Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Osée 10.13
Bible en Swahili de l’est


1 Israeli ni mzabibu, utoao matunda yake; kwa kadiri ya wingi wa matunda yake, kwa kadiri iyo hiyo ameongeza madhabahu zake; kwa kadiri ya wema wa nchi yake, kwa kadiri iyo hiyo wamefanya nguzo nzuri.
Osée 8.11 Esaïe 5.1-5.7 Osée 12.11 Lévitique 26.1 1 Rois 14.23
2 Moyo wao umegawanyika; sasa wataonekana kuwa na hatia; yeye atazipiga madhabahu zao, ataziharibu nguzo zao.
Michée 5.13 1 Rois 18.21 Sophonie 1.5 Jacques 4.4 Osée 10.5-10.8
3 Yakini sasa watasema, Hatuna mfalme; kwa maana hatumchi Bwana; na mfalme huyu je! Aweza kututendea nini?
Osée 10.15 Osée 10.7 Osée 13.11 Osée 11.5 Jean 19.15
4 Hunena maneno yasiyo na maana; huapa kwa uongo wafanyapo maagano; basi ndipo hukumu huchipuka kama mbaruti katika matuta ya shamba.
Amos 6.12 Amos 5.7 Osée 4.2 Ezéchiel 17.13-17.19 2 Rois 17.3-17.4
5 Wakaao Samaria wataona hofu kwa ajili ya ndama za Beth-Aveni; kwa maana watu wa mji huo wataulilia, na makuhani wake walioufurahia, kwa sababu ya utukufu wake; kwa maana umetoweka.
Osée 9.11 Osée 8.5-8.6 2 Rois 23.5 Osée 4.15 Osée 5.8
6 Nayo itachukuliwa Ashuru, iwe zawadi kwa mfalme Yarebu; Efraimu atapata aibu, na Israeli atalionea haya shauri lake mwenyewe.
Osée 5.13 Esaïe 30.3 Jérémie 7.24 Daniel 11.8 Jérémie 2.26-2.27
7 Katika habari za Samaria, mfalme wake amekatiliwa mbali, kama povu usoni pa maji.
Osée 10.3 2 Rois 17.4 2 Rois 1.3 Osée 10.15 2 Rois 15.30
8 Mahali pa Aveni palipoinuka, yaani, dhambi ya Israeli, pataharibika; mwiba na mbigili itamea juu ya madhabahu zake; nao wataiambia milima, Tusitirini; na vilima, Tuangukieni.
Luc 23.30 Apocalypse 6.16 Osée 9.6 Esaïe 2.19 1 Rois 12.28-12.30
9 Ee Israeli, umefanya dhambi tangu siku za Gibea; huko ndiko walikosimama; ili vita vilivyokuwa juu ya wana wa uovu visiwapate katika Gibea.
Osée 9.9 Juges 20.5 Genèse 6.5 Juges 20.13-20.14 Sophonie 3.6-3.7
10 Wakati nitakapopenda nitawaadhibu; na hao mataifa watakusanyika juu yao, watakapofungwa kwa sababu ya makosa yao mawili.
Ezéchiel 5.13 Jérémie 16.16 Osée 8.1 Jérémie 15.6 Ezéchiel 16.42
11 Naye Efraimu ni ndama aliyefundishwa, apendaye kupura; lakini nimepitisha kongwa juu ya shingo yake nzuri; nitampandisha mwenye kupanda juu ya Efraimu; Yuda atalima, na Yakobo atavunja madongoa yake.
Osée 4.16 Deutéronome 25.4 Jérémie 50.11 Romains 16.18 2 Chroniques 28.5-28.8
12 Jipandieni katika haki, vuneni kwa fadhili; uchimbueni udongo wa mashamba yenu, kwa maana wakati umewadia wa kumtafuta Bwana, hata atakapokuja na kuwanyeshea haki.
Jérémie 4.3-4.4 Proverbes 11.18 Osée 6.3 Jacques 3.18 Esaïe 45.8
13 Mmelima dhuluma, mmevuna uovu; mmekula matunda ya uongo; kwa maana uliitumainia njia yako, na wingi wa mashujaa wako.
Job 4.8 Galates 6.7-6.8 Psaumes 33.16 Osée 8.7 Proverbes 22.8
14 Kwa sababu hiyo fitina itatokea kati ya watu wako, na ngome zako zote zitaharibiwa, kama vile Shalmani alivyoharibu Betharbeli, katika siku ya vita; mama akavunjika-vunjika pamoja na watoto wake.
Osée 13.16 Amos 9.5 2 Rois 18.9-18.10 Habakuk 1.10 Esaïe 13.16-13.18
15 Hivyo ndivyo Betheli atakavyowatenda ninyi, kwa sababu ya ubaya wenu mwingi; wakati wa mapambazuko mfalme wa Israeli atakatiliwa mbali kabisa.
Osée 10.5 Osée 10.7 Amos 7.9-7.17 Osée 10.3 Esaïe 16.14

Cette Bible est dans le domaine public.