubwa la kusagia, na kutoswa katika kilindi cha bahari.
Marc 9.42 Psaumes 105.15 Romains 14.13-14.15 2 Thessaloniciens 1.6-1.9 Matthieu 18.10
7 Ole ni wa ulimwengu kwa sababu ya mambo ya kukosesha! Maana hayana budi kuja mambo ya kukosesha; lakini ole wake mtu yule aliletaye jambo la kukosesha!
Luc 17.1 1 Corinthiens 11.19 Matthieu 26.24 2 Timothée 3.1-3.5 Genèse 13.7
8 Basi mkono wako au mguu wako ukikukosesha, ukate ukautupe mbali nawe; ni afadhali kuingia katika uzima hali umepungukiwa na mkono au mguu, kuliko kuwa na mikono miwili au miguu miwili, na kutupwa katika moto wa milele.
Matthieu 5.29-5.30 Matthieu 25.41 Apocalypse 14.10 Apocalypse 20.15 Luc 16.24
9 Na jicho lako likikukosesha, ling’oe, ukalitupe mbali nawe; ni afadhali kuingia katika uzima una chongo, kuliko kuwa na macho mawili, na kutupwa katika jehanum ya moto.
Matthieu 5.29 Matthieu 18.8 Matthieu 5.22 Marc 9.47 Matthieu 16.26
10 Angalieni msidharau mmojawapo wadogo hawa; kwa maana nawaambia ya kwamba malaika wao mbinguni siku zote huutazama uso wa Baba yangu aliye mbinguni.
Hébreux 1.14 Psaumes 91.11 Psaumes 34.7 Romains 14.10 1 Thessaloniciens 4.8
11 [Kwa maana Mwana wa Adamu alikuja kukiokoa kilichopotea.]
12 Mwaonaje? Mtu akiwa na kondoo mia, mmoja akampotea, je! Hawaachi wale tisa na tisini, akaenda milimani, na kumtafuta yule aliyepotea?
Luc 15.4-15.7 Ezéchiel 34.12 Ezéchiel 34.28 Ezéchiel 34.16 Jérémie 50.6
13 Hata akipata kumwona, amin, nawaambia, amfurahia huyo zaidi, kuliko wale tisa na tisini wasiopotea.
Jean 4.34-4.36 Jacques 2.13 Sophonie 3.17 Esaïe 62.5 Luc 15.23-15.24
14 Vivyo hivyo haipendezi mbele za Baba yenu aliye mbinguni kwamba mmoja wa wadogo hawa apotee.
Jean 17.12 2 Pierre 3.9 Ephésiens 1.5-1.7 Romains 8.28-8.39 Matthieu 6.32

Le pardon

15 Na ndugu yako akikukosa, enenda ukamwonye, wewe na yeye peke yenu; akikusikia, umempata nduguyo.
Lévitique 19.17 Colossiens 3.13 2 Thessaloniciens 3.15 Luc 17.3-17.4 Lévitique 6.2-6.7
16 La, kama hasikii, chukua pamoja nawe tena mtu mmoja au wawili, ili kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu kila neno lithibitike.
Deutéronome 19.15 2 Corinthiens 13.1 Hébreux 10.28 1 Timothée 5.19 Jean 8.17
17 Na asipowasikiliza wao, liambie kanisa; na asipolisikiliza kanisa pia, na awe kwako kama mtu wa mataifa na mtoza ushuru.
2 Thessaloniciens 3.6 1 Corinthiens 5.3-5.5 Ephésiens 5.11-5.12 Esdras 6.21 1 Corinthiens 5.9-6.7
18 Amin, nawaambieni, yo yote mtakayoyafunga duniani yatakuwa yamefungwa mbinguni; na yo yote mtakayoyafungua duniani yatakuwa yamefunguliwa mbinguni.
Matthieu 16.19 Jean 20.23 2 Corinthiens 2.10 Apocalypse 3.7-3.8
19 Tena nawaambia, ya kwamba wawili wenu watakapopatana duniani katika jambo lo lote watakaloliomba, watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni.
1 Jean 5.14-5.16 Jacques 5.14-5.16 Marc 11.24 Matthieu 7.7 Ephésiens 6.18-6.20
20 Kwa kuwa walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu, nami nipo papo hapo katikati yao.
Jean 20.26 Apocalypse 21.3 1 Corinthiens 5.4 Jean 20.19 Exode 20.24
21 Kisha Petro akamwendea akamwambia, Bwana, ndugu yangu anikose mara ngapi nami nimsamehe? Hata mara saba?
Luc 17.3-17.4 Matthieu 18.15
22 Yesu akamwambia, Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini.
Colossiens 3.13 Ephésiens 4.31-5.1 Matthieu 6.14-6.15 Marc 11.25 Matthieu 6.11-6.12
23 Kwa sababu hii ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyetaka kufanya hesabu na watumwa wake.
Matthieu 13.24 Matthieu 25.19-25.30 Matthieu 13.47 2 Corinthiens 5.10-5.11 Matthieu 3.2
24 Alipoanza kuifanya, aliletewa mtu mmoja awiwaye talanta elfu kumi.
Luc 7.41-7.42 Psaumes 40.12 Luc 13.4 Luc 16.5 1 Chroniques 29.7
25 Naye alipokosa cha kulipa, bwana wake akaamuru auzwe, yeye na mkewe na watoto wake, na vitu vyote alivyo navyo, ikalipwe ile deni.
2 Rois 4.1 Néhémie 5.5 Lévitique 25.39 Néhémie 5.8 Luc 7.42
26 Basi yule mtumwa akaanguka, akamsujudia akisema, Bwana, nivumilie, nami nitakulipa yote pia.
Luc 7.43 Matthieu 8.2 Romains 10.3 Matthieu 18.29
27 Bwana wa mtumwa yule akamhurumia, akamfungua, akamsamehe ile deni.
Psaumes 145.8 Néhémie 9.17 Osée 11.8 Juges 10.16 Psaumes 86.15
28 Mtumwa yule akatoka, akamwona mmoja wa wajoli wake, aliyemwia dinari mia akamkamata,akamshika koo,akisema Nilipe uwiwacho.
Matthieu 20.2 Néhémie 10.31 Esaïe 58.3 Deutéronome 15.2 Ezéchiel 45.9
29 Basi mjoli wake akaanguka miguuni pake, akamsihi, akisema, Nivumilie, nami nitakulipa yote pia.
Matthieu 18.26 Matthieu 6.12 Philémon 1.18-1.19
30 Lakini hakutaka, akaenda, akamtupa kifungoni, hata atakapoilipa ile deni.
1 Rois 21.27-21.29 1 Rois 22.27
31 Basi wajoli wake walipoyaona yaliyotendeka, walisikitika sana, wakaenda wakamweleza bwana wao yote yaliyotendeka.
Genèse 37.2 Hébreux 13.17 Marc 3.5 Jérémie 9.1 Luc 19.41
32 Ndipo bwana wake akamwita, akamwambia, Ewe mtumwa mwovu, nalikusamehe wewe deni ile yote, uliponisihi;
Luc 19.22 Matthieu 25.26 Romains 3.19
33 nawe, je! Haikukupasa kumrehemu mjoli wako, kama mimi nilivyokurehemu wewe?
Colossiens 3.13 Ephésiens 4.32-5.2 Matthieu 6.12 Matthieu 5.44-5.45 Luc 6.35-6.36
34 Bwana wake akaghadhibika, akampeleka kwa watesaji, hata atakapoilipa deni ile yote.
Matthieu 5.25-5.26 Luc 12.58-12.59 Matthieu 18.30 Apocalypse 14.10-14.11 2 Thessaloniciens 1.8-1.9
35 Ndivyo na Baba yangu wa mbinguni atakavyowatenda ninyi, msiposamehe kwa mioyo yenu kila mtu ndugu yake.
Luc 6.37-6.38 Matthieu 6.14-6.15 Marc 11.25 Matthieu 7.1-7.2 Matthieu 6.12

Cette Bible est dans le domaine public.