Reproches contre les alliances politiques
 1 Wakati nitakapo kumponya Israeli, ndipo yafunuliwapo maovu ya Efraimu, na ubaya wa Samaria; maana wanatenda uongo, na mwivi huvunja nyumba za watu, na kundi la wanyang’anyi hushambulia nje.
Osée 6.4  Osée 4.2  Osée 8.5  Amos 8.14  Esaïe 28.1  
 2 Wala hawafikiri mioyoni mwao ya kwamba naukumbuka uovu wao wote; sasa matendo yao wenyewe yamewazunguka pande zote; yako mbele za uso wangu.
Jérémie 2.19  Jérémie 14.10  Psaumes 90.8  Psaumes 9.16  Hébreux 4.13  
 3 Humfurahisha mfalme kwa uovu wao, na wakuu wao kwa uongo wao.
Romains 1.32  Michée 7.3  Jérémie 28.1-28.4  Jérémie 9.2  Jérémie 37.19  
 4 Hao wote ni wazinzi; wamekuwa kama tanuu iliyotiwa moto na mwokaji; huacha kuuchochea moto, tangu kuukanda unga hata umekwisha kutiwa chachu.
Jérémie 9.2  Osée 4.12  Jacques 4.4  Jérémie 5.7-5.8  Osée 7.6-7.7  
 5 Sikukuu ya mfalme wetu, wakuu walijitapisha kwa ukali wa divai; alinyosha mkono wake pamoja na wenye mzaha.
Esaïe 28.1  Esaïe 5.11-5.12  Proverbes 13.20  Psaumes 1.1  1 Rois 13.4  
 6 Maana wamefanya moyo wao kuwa tayari kama tanuu, wakati waoteapo; hasira yao hulala usiku kucha; asubuhi yawaka kama moto utoao miali.
Osée 7.4  2 Samuel 13.28-13.29  Osée 7.7  Michée 2.1  1 Samuel 19.11-19.15  
 7 Wote wamepata moto kama tanuu, nao hula makadhi wao; wafalme wao wote wameanguka; hakuna hata mmoja wao aniitaye mimi.
2 Rois 15.14  2 Rois 15.25  2 Rois 15.10  2 Rois 15.30  Esaïe 64.7  
 8 Efraimu ajichanganya na mataifa; Efraimu ni mkate usiogeuzwa.
Psaumes 106.35  Osée 5.13  1 Rois 18.21  Malachie 2.11  Osée 9.3  
 9 Wageni wamekula nguvu zake, naye hana habari; naam, nywele za mvi zimeonekana huko na huko juu yake, naye hana habari.
Osée 8.7  Esaïe 42.22-42.25  Esaïe 1.7  2 Rois 13.22  2 Rois 15.19  
 10 Na kiburi cha Israeli chamshuhudia mbele ya uso wake; ila hata hivyo hawakumrudia Bwana, Mungu wao, wala hawakumtafuta kwa ajili ya hayo yote.
Osée 5.5  Esaïe 9.13  Amos 4.6-4.13  Jérémie 8.5-8.6  Zacharie 1.4  
 11 Naye Efraimu amekuwa kama njiwa mpumbavu, asiye na fahamu; humwita Misri, huenda Ashuru.
Osée 5.13  Osée 12.1  Osée 4.11  Osée 11.11  Osée 9.3  
 12 Watakapokwenda nitatandika wavu wangu juu yao; nitawashusha kama ndege wa angani; nitawarudi, kama vile mkutano wao ulivyosikia.
Ezéchiel 12.13  Deutéronome 28.15-28.68  Deutéronome 31.16-31.29  Deutéronome 29.22-29.28  Ecclésiaste 9.12  
 13 Ole wao! Kwa kuwa wamenikimbia; uharibifu na uwapate! Kwa kuwa wameniasi; ingawa ninataka kuwakomboa, hata hivyo wamenena uongo juu yangu.
Osée 9.12  Osée 11.12  Michée 6.4  Psaumes 139.7-139.9  Esaïe 41.14  
 14 Wala hawakunililia kwa moyo, lakini wanalalamika vitandani mwao; hujikutanisha ili kupata nafaka na divai; huniasi mimi.
Amos 2.8  Job 35.9-35.10  Michée 2.11  Zacharie 7.5  Juges 9.27  
 15 Ingawa nimewafundisha na kuwatia nguvu mikono yao, hata hivyo hukusudia udhalimu juu yangu.
Nahum 1.9  Romains 1.21  Psaumes 62.3  Psaumes 106.43-106.45  2 Rois 13.5  
 16 Wao hurudi, lakini si kwake Aliye juu; wamekuwa kama upinde usiotumainika; wakuu wao wataanguka kwa upanga, kwa sababu ya jeuri ya ndimi zao; jambo hili litakuwa kwao sababu ya kuchekwa katika nchi ya Misri.Psaumes 78.57  Osée 9.3  Psaumes 73.9  Ezéchiel 23.32  Psaumes 12.4