Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Lévitique 12.8
Bible en Swahili de l’est


La purification de la femme après l’accouchement

1 Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
2 Nena na hao wana wa Israeli, uwaambie, Mwanamke akitunga mimba na kuzaa mtoto mume, ndipo atakuwa yu najisi siku saba; kama katika siku za kutengwa kwake kwa ajili ya hedhi, ndivyo atakavyokuwa najisi.
Lévitique 15.19 Lévitique 18.19 Luc 2.22 Genèse 1.28 Genèse 3.16
3 Siku nane mtoto atatahiriwa govi ya zunga lake.
Luc 1.59 Luc 2.21 Jean 7.22-7.23 Genèse 17.11-17.12 Romains 3.19
4 Na huyo mwanamke atakaa katika damu ya kutakata kwake siku thelathini na tatu; asiguse kitu kilicho kitakatifu, wala asiingie mahali patakatifu, hata siku hizo za kutakata kwake zitakapotimia.
Lévitique 15.25-15.28 Aggée 2.13 Luc 2.22-2.23
5 Lakini kwamba amezaa mtoto mke ndipo atakuwa najisi juma mbili, kama katika kutengwa kwake; naye atakaa katika damu ya kutakata kwake muda wa siku sitini na sita.
Genèse 3.13 Lévitique 12.4 1 Timothée 2.14-2.15 Lévitique 12.2
6 Kisha hizo siku za kutakaswa kwake zitakapotimia, kwa ajili ya mwana, au kwa ajili ya binti, ataleta mwana-kondoo wa mwaka mmoja kuwa sadaka ya kuteketezwa na kinda la njiwa, au hua, kuwa sadaka ya dhambi, awalete mlangoni pa hema ya kukutania, na kumpa kuhani;
Luc 2.22 Nombres 6.10 Hébreux 7.26 Lévitique 15.14 Lévitique 12.2
7 na yeye atawasongeza mbele za Bwana, na kufanya upatanisho kwa ajili yake; naye atatakasika na jicho la damu yake. Hii ndiyo amri yake huyo azaaye, kwamba ni mtoto mume au mke.
Romains 3.26 Lévitique 1.4 Galates 3.28 1 Corinthiens 7.14 Lévitique 15.28-15.30
8 Kama mali yake huyo mwanamke haimfikilii mwana-kondoo, hapo ndipo atakapochukua hua wawili, au makinda mawili ya njiwa; mmoja kuwa sadaka ya kuteketezwa, na wa pili kuwa sadaka ya dhambi; naye kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake, naye atakuwa safi.
Lévitique 5.7 Lévitique 4.26 Lévitique 1.14 Lévitique 14.22 Lévitique 15.14

Cette Bible est dans le domaine public.