Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 29.7
Bible en Swahili de l’est


Sur l’Égypte et le pharaon

1 Katika mwaka wa kumi, mwezi wa kumi, siku ya kumi na mbili ya mwezi, neno la Bwana likanijia, kusema,
Ezéchiel 26.1 Ezéchiel 29.17 Ezéchiel 20.1 Ezéchiel 8.1 Ezéchiel 40.1
2 Mwanadamu, elekeza uso wako juu ya Farao, mfalme wa Misri, ukatabiri juu yake, na juu ya Misri yote;
Ezéchiel 6.2 Jérémie 46.2-46.16 Jérémie 44.30 Jérémie 43.8-43.13 Esaïe 18.1-19.17
3 nena, useme, Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, mimi ni juu yako, Ewe Farao, mfalme wa Misri, joka kubwa aoteaye kati ya mito yake, aliyesema, Mto wangu ni wangu mwenyewe, nami nimeufanya kwa ajili ya nafsi yangu.
Esaïe 27.1 Ezéchiel 32.2 Psaumes 74.13-74.14 Jérémie 44.30 Esaïe 51.9
4 Nami nitatia kulabu katika taya zako, nami nitawashikamanisha samaki wa mito yako na magamba yako; nami nitakutoa katika mito yako, pamoja na samaki wa mito yako walioshikamana na magamba yako.
2 Rois 19.28 Ezéchiel 38.4 Amos 4.2 Job 41.1-41.2 Habakuk 1.14-1.15
5 Nami nitakuacha hali umetupwa jangwani, wewe na samaki wote wa mito yako; utaanguka juu ya uso wa uwanda; hutakusanywa, wala kuwekwa pamoja; nimekutoa uwe chakula cha wanyama wa nchi, na cha ndege wa angani.
Jérémie 8.2 Ezéchiel 32.4-32.6 Jérémie 34.20 Jérémie 7.33 Jérémie 25.33
6 Na watu wote wakaao Misri watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, kwa sababu wamekuwa mwanzi wa kutegemewa kwa nyumba ya Israeli.
2 Rois 18.21 Esaïe 36.6 Esaïe 30.2-30.7 Exode 9.14 Lamentations 4.17
7 Walipokushika kwa mkono wako, ulivunjika, ukawararua mabega yao yote; nao walipokutegemea, ulivunjika, ukawatetemesha viuno vyao vyote.
Ezéchiel 17.15-17.17 Psaumes 118.8-118.9 Proverbes 25.19 Jérémie 37.5-37.11 Psaumes 146.3-146.4
8 Basi, Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, nitaleta upanga juu yako, nami nitakatilia mbali nawe wanadamu na wanyama.
Ezéchiel 14.17 Jérémie 7.20 Ezéchiel 32.10-32.13 Exode 12.12 Jérémie 46.13-46.26
9 Nayo nchi ya Misri itakuwa ukiwa na jangwa; nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana; kwa sababu amesema, Mto huu ni wangu, nami nimeufanya.
Ezéchiel 29.3 Proverbes 18.12 Ezéchiel 29.10-29.12 Proverbes 16.18 Proverbes 29.23
10 Basi, tazama, mimi ni juu yako, na juu ya mito yako, nami nitaifanya nchi ya Misri kuwa jangwa tupu, na ukiwa, toka Migdoli hata Sewene, hata mpaka wa Kushi.
Ezéchiel 30.12 Jérémie 46.14 Jérémie 44.1 Habakuk 3.8 Ezéchiel 30.6-30.9
11 Hautapita kati yake mguu wa mwanadamu, wala hautapita kati yake mguu wa mnyama, wala haitakaliwa na watu, muda wa miaka arobaini.
Ezéchiel 32.13 Jérémie 43.11-43.12 Ezéchiel 31.12 Daniel 9.2 Jérémie 29.10
12 Nami nitaifanya nchi ya Misri kuwa ukiwa, kati ya nchi zilizo ukiwa, na miji yake, kati ya miji iliyoharibika, itakuwa maganjo muda wa miaka arobaini; nami nitawatawanya Wamisri kati ya mataifa, nami nitawatapanya kati ya nchi mbalimbali.
Ezéchiel 30.23 Ezéchiel 30.7 Jérémie 46.19 Jérémie 27.6-27.11 Ezéchiel 30.26
13 Maana Bwana MUNGU asema hivi; Mwisho wa miaka arobaini nitawakusanya Wamisri, na kuwatoa katika hizo kabila za watu, ambazo walitawanyika kati yao;
Jérémie 46.26 Esaïe 19.22
14 nami nitawarejeza Wamisri walio katika hali ya kufungwa, nami nitawarudisha hata nchi ya Pathrosi, hata nchi ya kuzaliwa kwao; na huko watakuwa ufalme duni.
Ezéchiel 30.14 Esaïe 11.11 Jérémie 44.1 Genèse 10.14 1 Chroniques 1.12
15 Utakuwa duni kuliko falme zote; wala hautajiinua tena juu ya mataifa; nami nitawapunguza, ili wasitawale tena juu ya mataifa.
Zacharie 10.11 Ezéchiel 30.13 Ezéchiel 17.6 Ezéchiel 32.2 Ezéchiel 31.2
16 Wala hautakuwa tena tumaini la nyumba ya Israeli, kufanya maovu yakumbukwe, watakapogeuka kuangalia nyuma yao; nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana MUNGU.
Osée 8.13 Jérémie 14.10 Lamentations 4.17 Esaïe 64.9 Ezéchiel 29.6-29.7
17 Ikawa katika mwaka wa ishirini na saba, mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya mwezi, neno la Bwana likanijia, kusema,
Ezéchiel 29.1 Ezéchiel 1.2 Ezéchiel 24.1
18 Mwanadamu, Nebukadreza, mfalme wa Babeli, alilihudumisha jeshi lake huduma kuu juu ya Tiro; kila kichwa kilitiwa upaa, na kila bega liliambuliwa ngozi, lakini alikuwa hana mshahara uliotoka Tiro, wala yeye wala jeshi lake, kwa huduma ile aliyohudumu juu yake.
Jérémie 27.6 Jérémie 25.9 Ezéchiel 26.7-26.12 Jérémie 48.37
19 Basi, Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, nitampa Nebukadreza, mfalme wa Babeli, hiyo nchi ya Misri; naye atawachukua watu wake jamii yote pia, na kutwaa mateka yake, na kutwaa mawindo yake, nayo yatakuwa ndio mshahara wa jeshi lake.
Jérémie 43.10-43.13 Ezéchiel 30.24-30.25 Ezéchiel 30.10-30.12 Ezéchiel 29.8-29.10 Ezéchiel 30.4
20 Nimempa nchi ya Misri kuwa malipo ya huduma aliyohudumu, kwa sababu walifanya kazi kwa ajili yangu; asema Bwana MUNGU.
Esaïe 10.6-10.7 Jérémie 25.9 Esaïe 45.1-45.3 2 Rois 10.30
21 Siku ile nitawachipushia nyumba ya Israeli pembe, nami nitakujalia kufumbua kinywa kati yao; nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.
Ezéchiel 33.22 Psaumes 132.17 Ezéchiel 24.27 Luc 1.69 Amos 3.7-3.8

Cette Bible est dans le domaine public.