Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Osée 10.6
Bible en Swahili de l’est


1 Israeli ni mzabibu, utoao matunda yake; kwa kadiri ya wingi wa matunda yake, kwa kadiri iyo hiyo ameongeza madhabahu zake; kwa kadiri ya wema wa nchi yake, kwa kadiri iyo hiyo wamefanya nguzo nzuri.
Osée 8.11 Esaïe 5.1-5.7 Osée 12.11 Jérémie 2.28 Lévitique 26.1
2 Moyo wao umegawanyika; sasa wataonekana kuwa na hatia; yeye atazipiga madhabahu zao, ataziharibu nguzo zao.
1 Rois 18.21 Michée 5.13 Sophonie 1.5 1 Samuel 5.4 Osée 8.5-8.6
3 Yakini sasa watasema, Hatuna mfalme; kwa maana hatumchi Bwana; na mfalme huyu je! Aweza kututendea nini?
Osée 10.15 Osée 10.7 Osée 13.11 Jean 19.15 Genèse 49.10
4 Hunena maneno yasiyo na maana; huapa kwa uongo wafanyapo maagano; basi ndipo hukumu huchipuka kama mbaruti katika matuta ya shamba.
Amos 5.7 Osée 4.2 Amos 6.12 2 Rois 17.3-17.4 Ezéchiel 17.13-17.19
5 Wakaao Samaria wataona hofu kwa ajili ya ndama za Beth-Aveni; kwa maana watu wa mji huo wataulilia, na makuhani wake walioufurahia, kwa sababu ya utukufu wake; kwa maana umetoweka.
Osée 8.5-8.6 Osée 9.11 Osée 4.15 Osée 5.8 2 Rois 23.5
6 Nayo itachukuliwa Ashuru, iwe zawadi kwa mfalme Yarebu; Efraimu atapata aibu, na Israeli atalionea haya shauri lake mwenyewe.
Osée 5.13 Esaïe 30.3 Jérémie 7.24 Daniel 11.8 Jérémie 3.24-3.25
7 Katika habari za Samaria, mfalme wake amekatiliwa mbali, kama povu usoni pa maji.
Osée 10.3 2 Rois 15.30 1 Rois 21.1 Osée 13.11 Jude 1.13
8 Mahali pa Aveni palipoinuka, yaani, dhambi ya Israeli, pataharibika; mwiba na mbigili itamea juu ya madhabahu zake; nao wataiambia milima, Tusitirini; na vilima, Tuangukieni.
Apocalypse 6.16 Luc 23.30 Osée 9.6 Esaïe 32.13 Esaïe 2.19
9 Ee Israeli, umefanya dhambi tangu siku za Gibea; huko ndiko walikosimama; ili vita vilivyokuwa juu ya wana wa uovu visiwapate katika Gibea.
Osée 9.9 Sophonie 3.6-3.7 Genèse 8.21 Juges 20.17-20.48 Juges 19.22-19.30
10 Wakati nitakapopenda nitawaadhibu; na hao mataifa watakusanyika juu yao, watakapofungwa kwa sababu ya makosa yao mawili.
Ezéchiel 5.13 Jérémie 16.16 Zacharie 14.2-14.3 Osée 8.10 Matthieu 22.7
11 Naye Efraimu ni ndama aliyefundishwa, apendaye kupura; lakini nimepitisha kongwa juu ya shingo yake nzuri; nitampandisha mwenye kupanda juu ya Efraimu; Yuda atalima, na Yakobo atavunja madongoa yake.
Osée 4.16 Jérémie 50.11 Deutéronome 25.4 Esaïe 28.24 Osée 11.4
12 Jipandieni katika haki, vuneni kwa fadhili; uchimbueni udongo wa mashamba yenu, kwa maana wakati umewadia wa kumtafuta Bwana, hata atakapokuja na kuwanyeshea haki.
Jérémie 4.3-4.4 Osée 6.3 Proverbes 11.18 Esaïe 45.8 Jacques 3.18
13 Mmelima dhuluma, mmevuna uovu; mmekula matunda ya uongo; kwa maana uliitumainia njia yako, na wingi wa mashujaa wako.
Job 4.8 Psaumes 33.16 Galates 6.7-6.8 Proverbes 22.8 Osée 8.7
14 Kwa sababu hiyo fitina itatokea kati ya watu wako, na ngome zako zote zitaharibiwa, kama vile Shalmani alivyoharibu Betharbeli, katika siku ya vita; mama akavunjika-vunjika pamoja na watoto wake.
Osée 13.16 Esaïe 22.1-22.4 2 Rois 19.11-19.13 Esaïe 33.14 Jérémie 13.14
15 Hivyo ndivyo Betheli atakavyowatenda ninyi, kwa sababu ya ubaya wenu mwingi; wakati wa mapambazuko mfalme wa Israeli atakatiliwa mbali kabisa.
Osée 10.5 Osée 10.7 Romains 7.13 Amos 7.9-7.17 Osée 10.3

Cette Bible est dans le domaine public.