Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Lévitique 20.13
Bible en Swahili de l’est


Peines contre diverses fautes

1 Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
2 Tena uwaambie wana wa Israeli, Mtu awaye yote miongoni mwa wana wa Israeli, au miongoni mwa wageni waketio katika Israeli, atakayetoa katika kizazi chake na kumpa Moleki, sharti atauawa; wenyeji wa nchi watampiga kwa mawe.
Deutéronome 21.21 Lévitique 18.21 Lévitique 24.23 Lévitique 20.27 Lévitique 24.14
3 Mimi nami nitamkazia uso wangu mtu huyo, nami nitamkatilia mbali na watu wake; kwa kuwa ametoa katika kizazi chake na kumpa Moleki, ili kupatia unajisi patakatifu pangu, na kulinajisi jina langu takatifu.
Lévitique 18.21 Ezéchiel 23.38-23.39 Ezéchiel 5.11 Lévitique 17.10 Ezéchiel 20.39
4 Tena kama wenyeji wa nchi wakimfumbia macho mtu huyo kwa njia yo yote, hapo atoapo katika kizazi chake na kumpa Moleki, wasimwue;
Deutéronome 17.2-17.5 Actes 17.30 Josué 7.12 Apocalypse 2.14 Deutéronome 13.8
5 ndipo mimi nitamkazia uso wangu mtu huyo, na jamaa zake, nami nitamkatilia mbali, na hao wote wamwandamao katika uzinifu, ili kufanya uzinifu pamoja na Moleki, watengwe mbali na watu wao.
Jérémie 3.2 Psaumes 106.39 Jérémie 32.39 Osée 2.13 Lévitique 17.7
6 Na mtu yule atakayewaendea wenye pepo, na wachawi, ili kuzini pamoja nao, nitakaza uso wangu juu ya mtu yule, nitamtenga na watu wake.
Lévitique 19.31 Lévitique 20.27 Esaïe 8.19 Nombres 15.39 Deutéronome 18.10-18.14
7 Jitakaseni basi, iweni watakatifu, kwa kuwa mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.
Ephésiens 1.4 Lévitique 11.44 1 Thessaloniciens 4.7 1 Thessaloniciens 4.3 Philippiens 2.12-2.13
8 Nanyi zishikeni sheria zangu, na kuzitenda; Mimi ndimi Bwana niwatakasaye ninyi.
Exode 31.13 Ezéchiel 37.28 Lévitique 21.8 1 Corinthiens 1.30 Apocalypse 22.14
9 Kwa maana kila mtu amlaaniye baba yake au mama yake hakika atauawa, amemlaani baba yake na mama yake; damu yake itakuwa juu yake.
Exode 21.17 Deutéronome 27.16 Marc 7.10 Matthieu 15.4 2 Samuel 1.16
10 Na mtu aziniye na mke wa mtu mwingine, naam, yeye aziniye na mke wa jirani yake, mtu mume aziniye, na mwanamke aziniye, hakika watauawa.
Lévitique 18.20 Exode 20.14 Jean 8.4-8.5 Deutéronome 5.18 2 Samuel 12.13
11 Na mtu mume atakayelala pamoja na mke wa baba yake amefunua utupu wa baba yake; wote wawili hakika watauawa; damu yao itakuwa juu yao.
Deutéronome 27.23 Deutéronome 27.20 1 Corinthiens 5.1 Lévitique 18.7-18.8 Amos 2.7
12 Na mtu mume akilala na mkwewe mwanamke wote wawili hakika watauawa; wamefanya yaliyo uchafuko; damu yao itakuwa juu yao.
Lévitique 18.15 Lévitique 18.23 Genèse 38.18 Deutéronome 27.23 Genèse 38.16
13 Tena mtu mume akilala pamoja na mtu mume, kama alalavyo na mtu mke, wote wawili wamefanya machukizo; hakika watauawa; damu yao itakuwa juu yao.
Jude 1.7 Lévitique 18.22 1 Timothée 1.10 1 Corinthiens 6.9 Deutéronome 23.17
14 Tena mtu mume akimwoa mke pamoja na mama yake, ni uovu mkuu; watachomwa moto, yeye mume na hao wanawake pia; ili kwamba usiwe uovu kati yenu.
Lévitique 18.17 Deutéronome 27.23 Lévitique 21.9 Amos 2.7 Josué 7.25
15 Tena mtu mume akilala na mnyama, hakika atauawa; nanyi mtamwua huyo mnyama.
Lévitique 18.23 Deutéronome 27.21 Exode 22.19
16 Tena mwanamke akimkaribia mnyama ye yote, na kulala pamoja naye, mtamwua huyo mwanamke, na mnyama pia; hakika watauawa; damu yao itakuwa ni juu yao.
Exode 19.13 Exode 21.32 Exode 21.28 Hébreux 12.20
17 Tena mtu mume akimwoa umbu lake, binti ya baba yake, au binti ya mama yake, na kuuona utupu wake, na huyo mwanamke kauona utupu wake huyo mume; ni jambo la aibu; watakatiliwa mbali mbele ya macho ya wana wa watu wao; amefunua utupu wa umbu lake; naye atauchukua uovu wake.
Lévitique 18.9 Deutéronome 27.22 2 Samuel 13.12 Genèse 20.12 Ezéchiel 22.11
18 Tena mtu mume akilala na mwanamke aliye na ugonjwa wake, na kufunua utupu wake; amelifunua jito la damu yake, naye mwanamke amefunua jito la damu yake; wote wawili watakatiliwa mbali na watu wao.
Lévitique 15.24 Lévitique 18.19 Ezéchiel 18.6 Ezéchiel 22.10
19 Usifunue utupu wa umbu la mama yako, wala umbu la baba yako; kwa kuwa huyo amefunua utupu wa jamaa yake ya karibu; watauchukua uovu wao.
Lévitique 18.6 Lévitique 18.12-18.30 Exode 6.20
20 Tena mtu mume akilala na mke wa mjomba wake, ameufunua utupu wa mjomba wake; watauchukua uovu wao; watakufa bila kuzaa mwana.
Lévitique 18.14 Luc 1.7 Psaumes 109.13 Luc 1.25 Job 18.19
21 Tena mtu mume akimtwaa mke wa nduguye, ni uchafu; ameufunua utupu wa nduguye; hao watakuwa hawana wana.
Lévitique 18.16 Matthieu 14.3-14.4
22 Basi zishikeni amri zangu zote, na hukumu zangu zote, na kuzifanya; ili kwamba hiyo nchi, ambayo nawapeleka ninyi kukaa, isiwatapike.
Lévitique 18.25-18.28 Ezéchiel 36.27 Psaumes 119.145 Psaumes 105.45 Esaïe 26.8-26.9
23 Nanyi msiende kwa kuziandama desturi za taifa, niitoayo mbele yenu; kwa kuwa wao waliyafanya mambo hayo yote, na kwa ajili ya hayo niliwachukia.
Lévitique 18.3 Deutéronome 9.5 Lévitique 18.30 Lévitique 18.24 Lévitique 18.27
24 Lakini mimi nimewaambia ninyi, Mtairithi nchi yao, nami nitawapa ninyi kuimiliki; nchi iliyojaa maziwa na asali; mimi ni Bwana, Mungu wenu, niliyewatenga ninyi na mataifa.
Exode 33.16 Deutéronome 14.2 Exode 3.8 1 Rois 8.53 Exode 3.17
25 Kwa ajili ya hayo mtapambanua kati ya mnyama aliye safi na mnyama aliye najisi, na kati ya ndege aliye tohara na ndege aliye najisi; nanyi msizifanye nafsi zenu kuwa machukizo kwa njia ya mnyama, au kwa njia ya ndege, au kwa njia ya kitu cho chote ambacho nchi imejaa nacho, niliowatenga nanyi kuwa ni najisi.
Deutéronome 14.3-14.21 Lévitique 11.1-11.47 Ephésiens 5.7-5.11 Actes 10.11-10.15 Actes 10.28
26 Nanyi mtakuwa watakatifu kwangu mimi; kwa kuwa mimi Bwana ni mtakatifu nami nimewatenga ninyi na mataifa, ili kwamba mwe wangu.
Lévitique 20.24 Lévitique 19.2 Lévitique 20.7 Apocalypse 4.8 1 Pierre 1.15-1.16
27 Tena mtu mume au mtu mke aliye na pepo, au aliye mchawi, hakika atauawa; watawapiga kwa mawe; damu yao itakuwa juu yao.
Lévitique 19.31 Lévitique 20.6 Exode 22.18 1 Samuel 28.7-28.9 Deutéronome 18.10-18.12

Cette Bible est dans le domaine public.