Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Daniel 7.17
Bible en Swahili de l’est


Visions de Daniel

Vision des quatre bêtes

1 Katika mwaka wa kwanza wa Belshaza, mfalme wa Babeli, Danielii aliona ndoto, na maono ya kichwa chake, kitandani mwake; basi akaiandika ndoto, akatoa habari ya jumla ya mambo hayo.
Daniel 4.5 Daniel 5.1 Daniel 7.15 Amos 3.7 Job 33.14-33.16
2 Danielii akanena, akisema, Naliona katika maono yangu wakati wa usiku; na tazama, hizo pepo nne za mbinguni zilivuma kwa nguvu juu ya bahari kubwa.
Apocalypse 7.1 Apocalypse 17.15
3 Ndipo wanyama wakubwa wanne wakatoka baharini, wote wa namna mbalimbali.
Apocalypse 13.1 Daniel 7.17 Ezéchiel 19.3-19.8 Zacharie 6.1-6.8 Psaumes 76.4
4 Wa kwanza alikuwa kama simba, naye alikuwa na mabawa ya tai; nikatazama, hata mabawa yake yakafutuka manyoya, akainuliwa katika nchi, akasimamishwa juu kwa miguu miwili kama mwanadamu; naye akapewa moyo wa kibinadamu.
Jérémie 4.7 Ezéchiel 17.3 Esaïe 14.13-14.17 Daniel 4.36 Esaïe 5.28-5.29
5 Na tazama, mnyama mwingine, wa pili, kama dubu, naye aliinuliwa upande mmoja, na mifupa mitatu ya mbavu ilikuwamo kinywani mwake katika meno yake; wakamwambia mnyama huyo hivi, Inuka, ule nyama tele.
Daniel 2.39 Osée 13.8 Jérémie 50.21-50.32 Ezéchiel 39.17-39.20 Esaïe 56.9
6 Kisha nikatazama, na kumbe! Mnyama mwingine, kama chui, naye juu ya mgongo wake alikuwa na mabawa manne kama ya ndege; mnyama huyo alikuwa na vichwa vinne; akapewa mamlaka.
Apocalypse 13.2 Daniel 2.39 Daniel 10.20 Daniel 8.5-8.8 Daniel 7.4
7 Baadaye nikaona katika njozi ya usiku, na tazama, mnyama wa nne, mwenye kutisha, mwenye nguvu, mwenye uwezo mwingi, naye alikuwa na meno ya chuma, makubwa sana; alikula na kuvunja vipande vipande, na kuyakanyaga mabaki kwa miguu yake; na umbo lake lilikuwa mbali kabisa na wale wa kwanza, naye alikuwa na pembe kumi.
Apocalypse 13.1 Apocalypse 12.3 Daniel 7.23-7.24 Apocalypse 17.12 Daniel 7.19-7.20
8 Nikaziangalia sana pembe zake, na tazama, pembe nyingine ikazuka kati yao, nayo ilikuwa ndogo, ambayo mbele yake pembe tatu katika zile za kwanza zikang’olewa kabisa; na tazama, katika pembe hiyo mlikuwa na macho kama macho ya mwanadamu, na kinywa kilichokuwa kikinena maneno makuu.
Apocalypse 13.5-13.6 Psaumes 12.3 Daniel 8.9-8.12 Apocalypse 13.1 Apocalypse 9.7
9 Nikatazama hata viti vya enzi vikawekwa, na mmoja aliye mzee wa siku ameketi; mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji, na nywele za kichwa chake kama sufu safi; kiti chake cha enzi kilikuwa miali ya moto, na gurudumu zake moto uwakao.
Apocalypse 1.14 Marc 9.3 Psaumes 90.2 Matthieu 17.2 Michée 5.2
10 Mto kama wa moto ukatoka ukapita mbele zake; maelfu elfu wakamtumikia, na elfu kumi mara elfu kumi wakasimama mbele zake; hukumu ikawekwa, na vitabu vikafunuliwa.
Esaïe 30.27 Apocalypse 5.11 Apocalypse 20.11-20.15 Psaumes 50.3 Psaumes 68.17
11 Nikatazama wakati huo; kwa sababu ya sauti ya yale maneno makubwa iliyoyasema ile pembe; nalitazama hata mnyama yule akauawa, mwili wake ukaharibiwa, akatolewa ateketezwe kwa moto.
Apocalypse 19.20 Apocalypse 20.10 Daniel 7.8 2 Thessaloniciens 2.8 Apocalypse 20.12
12 Na kwa habari za wale wanyama wengine, walinyang’anywa mamlaka yao; walakini maisha yao yalidumishwa kwa wakati na majira.
Daniel 8.7 Daniel 7.4-7.6
13 Nikaona katika njozi za usiku, na tazama, mmoja aliye mfano wa mwanadamu akaja pamoja na mawingu ya mbingu akamkaribia huyo mzee wa siku, wakamleta karibu naye.
Matthieu 26.64 Apocalypse 1.7 Apocalypse 1.13 Matthieu 24.30 Apocalypse 14.14
14 Naye akapewa mamlaka, na utukufu, na ufalme, ili watu wa kabila zote, na taifa zote, na lugha zote, wamtumikie; mamlaka yake ni mamlaka ya milele, ambayo hayatapita kamwe, na ufalme wake ni ufalme usioweza kuangamizwa.
Daniel 7.27 Apocalypse 11.15 Daniel 2.44 Hébreux 12.28 Jean 3.35
15 Basi, mimi Danielii, roho yangu ilihuzunika mwilini mwangu, na hayo maono ya kichwa changu yakanifadhaisha.
Daniel 7.28 Daniel 4.5 Jérémie 17.16 Daniel 8.27 Genèse 40.7-40.8
16 Nikamkaribia mmoja wa hao waliosimama karibu, nikamwuliza maana ya kweli ya hayo yote. Basi akaniambia, akanijulisha tafsiri ya mambo hayo.
Apocalypse 7.13-7.14 Apocalypse 5.5 Daniel 7.10 Daniel 9.22 Daniel 12.5-12.6
17 Wanyama hao wakubwa walio wanne ni wafalme wanne watakaotokea duniani.
Daniel 8.19-8.22 Apocalypse 13.1 Apocalypse 13.11 Psaumes 17.14 Daniel 2.37-2.40
18 Lakini watakatifu wake Aliye juu wataupokea ufalme, na kuumiliki huo ufalme milele, naam hata milele na milele.
Apocalypse 20.4 Apocalypse 2.26-2.27 Psaumes 149.5-149.9 Daniel 7.27 Esaïe 60.12-60.14
19 Kisha nalitaka kujua maana ya yule mnyama wa nne, aliyekuwa mbali na wenziwe wote, mwenye kutisha sana, ambaye meno yake yalikuwa ya chuma, na makucha yake ya shaba; aliyekula, na kuvunja vipande vipande, na kuyakanyaga mabaki kwa miguu yake;
Daniel 7.7 Daniel 2.40-2.43
20 na habari za zile pembe kumi zilizokuwa kichwani mwake, na ile pembe nyingine iliyozuka, ambayo mbele yake zilianguka pembe tatu; yaani, pembe ile yenye macho, na kanwa lililonena makuu, ambayo kuonekana kwake kulikuwa hodari kuliko wenzake.
Daniel 7.8 Daniel 11.36-11.37 Daniel 7.23 Daniel 7.11 Daniel 8.9-8.11
21 Nikatazama, na pembe iyo hiyo ilifanya vita na watakatifu, ikawashinda;
Daniel 12.7 Daniel 8.24 Apocalypse 17.14 Apocalypse 13.5-13.18 Apocalypse 17.6
22 hata akaja huyo mzee wa siku, nao watakatifu wake Aliye juu wakapewa hukumu; na majira yakawadia watakatifu waumiliki ufalme.
Daniel 7.18 Apocalypse 20.4 Apocalypse 11.11-11.18 Apocalypse 19.11-19.21 Apocalypse 14.8-14.20
23 Akanena hivi, Huyo mnyama wa nne atakuwa ni ufalme wa nne juu ya dunia, utakaokuwa mbali na falme zile zote, nao utakula dunia yote, na kuikanyaga, na kuivunja vipande vipande.
Daniel 2.40 Luc 2.1 Daniel 7.7
24 Na habari za zile pembe kumi, katika ufalme huo wataondoka wafalme kumi; na mwingine ataondoka baada ya hao; naye atakuwa mbali na hao wa kwanza; naye atawashusha wafalme watatu.
Daniel 7.20 Apocalypse 13.1 Apocalypse 17.16-17.18 Apocalypse 17.12-17.13 Daniel 11.36
25 Naye atanena maneno kinyume chake Aliye juu, naye atawadhoofisha watakatifu wake Aliye juu; naye ataazimu kubadili majira na sheria; nao watatiwa mikononi mwake kwa wakati, na nyakati mbili, na nusu wakati.
Apocalypse 12.14 Daniel 12.7 Daniel 2.21 2 Thessaloniciens 2.4 Apocalypse 11.2-11.3
26 Lakini hukumu itawekwa, nao watamwondolea mamlaka yake, kuipoteza na kuiangamiza, hata milele.
Apocalypse 11.13 Daniel 7.10-7.11 Daniel 7.22 Apocalypse 20.10-20.11 2 Thessaloniciens 2.8
27 Na ufalme, na mamlaka, na ukuu wa ufalme, chini ya mbingu zote, watapewa watu wa watakatifu wake Aliye juu; ufalme wake ni ufalme wa milele, na wote wenye mamlaka watamtumikia na kumtii.
Daniel 2.44 Psaumes 72.11 Luc 1.33 Psaumes 22.27 Psaumes 86.9
28 Huu ndio mwisho wa jambo lile. Nami, Danielii, fikira zangu zilinifadhaisha, na uso wangu ulinibadilika; lakini naliliweka jambo hilo moyoni mwangu.
Luc 2.51 Luc 2.19 Daniel 8.27 Daniel 4.19 Daniel 10.8

Cette Bible est dans le domaine public.