Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 9.1
Bible en Swahili de l’est


1 Laiti kichwa changu kingekuwa maji, na macho yangu kuwa chemchemi ya machozi, ili nipate kulia mchana na usiku kwa ajili yao waliouawa wa binti ya watu wangu!
Jérémie 13.17 Esaïe 22.4 Jérémie 6.26 Lamentations 2.11 Jérémie 8.21-8.22
2 Laiti ningekuwa na mahali pa kukaa jangwani, kibanda cha wasafiri; nipate kuwaacha watu wangu, na kuondoka kwao! Maana wao ni wazinzi, wote pia, mkutano wa watu wenye hiana.
Jérémie 23.10 Jérémie 5.7-5.8 Osée 4.2 Jérémie 12.1 Osée 7.4
3 Huupinda ulimi wao, kana kwamba ni upinde, ili kusema uongo; nao wamepata nguvu katika nchi, lakini si katika uaminifu; maana huendelea toka ubaya hata ubaya, wala hawanijui mimi, asema Bwana.
Jérémie 4.22 Jérémie 9.8 Juges 2.10 Romains 3.13 1 Samuel 2.12
4 Jihadharini, kila mtu na jirani yake, wala msimtumaini ndugu awaye yote; maana kila ndugu atachongea, na kila jirani atakwenda huko na huko na kusingizia.
Psaumes 12.2-12.3 Proverbes 26.24-26.25 Lévitique 19.16 Jérémie 6.28 Michée 7.5-7.6
5 Nao watadanganya kila mtu jirani yake, wala hawatasema kweli; wameuzoeza ulimi wao kusema uongo; hujidhoofisha ili kutenda uovu.
Job 15.5 Michée 6.12 Proverbes 4.16 Jérémie 9.8 Psaumes 64.3
6 Makao yako ya katikati ya hadaa; kwa hadaa wanakataa kunijua mimi, asema Bwana.
Proverbes 1.24 Job 21.14-21.15 Jean 3.19-3.20 Jérémie 13.10 Proverbes 1.29
7 Basi, kwa hiyo Bwana wa majeshi asema hivi, Tazama, nitawayeyusha na kuwajaribu; maana nisipotenda hivi, nitende nini kwa ajili ya binti ya watu wangu?
Esaïe 1.25 Malachie 3.3 Jérémie 6.27 Zacharie 13.9 Esaïe 48.10
8 Ulimi wao ni mshale ufishao; husema maneno ya hadaa; mtu mmoja husema maneno ya amani na mwenzake kwa kinywa chake, lakini moyoni mwake humwotea.
Psaumes 28.3 Jérémie 9.3 Psaumes 120.3 Psaumes 57.4 Psaumes 55.21
9 Je! Nisiwapatilize kwa mambo hayo? Asema Bwana; na nafsi yangu je! Nisijilipize kisasi juu ya taifa la namna hii?
Jérémie 5.9 Jérémie 5.29 Esaïe 1.24
10 Kwa milima nitalia na kulalama, Na kwa malisho ya nyikani nitafanya maombolezo; Kwa sababu yameteketea, hata hapana apitaye, Wala hapana awezaye kusikia sauti ya ng’ombe; Ndege wa angani, na wanyama wa mwituni, Wamekimbia, wamekwenda zao.
Jérémie 12.4 Osée 4.3 Ezéchiel 29.11 Jérémie 7.29 Ezéchiel 14.15
11 Nami nitafanya Yerusalemu kuwa magofu, Makao ya mbweha; Nami nitaifanya miji ya Yuda kuwa ukiwa, Isikaliwe na mtu awaye yote.
Esaïe 25.2 Jérémie 51.37 Esaïe 34.13 Esaïe 13.22 Jérémie 10.22
12 Ni nani aliye na hekima, apate kuelewa na haya? Tena ni nani ambaye kinywa cha Bwana kimesema naye, apate kuyatangaza? Nayo ni nini maana yake nchi hii kuharibika, na kuteketea kama nyika, asipite mtu?
Psaumes 107.43 Osée 14.9 Psaumes 107.34 Deutéronome 32.29 Jérémie 16.10-16.13
13 Naye Bwana asema, Ni kwa sababu wameiacha sheria yangu niliyoweka mbele yao, wala hawakuitii sauti yangu, wala kuenenda katika hiyo;
2 Chroniques 7.19 Jérémie 22.9 Psaumes 119.53 Esdras 9.10 Sophonie 3.1-3.6
14 bali wameenenda katika ushupavu wa mioyo yao wenyewe, na kuandamana na Mabaali, kama walivyofundishwa na baba zao.
Jérémie 7.24 1 Pierre 1.18 Romains 1.21-1.24 Jérémie 3.17 Galates 1.14
15 Basi, Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Tazama, nitawalisha pakanga, naam, watu hawa, nami nitawapa maji ya uchungu wayanywe.
Jérémie 8.14 Lamentations 3.15 Psaumes 80.5 Jérémie 23.15 Deutéronome 29.18
16 Nami nitawatawanya kati ya mataifa, ambao wao hawakuwajua; wala baba zao, nami nitatuma upanga nyuma yao, hata nitakapowaangamiza kabisa.
Lévitique 26.33 Ezéchiel 5.2 Ezéchiel 5.12 Deutéronome 28.64 Jérémie 44.27
17 Bwana wa majeshi asema hivi, Fikirini ninyi, mkawaite wanawake waombolezao, ili waje; mkatume na kuwaita wanawake wenye ustadi, ili waje;
Ecclésiaste 12.5 2 Chroniques 35.25 Marc 5.38 Job 3.8 Matthieu 9.23
18 na wafanye haraka na kutuombolezea, ili macho yetu yachuruzike machozi, na kope zetu zibubujike maji.
Jérémie 14.17 Jérémie 9.1 Esaïe 22.4 Lamentations 2.18 Lamentations 1.2
19 Maana sauti ya maombolezo imesikiwa toka Sayuni, Jinsi tulivyotekwa! tulivyofadhaika sana! Kwa sababu tumeiacha nchi, kwa kuwa wameangusha makao yetu.
Jérémie 4.13 Deutéronome 28.29 Ezéchiel 7.16-7.18 Lévitique 18.28 Lamentations 4.15
20 Lakini lisikieni neno la Bwana, enyi wanawake, Na masikio yenu yapokee neno la kinywa chake; Mkawafundishe binti zenu kuomboleza, Na kila mmoja jirani yake kulia.
Esaïe 32.9-32.13 Job 22.22 Luc 23.27-23.30 Jérémie 9.17-9.18 Esaïe 3.16
21 Kwa maana mauti imepandia madirishani mwetu, imeingia majumbani mwetu; Ipate kuwakatilia mbali watoto walio nje, na vijana katika njia kuu.
Jérémie 15.7 2 Chroniques 36.17 Jérémie 6.11 Amos 6.10-6.11 Ezéchiel 9.5-9.6
22 Nena, Bwana asema hivi, Mizoga ya watu itaanguka kama samadi juu ya mashamba, Na kama konzi ya ngano nyuma yake avunaye, wala hapana mtu atakayeikusanya.
Jérémie 8.2 Esaïe 5.25 Jérémie 25.33 Psaumes 83.10 Jérémie 16.4
23 Bwana asema hivi, Mwenye hekima asijisifu kwa sababu ya hekima yake, wala mwenye nguvu asijisifu kwa sababu ya nguvu zake, wala tajiri asijisifu kwa sababu ya utajiri wake;
Ecclésiaste 9.11 1 Corinthiens 1.27-1.29 Job 31.24-31.25 Marc 10.24 1 Corinthiens 3.18-3.20
24 bali ajisifuye na ajisifu kwa sababu hii, ya kwamba ananifahamu mimi, na kunijua, ya kuwa mimi ni Bwana, nitendaye wema, na hukumu, na haki, katika nchi; maana mimi napendezwa na mambo hayo, asema Bwana,
1 Corinthiens 1.31 Michée 7.18 2 Corinthiens 10.17 Galates 6.14 1 Jean 5.20
25 Tazama, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapowaadhibu wote waliotahiriwa katika hali yao ya kutokutahiriwa;
Romains 2.8-2.9 Ezéchiel 28.10 Romains 2.25-2.26 Amos 3.2 Galates 5.2-5.6
26 Misri, na Yuda, na Edomu, na wana wa Amoni, na Moabu, na wote wenye kunyoa denge, wakaao nyikani; maana mataifa hayo yote hawana tohara, wala nyumba yote ya Israeli hawakutahiriwa mioyo yao.
Lévitique 26.41 Jérémie 4.4 Ezéchiel 44.7 Jérémie 49.32 Romains 2.28-2.29

Cette Bible est dans le domaine public.