Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Osée 1.10
Bible en Swahili de l’est


Les mariages d’Osée

Osée et la femme prostituée

1 Hili ndilo neno la Bwana lililomjia Hosea, mwana wa Beeri, siku za Uzia, na Yothamu, na Ahazi, na Hezekia, wafalme wa Yuda; na siku za Yeroboamu, mwana wa Yoashi, mfalme wa Israeli.
Michée 1.1 Esaïe 1.1 Amos 1.1 Romains 9.25 2 Rois 15.32
2 Hapo kwanza Bwana aliponena kwa kinywa cha Hosea, Bwana alimwambia Hosea, Enenda ukatwae mke wa uzinzi, na watoto wa uzinzi; kwa maana nchi hii inafanya uzinzi mwingi, kwa kumwacha Bwana.
Osée 3.1 Deutéronome 31.16 Osée 2.4-2.5 Apocalypse 17.1-17.2 Ezéchiel 6.9
3 Basi akaenda akamwoa Gomeri, binti Diblaimu; naye akachukua mimba, akamzalia mtoto mwanamume.
Esaïe 8.1-8.3
4 Bwana akamwambia, Mwite jina lake Yezreeli; kwa maana bado kitambo kidogo, nitaipatiliza nyumba ya Yehu damu ya Yezreeli, na kuukomesha ufalme wa nyumba ya Israeli.
2 Rois 10.7-10.8 Matthieu 1.21 2 Rois 10.10-10.11 Ezéchiel 23.10 Jérémie 23.2
5 Tena itakuwa siku ile, nitauvunja upinde wa Israeli katika bonde la Yezreeli.
Juges 6.33 Josué 17.16 Psaumes 37.15 Osée 2.18 Psaumes 46.9
6 Akachukua mimba tena, akazaa mtoto mwanamke. Bwana akamwambia, Mwite jina lake Lo-ruhama kwa maana sitairehemu nyumba ya Israeli tena,nisije nikawasamehe kwa njia yoyote.
1 Pierre 2.10 Osée 2.23 2 Rois 17.6 Osée 2.4 Esaïe 27.11
7 Lakini nitairehemu nyumba ya Yuda; nitawaokoa kwa Bwana, Mungu wao; wala sitawaokoa kwa upinde, wala kwa upanga, wala kwa silaha, wala kwa farasi, wala kwa wapanda farasi.
Zacharie 4.6 2 Rois 19.35 Osée 11.12 Zacharie 9.9-9.10 Psaumes 44.3-44.6
8 Basi, akiisha kumwachisha Lo-ruhama, akachukua mimba, akazaa mtoto mwanamume.
9 Bwana akasema, Mwite jina lake Lo-ami kwa maana ninyi si watu wangu,wala mimi sitakuwa MUNGU wenu.
Jérémie 15.1
10 Tena itakuwa ya kwamba hesabu ya wana wa Israeli itafanana na mchanga wa bahari, usioweza kupimwa wala kuhesabiwa; tena itakuwa, badala ya kuambiwa, Ninyi si watu wangu, wataambiwa, Ninyi ndio wana wa Mungu aliye hai.
2 Corinthiens 6.18 Galates 4.6-4.7 Esaïe 66.20 Romains 9.25-9.28 Genèse 13.16
11 Na wana wa Yuda na wana wa Israeli watakusanyika pamoja, nao watajiwekea kichwa kimoja, nao watakwea watoke katika nchi hii; kwa maana siku ya Yezreeli itakuwa kuu sana.
Esaïe 11.12-11.13 Osée 3.5 Jérémie 50.4-50.5 Ezéchiel 37.16-37.25 Jérémie 23.5-23.8

Cette Bible est dans le domaine public.