Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Osée 6.8
Bible en Swahili de l’est


1 Njoni, tumrudie Bwana; maana yeye amerarua, na yeye atatuponya; yeye amepiga, na yeye atatufunga jeraha zetu.
Deutéronome 32.39 1 Samuel 2.6 Job 5.18 Job 34.29 Osée 14.4
2 Baada ya siku mbili atatufufua; siku ya tatu atatuinua, nasi tutaishi mbele zake.
Ezéchiel 37.11-37.13 Psaumes 30.4-30.5 1 Corinthiens 15.4 Esaïe 26.19 Jean 14.19
3 Nasi na tujue, naam, tukaendelee kumjua Bwana; kutokea kwake ni yakini kama asubuhi; naye atatujilia kama mvua, kama mvua ya vuli iinyweshayo nchi.
Psaumes 72.6 Proverbes 2.1-2.5 Actes 17.11 Philippiens 3.13-3.15 Michée 4.2
4 Ee Efraimu, nikutendee nini? Ee Yuda, nikutendee nini? Kwa maana fadhili zenu ni kama wingu la asubuhi na kama umande utowekao mapema.
Osée 11.8 Osée 13.3 Psaumes 78.34-78.37 Luc 19.41-19.42 Jérémie 3.19
5 Kwa sababu hiyo nimewakata-kata kwa vinywa vya manabii; nimewaua kwa maneno ya kinywa changu; na hukumu yangu itatokea kama mwanga.
Jérémie 23.29 Jérémie 1.10 Jérémie 5.14 Hébreux 4.12 Ezéchiel 43.3
6 Maana nataka fadhili wala si sadaka; na kumjua Mungu kuliko sadaka za kuteketezwa.
Matthieu 12.7 Matthieu 9.13 Esaïe 1.11 1 Samuel 15.22 1 Jean 3.6
7 Lakini wao wamelivunja hilo agano kama Adamu; huko wamenitenda mambo ya hiana.
Osée 5.7 Osée 8.1 Genèse 3.11 Job 31.33 Esaïe 48.8
8 Gileadi ni mji wa hao watendao maovu, umetiwa rangi ya damu.
Osée 12.11 Psaumes 10.8 Josué 21.38 2 Samuel 3.27 Actes 23.12-23.15
9 Na kama vile makundi ya wanyang’anyi wamwoteavyo mtu, ndivyo kundi la makuhani wauavyo katika njia ielekeayo Shekemu; naam, wametenda mambo maovu sana.
Osée 7.1 Osée 5.1 Sophonie 3.3 Jean 11.47 1 Rois 12.25
10 Katika nyumba ya Israeli nimeona jambo bovu kabisa; huko uzinzi umeonekana katika Efraimu; Israeli ametiwa unajisi.
Osée 5.3 Jérémie 5.30-5.31 Jérémie 23.14 1 Rois 15.30 2 Rois 17.7
11 Tena, Ee Yuda, wewe umeandikiwa mavuno, hapo nitakapowarudisha wafungwa wa watu wangu.
Joël 3.13 Jérémie 51.33 Sophonie 2.7 Psaumes 126.1 Job 42.10

Cette Bible est dans le domaine public.