Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 7.18
Bible en Swahili de l’est


Reproches et menaces

1 Neno hili ndilo lililomjia Yeremia, kutoka kwa Bwana, kusema,
2 Simama langoni pa nyumba ya Bwana, ukatangaze hapo neno hili, ukisema, Sikilizeni neno la Bwana, ninyi nyote wa Yuda, mnaoingia katika malango haya ili kumwabudu Bwana.
Jérémie 26.2 Apocalypse 2.11 Apocalypse 2.29 Jérémie 22.1-22.2 Michée 1.2
3 Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Tengenezeni njia zenu, na matendo yenu, nami nitawakalisha ninyi mahali hapa.
Jérémie 18.11 Jérémie 26.13 Matthieu 3.8-3.10 Jérémie 35.15 Ezéchiel 33.4-33.11
4 Msitumainie maneno ya uongo, mkisema, Hekalu la Bwana, Hekalu la Bwana, Hekalu la Bwana ndiyo haya.
Michée 3.11 Ezéchiel 13.19 Jérémie 6.14 Jérémie 28.15 Jérémie 29.23
5 Maana kama mkitengeneza kabisa njia zenu na matendo yenu; kama mkihukumu hukumu ya haki kati ya mtu na jirani yake;
1 Rois 6.12-6.13 Jérémie 4.1-4.2 Jérémie 22.3 Esaïe 1.19 Juges 5.1
6 kama hamwonei mgeni, wala yatima, wala mjane, wala kumwaga damu isiyo na hatia mahali hapa, wala kuifuata miungu mingine kwa hasara yenu wenyewe;
Deutéronome 8.19 Jérémie 13.10 Jérémie 2.34 Exode 22.21-22.24 Deutéronome 6.14-6.15
7 ndipo nitakapowakalisha mahali hapa, katika nchi hii niliyowapa baba zenu, tokea zamani hata milele.
Deutéronome 4.40 Jérémie 3.18 Jérémie 25.5 Jérémie 18.7-18.8 Jérémie 17.20-17.27
8 Angalieni, mnatumainia maneno ya uongo, yasiyoweza kufaidia.
Jérémie 7.4 Esaïe 28.15 Jérémie 23.26 Jérémie 14.13-14.14 Jérémie 8.10
9 Je! Mtaiba, na kuua, na kuzini, na kuapa kwa uongo, na kumfukizia Baali uvumba, na kuifuata miungu mingine ambayo hamkuijua;
Jérémie 7.6 Exode 20.3 Jérémie 11.17 Jérémie 11.13 Jacques 4.1-4.4
10 kisha mtakuja na kusimama mbele zangu katika nyumba hii, iitwayo kwa jina langu, na kusema, Tumepona; ili mpate kufanya machukizo hayo yote?
Jérémie 32.34 Ezéchiel 23.39 Jérémie 7.30 Jérémie 7.14 Jérémie 7.11
11 Je! Nyumba hii, iitwayo kwa jina langu, imekuwa pango la wanyang’anyi machoni penu? Angalieni, mimi, naam, mimi, nimeliona jambo hili, asema Bwana.
Matthieu 21.13 Esaïe 56.7 Marc 11.17 Jérémie 16.16-16.17 Hébreux 4.13
12 Lakini enendeni sasa hata mahali pangu palipokuwapo katika Shilo, nilipolikalisha jina langu hapo kwanza, mkaone nilivyopatenda kwa sababu ya uovu wa watu wangu Israeli.
1 Samuel 4.10-4.11 Psaumes 78.60-78.64 Juges 18.31 1 Samuel 4.22 Josué 18.1
13 Na sasa, kwa sababu mmezifanya kazi hizi zote asema Bwana, nami nikasema nanyi, nikiamka mapema na kunena, lakini hamkusikia; nami nikawaita wala hamkuniitikia;
Esaïe 65.12 Jérémie 7.25 Proverbes 1.24 2 Chroniques 36.15-36.16 Jérémie 35.15
14 basi, nitaitenda nyumba hii, iitwayo kwa jina langu, mnayoitumainia, na mahali hapa nilipowapa ninyi na baba zenu, kama nilivyopatenda Shilo.
Jérémie 7.4 2 Rois 25.9 Deutéronome 28.52 Jérémie 7.10 Jérémie 26.6-26.9
15 Nami nitawatupa ninyi mbali na macho yangu, kama nilivyowatupa ndugu zenu wote, yaani, wazao wote wa Efraimu.
Jérémie 15.1 2 Rois 17.23 Jérémie 52.3 Jérémie 3.8 2 Chroniques 15.9
16 Basi, wewe usiwaombee watu hawa, wala usiwapazie sauti yako, wala kuwaombea dua, wala usinisihi kwa ajili yao; kwa maana sitakusikiliza.
Exode 32.10 Jérémie 11.14 Jérémie 15.1 Deutéronome 9.14 1 Jean 5.16
17 Je! Huoni wanavyotenda katika miji ya Yuda, na katika njia kuu za Yerusalemu?
Ezéchiel 14.23 Ezéchiel 8.6-8.18 Jérémie 6.27
18 Watoto huokota kuni, na baba zao huwasha moto, na wanawake hukanda unga, ili kumfanyizia mikate malkia wa mbinguni, na kuwamiminia miungu mingine sadaka za kinywaji, wapate kunikasirisha mimi.
Jérémie 19.13 Jérémie 44.17-44.19 1 Rois 14.9 Ezéchiel 20.28 Deutéronome 32.37-32.38
19 Je! Watu hawa wanikasirisha mimi? Asema Bwana; hawajikasirishi nafsi zao, na kuzitia haya nyuso zao wenyewe?
1 Corinthiens 10.22 Jérémie 20.11 Esaïe 1.20 Esdras 9.7 Esaïe 1.24
20 Kwa hiyo, Bwana MUNGU asema hivi, Tazama, hasira yangu na ghadhabu yangu zitamwagwa juu ya mahali hapa, juu ya wanadamu, na juu ya wanyama, na juu ya miti ya mashamba, na juu ya mazao ya nchi; nayo itateketea, isizimike.
Jérémie 42.18 Lamentations 2.3-2.5 Lamentations 4.11 Esaïe 42.25 Jérémie 44.6
21 Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Tieni sadaka zenu za kuteketezwa pamoja na dhabihu zenu, mkale nyama.
Osée 8.13 Jérémie 6.20 Esaïe 1.11-1.15 Amos 5.21-5.23
22 Maana sikusema na baba zenu, wala sikuwaamuru kwa habari za sadaka za kuteketezwa na dhabihu, siku ile nilipowatoa katika nchi ya Misri;
Osée 6.6 1 Samuel 15.22 Psaumes 40.6 Marc 12.33 Psaumes 50.8-50.17
23 lakini naliwaamuru neno hili, nikisema, Sikilizeni sauti yangu, nami nitakuwa Mungu wenu nanyi mtakuwa watu wangu; mkaende katika njia ile yote nitakayowaamuru mpate kufanikiwa.
Exode 15.26 Deutéronome 5.33 Deutéronome 6.3 Jérémie 42.6 Jérémie 11.4
24 Lakini hawakusikiliza, wala kutega sikio lao, bali walikwenda kwa mashauri yao wenyewe, na kwa ushupavu wa mioyo yao mibaya, wakaenda nyuma wala si mbele.
Deutéronome 29.19 Jérémie 7.26 Psaumes 81.11-81.12 Ezéchiel 20.13 Jérémie 8.5
25 Tokea siku ile baba zenu walipotoka katika nchi ya Misri hata leo, nimewatuma watumishi wangu wote manabii kwenu ninyi, nikiamka mapema kila siku, na kuwatuma.
Jérémie 25.4 2 Chroniques 36.15 Ezéchiel 2.3 Jérémie 7.13 Esdras 9.7
26 Lakini hawakunisikiliza, wala kutega sikio lao; bali walifanya shingo yao kuwa ngumu; walitenda mabaya kuliko baba zao.
Jérémie 16.12 2 Chroniques 30.8 Jérémie 19.15 Matthieu 23.32 Jérémie 7.24
27 Nawe utawaambia maneno hayo yote; lakini hawatakusikiliza, nawe utawaita; lakini hawatakuitikia.
Jérémie 26.2 Esaïe 50.2 Zacharie 7.13 Esaïe 65.12 Jérémie 1.7
28 Nawe utawaambia, Taifa hili ndilo lisilosikiliza sauti ya Bwana, Mungu wao, wala kupokea mafundisho; uaminifu umepotea, umekatiliwa mbali na vinywa vyao.
Esaïe 59.14-59.15 Michée 7.2-7.5 Proverbes 1.7 Jérémie 32.33 Jérémie 5.3
29 Zikate nywele zako, Ee Yerusalemu, uzitupe, Ukafanye maombolezo juu ya vilele vya milima; Kwa maana Bwana amekikataa na kukitupa Kizazi cha ghadhabu yake.
Job 1.20 Jérémie 6.30 Michée 1.16 Jérémie 16.6 Esaïe 15.2-15.3
30 Maana wana wa Yuda wametenda yaliyo maovu machoni pangu, asema Bwana; wameweka machukizo yao ndani ya nyumba hiyo, iitwayo kwa jina langu, hata kuitia unajisi.
Ezéchiel 7.20 Jérémie 32.34 Daniel 9.27 2 Chroniques 33.7 2 Chroniques 33.4-33.5
31 Nao wamepajenga mahali palipoinuka pa Tofethi, palipo katika bonde la mwana wa Hinomu, ili kuwateketeza wana wao na binti zao motoni; jambo ambalo mimi sikuliagiza, wala halikuingia moyoni mwangu.
2 Rois 23.10 Deutéronome 17.3 2 Rois 17.17 Jérémie 32.35 Lévitique 18.21
32 Basi angalieni, siku zinakuja, asema Bwana, ambazo katika siku hizo halitaitwa tena Tofethi, wala Bonde la mwana wa Hinomu bali litaitwa, Bonde la Machinjo; maana watazika watu katika Tofethi, hata hapatakuwapo mahali pa kuzika tena.
Jérémie 19.6 Jérémie 19.11 2 Rois 23.10 Ezéchiel 6.5-6.7 Jérémie 7.31
33 Na mizoga ya watu hawa itakuwa chakula cha ndege wa angani, na cha wanyama wa nchi; wala hapana mtu atakayewafukuza.
Deutéronome 28.26 Jérémie 12.9 Jérémie 16.4 Jérémie 34.20 Apocalypse 19.17-19.18
34 Ndipo katika miji ya Yuda, na katika njia kuu za Yerusalemu, nitaikomesha sauti ya kicheko na sauti ya furaha, sauti ya bwana arusi na sauti ya bibi arusi; kwa maana nchi hiyo itakuwa ukiwa.
Ezéchiel 26.13 Apocalypse 18.23 Osée 2.11 Esaïe 24.7-24.8 Jérémie 16.9

Cette Bible est dans le domaine public.