Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Osée 6.4
Bible en Swahili de l’est


1 Njoni, tumrudie Bwana; maana yeye amerarua, na yeye atatuponya; yeye amepiga, na yeye atatufunga jeraha zetu.
Deutéronome 32.39 1 Samuel 2.6 Job 5.18 Job 34.29 Osée 14.4
2 Baada ya siku mbili atatufufua; siku ya tatu atatuinua, nasi tutaishi mbele zake.
Ezéchiel 37.11-37.13 Psaumes 30.4-30.5 1 Corinthiens 15.4 Esaïe 26.19 Jean 14.19
3 Nasi na tujue, naam, tukaendelee kumjua Bwana; kutokea kwake ni yakini kama asubuhi; naye atatujilia kama mvua, kama mvua ya vuli iinyweshayo nchi.
Psaumes 72.6 Proverbes 2.1-2.5 Actes 17.11 Philippiens 3.13-3.15 Michée 4.2
4 Ee Efraimu, nikutendee nini? Ee Yuda, nikutendee nini? Kwa maana fadhili zenu ni kama wingu la asubuhi na kama umande utowekao mapema.
Osée 11.8 Osée 13.3 Psaumes 78.34-78.37 Jérémie 5.23 Juges 2.18-2.19
5 Kwa sababu hiyo nimewakata-kata kwa vinywa vya manabii; nimewaua kwa maneno ya kinywa changu; na hukumu yangu itatokea kama mwanga.
Jérémie 23.29 Jérémie 1.10 Jérémie 5.14 Hébreux 4.12 Apocalypse 2.16
6 Maana nataka fadhili wala si sadaka; na kumjua Mungu kuliko sadaka za kuteketezwa.
Matthieu 12.7 Matthieu 9.13 Esaïe 1.11 1 Samuel 15.22 1 Jean 3.6
7 Lakini wao wamelivunja hilo agano kama Adamu; huko wamenitenda mambo ya hiana.
Osée 8.1 Osée 5.7 Job 31.33 Genèse 3.11 Esaïe 48.8
8 Gileadi ni mji wa hao watendao maovu, umetiwa rangi ya damu.
Osée 12.11 Psaumes 59.2 Jérémie 11.19 Psaumes 10.8 Josué 21.38
9 Na kama vile makundi ya wanyang’anyi wamwoteavyo mtu, ndivyo kundi la makuhani wauavyo katika njia ielekeayo Shekemu; naam, wametenda mambo maovu sana.
Osée 7.1 Osée 5.1 Michée 3.9 Sophonie 3.3 Jean 11.47
10 Katika nyumba ya Israeli nimeona jambo bovu kabisa; huko uzinzi umeonekana katika Efraimu; Israeli ametiwa unajisi.
Osée 5.3 Jérémie 5.30-5.31 Jérémie 23.14 Ezéchiel 23.5 Jérémie 2.12-2.13
11 Tena, Ee Yuda, wewe umeandikiwa mavuno, hapo nitakapowarudisha wafungwa wa watu wangu.
Joël 3.13 Jérémie 51.33 Sophonie 2.7 Psaumes 126.1 Job 42.10

Cette Bible est dans le domaine public.