Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Aggée 1.1
Bible en Swahili de l’est


Appel à reconstruire le temple

1 Katika mwaka wa pili wa Dario mfalme, mwezi wa sita, siku ya kwanza ya mwezi, neno la Bwana lilimjia Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, liwali wa Yuda, na Yoshua, mwana wa Yehosadaki, kuhani mkuu, kwa kinywa chake Hagai nabii, kusema,
Esdras 2.2 Aggée 2.10 Esdras 3.8 Esdras 3.2 Matthieu 1.12-1.13
2 Bwana wa majeshi asema hivi, ya kwamba, Watu hawa husema, Huu sio wakati utupasao kuja, huu sio wakati wa kujenga nyumba ya Bwana.
Néhémie 4.10 Nombres 13.31 Ecclésiaste 9.10 Cantique 5.2-5.3 Proverbes 22.13
3 Ndipo neno la Bwana lilikuja kwa kinywa cha nabii Hagai, kusema,
Esdras 5.1 Zacharie 1.1
4 Je! Huu ndio wakati wa ninyi kukaa katika nyumba zenye mapambo ya mbao, iwapo nyumba hii inakaa hali ya kuharibika?
2 Samuel 7.2 Psaumes 132.3-132.5 Matthieu 6.33 Lamentations 4.1 Michée 3.12
5 Basi sasa, Bwana wa majeshi asema hivi, Zitafakarini njia zenu.
Lamentations 3.40 Daniel 10.12 Exode 7.23 Galates 6.4 Ezéchiel 40.4
6 Mmepanda mbegu nyingi mkavuna kidogo; mnakula lakini hamshibi; mnakunywa lakini hamkujazwa na vinywaji; mnajivika nguo lakini hapana aonaye moto; na yeye apataye mshahara apata mshahara ili kuutia katika mfuko uliotoboka-toboka.
Aggée 2.16 Malachie 3.9-3.11 Deutéronome 28.38-28.40 Aggée 1.9 Osée 8.7
7 Bwana wa majeshi asema hivi, Zitafakarini njia zenu.
Aggée 1.5 Psaumes 119.59-119.60 Esaïe 28.10 Philippiens 3.1
8 Pandeni milimani, mkalete miti, mkaijenge nyumba; nami nitaifurahia, nami nitatukuzwa, asema Bwana.
Psaumes 132.13-132.14 Aggée 2.7 Jonas 3.1-3.2 Jean 13.31-13.32 Matthieu 3.8-3.9
9 Mlitazamia vingi, kumbe vikatokea vichache; tena mlipovileta nyumbani nikavipeperusha. Ni kwa sababu gani? Asema Bwana wa majeshi. Ni kwa sababu ya nyumba yangu inayokaa hali ya kuharibika, wakati ambapo ninyi mnakimbilia kila mtu nyumbani kwake.
Aggée 1.4 Aggée 1.6 Esaïe 40.7 2 Rois 19.7 1 Corinthiens 11.30-11.32
10 Basi, kwa ajili yenu mbingu zimezuiliwa zisitoe umande, nayo nchi imezuiliwa isitoe matunda yake.
Lévitique 26.19 1 Rois 17.1 Deutéronome 28.23-28.24 Joël 1.18-1.20 1 Rois 8.35
11 Nami nikaita wakati wa joto uje juu ya nchi, na juu ya milima, na juu ya nafaka, na juu ya divai mpya, na juu ya mafuta, na juu ya kila kitu itoacho nchi, na juu ya wanadamu, na juu ya wanyama, na juu ya kazi zote za mikono.
Aggée 2.17 Deutéronome 28.22 2 Rois 8.1 1 Rois 17.1 Amos 7.4
12 Ndipo Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, na Yoshua, mwana wa Yehosadaki, kuhani mkuu, pamoja na hayo mabaki yote ya watu, wakaitii sauti ya Bwana, Mungu wao, na maneno ya Hagai nabii, kama Bwana, Mungu wao, alivyomtuma; nao watu wakaogopa mbele za Bwana.
Aggée 1.14 Esaïe 50.10 Aggée 2.2 Esdras 5.2 Ecclésiaste 12.13
13 Ndipo Hagai mjumbe wa Bwana, katika ujumbe wa Bwana, akawaambia watu, akisema, Mimi nipo pamoja nanyi, asema Bwana.
Romains 8.31 Malachie 2.7 Esaïe 43.2 Esaïe 41.10 Ezéchiel 3.17
14 Bwana akaiamsha roho ya Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, liwali wa Yuda, na roho ya Yoshua, mwana wa Yehosadaki, kuhani mkuu, na roho zao mabaki ya watu; wakaenda, wakafanya kazi katika nyumba ya Bwana wa majeshi, Mungu wao;
Aggée 2.21 Esdras 5.2 Aggée 1.1 2 Chroniques 36.22 Esdras 5.8
15 katika siku ya ishirini na nne ya mwezi, katika mwezi wa sita, katika mwaka wa pili wa Dario mfalme.
Aggée 1.1 Aggée 2.20 Aggée 2.10 Aggée 2.1

Cette Bible est dans le domaine public.