Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Osée 7.8
Bible en Swahili de l’est


Reproches contre les alliances politiques

1 Wakati nitakapo kumponya Israeli, ndipo yafunuliwapo maovu ya Efraimu, na ubaya wa Samaria; maana wanatenda uongo, na mwivi huvunja nyumba za watu, na kundi la wanyang’anyi hushambulia nje.
Osée 4.2 Osée 6.4 Osée 8.9 Osée 5.1 Osée 10.5
2 Wala hawafikiri mioyoni mwao ya kwamba naukumbuka uovu wao wote; sasa matendo yao wenyewe yamewazunguka pande zote; yako mbele za uso wangu.
Psaumes 90.8 Jérémie 2.19 Jérémie 14.10 1 Corinthiens 4.5 Osée 9.9
3 Humfurahisha mfalme kwa uovu wao, na wakuu wao kwa uongo wao.
Michée 7.3 Romains 1.32 Jérémie 28.1-28.4 Osée 7.5 Amos 7.10-7.13
4 Hao wote ni wazinzi; wamekuwa kama tanuu iliyotiwa moto na mwokaji; huacha kuuchochea moto, tangu kuukanda unga hata umekwisha kutiwa chachu.
Jérémie 9.2 Jacques 4.4 Jérémie 5.7-5.8 Osée 7.6-7.7 Osée 4.2
5 Sikukuu ya mfalme wetu, wakuu walijitapisha kwa ukali wa divai; alinyosha mkono wake pamoja na wenye mzaha.
Esaïe 28.1 Marc 6.21 Habakuk 2.15-2.16 Daniel 5.23 Daniel 5.1-5.4
6 Maana wamefanya moyo wao kuwa tayari kama tanuu, wakati waoteapo; hasira yao hulala usiku kucha; asubuhi yawaka kama moto utoao miali.
Michée 2.1 1 Samuel 19.11-19.15 Psaumes 21.9 Psaumes 10.8-10.9 Proverbes 4.16
7 Wote wamepata moto kama tanuu, nao hula makadhi wao; wafalme wao wote wameanguka; hakuna hata mmoja wao aniitaye mimi.
2 Rois 15.25 2 Rois 15.10 2 Rois 15.30 2 Rois 15.14 Esaïe 43.22
8 Efraimu ajichanganya na mataifa; Efraimu ni mkate usiogeuzwa.
Psaumes 106.35 Osée 5.13 Apocalypse 3.15-3.16 Esdras 9.1 Osée 8.2-8.4
9 Wageni wamekula nguvu zake, naye hana habari; naam, nywele za mvi zimeonekana huko na huko juu yake, naye hana habari.
Osée 8.7 2 Rois 15.19 2 Rois 13.3-13.7 Proverbes 23.35 Esaïe 57.1
10 Na kiburi cha Israeli chamshuhudia mbele ya uso wake; ila hata hivyo hawakumrudia Bwana, Mungu wao, wala hawakumtafuta kwa ajili ya hayo yote.
Osée 5.5 Esaïe 9.13 Amos 4.6-4.13 Jérémie 3.3 Osée 6.1
11 Naye Efraimu amekuwa kama njiwa mpumbavu, asiye na fahamu; humwita Misri, huenda Ashuru.
Osée 12.1 Osée 5.13 Osée 11.11 Osée 4.11 Osée 9.3
12 Watakapokwenda nitatandika wavu wangu juu yao; nitawashusha kama ndege wa angani; nitawarudi, kama vile mkutano wao ulivyosikia.
Ezéchiel 12.13 Deutéronome 28.15-28.68 Jérémie 44.4 Deutéronome 32.15-32.43 Ezéchiel 17.20
13 Ole wao! Kwa kuwa wamenikimbia; uharibifu na uwapate! Kwa kuwa wameniasi; ingawa ninataka kuwakomboa, hata hivyo wamenena uongo juu yangu.
Osée 9.12 Osée 11.12 Jérémie 44.17-44.18 Esaïe 63.8 Matthieu 23.13-23.29
14 Wala hawakunililia kwa moyo, lakini wanalalamika vitandani mwao; hujikutanisha ili kupata nafaka na divai; huniasi mimi.
Amos 2.8 Zacharie 7.5 Juges 9.27 Jérémie 3.10 Job 35.9-35.10
15 Ingawa nimewafundisha na kuwatia nguvu mikono yao, hata hivyo hukusudia udhalimu juu yangu.
Nahum 1.9 2 Corinthiens 10.5 Actes 4.25 Proverbes 3.11 Apocalypse 3.19
16 Wao hurudi, lakini si kwake Aliye juu; wamekuwa kama upinde usiotumainika; wakuu wao wataanguka kwa upanga, kwa sababu ya jeuri ya ndimi zao; jambo hili litakuwa kwao sababu ya kuchekwa katika nchi ya Misri.
Psaumes 78.57 Osée 9.3 Psaumes 73.9 Ezéchiel 23.32 Psaumes 12.4

Cette Bible est dans le domaine public.