1 Njoni, tumrudie Bwana; maana yeye amerarua, na yeye atatuponya; yeye amepiga, na yeye atatufunga jeraha zetu.
Deutéronome 32.39  1 Samuel 2.6  Job 5.18  Esaïe 2.3  Job 34.29  
 2 Baada ya siku mbili atatufufua; siku ya tatu atatuinua, nasi tutaishi mbele zake.
Ezéchiel 37.11-37.13  1 Corinthiens 15.4  Esaïe 26.19  Jean 14.19  2 Rois 20.5  
 3 Nasi na tujue, naam, tukaendelee kumjua Bwana; kutokea kwake ni yakini kama asubuhi; naye atatujilia kama mvua, kama mvua ya vuli iinyweshayo nchi.
Proverbes 2.1-2.5  Psaumes 72.6  Philippiens 3.13-3.15  Actes 17.11  Michée 4.2  
 4 Ee Efraimu, nikutendee nini? Ee Yuda, nikutendee nini? Kwa maana fadhili zenu ni kama wingu la asubuhi na kama umande utowekao mapema.
Osée 13.3  Osée 11.8  Psaumes 78.34-78.37  Jérémie 9.7  Psaumes 106.12-106.13  
 5 Kwa sababu hiyo nimewakata-kata kwa vinywa vya manabii; nimewaua kwa maneno ya kinywa changu; na hukumu yangu itatokea kama mwanga.
Jérémie 23.29  Jérémie 1.10  Jérémie 5.14  Hébreux 4.12  2 Rois 1.16  
 6 Maana nataka fadhili wala si sadaka; na kumjua Mungu kuliko sadaka za kuteketezwa.
Matthieu 9.13  Matthieu 12.7  Esaïe 1.11  1 Samuel 15.22  1 Jean 3.6  
 7 Lakini wao wamelivunja hilo agano kama Adamu; huko wamenitenda mambo ya hiana.
Osée 8.1  Osée 5.7  Genèse 3.11  Job 31.33  Jérémie 5.11  
 8 Gileadi ni mji wa hao watendao maovu, umetiwa rangi ya damu.Osée 12.11  Esaïe 59.6  Michée 7.2  2 Samuel 20.8  Actes 25.3  
 9 Na kama vile makundi ya wanyang’anyi wamwoteavyo mtu, ndivyo kundi la makuhani wauavyo katika njia ielekeayo Shekemu; naam, wametenda mambo maovu sana.
Osée 7.1  Osée 5.1  Ezéchiel 22.27  Proverbes 1.11-1.19  Job 1.15-1.17  
 10 Katika nyumba ya Israeli nimeona jambo bovu kabisa; huko uzinzi umeonekana katika Efraimu; Israeli ametiwa unajisi.
Osée 5.3  Jérémie 5.30-5.31  Jérémie 23.14  1 Rois 15.30  2 Rois 17.7  
 11 Tena, Ee Yuda, wewe umeandikiwa mavuno, hapo nitakapowarudisha wafungwa wa watu wangu.
Joël 3.13  Jérémie 51.33  Sophonie 2.7  Psaumes 126.1  Job 42.10