Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Lévitique 10.1
Bible en Swahili de l’est


Faute et mort de Nadab et Abihu

1 Na Nadabu na Abihu, wana wa Haruni, wakatwaa kila mtu chetezo chake, wakatia moto ndani yake, wakatia na uvumba, nao wakatoa moto wa kigeni mbele ya Bwana, ambao yeye hakuwaagiza.
Nombres 26.61 Lévitique 16.12 Exode 24.1 Nombres 16.46 Exode 28.1
2 Kisha moto ukatoka hapo mbele za Bwana, nao ukawala, nao wakafa mbele za Bwana.
Nombres 26.61 Lévitique 9.24 Nombres 16.35 Nombres 3.3-3.4 2 Samuel 6.7
3 Ndipo Musa akamwambia Haruni, Jambo hili ni hilo Bwana alilolinena, akisema, Nitatakaswa mimi katika hao wanikaribiao, nami nitatukuzwa mbele ya watu hao wote. Haruni akanyamaza kimya.
Lévitique 21.6 Ezéchiel 28.22 Esaïe 49.3 Exode 19.22 Psaumes 39.9
4 Musa akawaita Mishaeli na Elisafani, wana wa Uzieli mjombaye Haruni, na kuwaambia, Njoni karibu, mwachukue hawa ndugu zenu, mkawaondoe hapa mbele ya maskani, mwende nao nje ya marago.
Exode 6.22 Exode 6.18 Nombres 3.30 Actes 5.6 Nombres 3.19
5 Basi wakaja karibu, na kuwachukua, hali wamevaa nguo zao, wakawachukua nje ya marago; kama Musa alivyosema.
Lévitique 8.13
6 Kisha Musa akamwambia Haruni na wanawe Eleazari na Ithamari, Msiache wazi nywele za vichwani mwenu, wala msiyararue mavao yenu; ili kwamba msife, tena asiukasirikie mkutano wote; lakini ndugu zenu, nyumba yote ya Israeli, na waomboleze kwa ajili ya hicho kichomo alichowasha Bwana.
Josué 22.18 Josué 7.1 Nombres 16.22 Josué 22.20 Lévitique 13.45
7 Wala hamtatoka nje mlangoni mwa hema ya kukutania, msije mkafa; kwa sababu mafuta ya kutiwa ya Bwana ya juu yenu. Nao wakafanya kama hilo neno la Musa.
Lévitique 21.12 Exode 28.41 Lévitique 8.30 Exode 30.30 2 Corinthiens 1.21
8 Kisha Bwana akanena na Haruni, na kumwambia,
9 Usinywe divai wala kileo cho chote, wewe, wala wanao pamoja nawe, hapo mwingiapo ndani ya hema ya kukutania, ili kwamba msife; amri hii itakuwa ni amri ya milele katika vizazi vyenu;
1 Timothée 3.3 Luc 1.15 Ezéchiel 44.21 Tite 1.7 Ephésiens 5.18
10 kisha, mpate kupambanua kati ya yaliyo matakatifu na hayo yaliyo ya siku zote, na kati ya yaliyo najisi na hayo yaliyo safi;
Ezéchiel 22.26 Lévitique 11.47 1 Pierre 1.14-1.16 Ezéchiel 44.23 Lévitique 20.25-20.26
11 tena mpate kuwafundisha wana wa Israeli amri hizi zote ambazo Bwana amewaambia kwa mkono wa Musa.
Malachie 2.7 Deutéronome 24.8 Jérémie 18.18 Néhémie 8.8 Deutéronome 33.10
12 Kisha Musa akanena na Haruni, na Eleazari, na Ithamari, hao wanawe waliobaki, Twaeni hiyo sadaka ya unga iliyosalia katika kafara za Bwana zilizotolewa kwa moto, mkaile pasipo kutiwa chachu, pale karibu na madhabahu; kwa kuwa ni takatifu sana;
Lévitique 21.22 Nombres 18.9-18.10 Lévitique 2.1-2.16 Lévitique 7.9 Ezéchiel 44.29
13 nanyi mtaila katika mahali patakatifu, kwa sababu ni haki yako, na haki ya wanao, katika hizo kafara zisongezwazo kwa Bwana kwa moto; kwani ni hivyo nilivyoagizwa.
Lévitique 2.3 Lévitique 6.16 Nombres 18.10
14 Na kidari cha kutikiswa, na mguu wa kuinuliwa, mtavila katika mahali palipo safi; wewe, na wanao, na binti zako pamoja nawe; kwa maana vimetolewa kuwa ni haki yako, na haki ya wanao, katika zile kafara za sadaka za amani za wana wa Israeli.
Nombres 18.11 Lévitique 9.21 Jean 4.34 Lévitique 7.29-7.34 Exode 29.24-29.28
15 Mguu wa kuinuliwa, na kidari cha kutikiswa, Watavileta pamoja na dhabihu zisongezwazo kwa njia ya moto, za hayo mafuta ili kuvitikisa viwe sadaka ya kutikiswa mbele za Bwana; kisha vitakuwa ni vyako wewe, na vya wanao pamoja nawe, ni haki yenu milele, kama Bwana alivyoagiza.
Lévitique 7.34 Genèse 17.17 Genèse 17.8 Lévitique 7.29-7.30 1 Corinthiens 9.13-9.14
16 Kisha Musa akamtafuta sana huyo mbuzi wa sadaka ya dhambi, naye, tazama, alikuwa amekwisha kuchomwa moto; naye akawakasirikia hao Eleazari na Ithamari, wana wa Haruni, hao waliobaki, akawaambia,
Lévitique 9.3 Lévitique 9.15 Ephésiens 4.26 Marc 3.5 Nombres 12.3
17 Kwa nini hamkula hiyo sadaka ya dhambi katika mahali patakatifu, kwa kuwa ni takatifu sana, naye amewapa ninyi ili kuuchukua uovu wa mkutano, na kuwafanyia upatanisho mbele za Bwana?
Exode 28.38 Nombres 18.1 Ezéchiel 18.19-18.20 Lévitique 7.6-7.7 Jean 1.29
18 Angalieni, hiyo damu yake haikuletwa ndani ya mahali patakatifu; iliwapasa kuila ndani ya mahali patakatifu, kama nilivyowaagiza.
Lévitique 6.30 Lévitique 6.26
19 Haruni akamwambia Musa, Angalia, hivi leo wamesongeza sadaka yao ya dhambi, na sadaka yao ya kuteketezwa, mbele za Bwana; kisha mambo kama haya yamenipata; tena kama ningalikula hiyo sadaka ya dhambi hivi leo, je! Lingekuwa ni jambo la kupendeza mbele za macho ya Bwana?
Lévitique 9.12 Lévitique 9.8 Malachie 1.13 Osée 9.4 Jérémie 6.20
20 Naye Musa aliposikia hayo, yakampendeza.
Matthieu 12.20 Zacharie 7.8-7.9 2 Chroniques 30.18-30.20 Matthieu 12.3-12.7

Cette Bible est dans le domaine public.