Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 31.35
Bible en Swahili de l’est


1 Wakati huo, asema Bwana, nitakuwa Mungu wa jamaa zote za Israeli, nao watakuwa watu wangu.
Jérémie 30.22 Esaïe 41.10 Zacharie 13.9 Genèse 17.7-17.8 Jérémie 30.24
2 Bwana asema hivi, Watu wale walioachwa na upanga walipata neema jangwani; yaani, Israeli, hapo nilipokwenda kumstarehesha.
Psaumes 95.11 Nombres 10.33 Deutéronome 1.33 Exode 15.9-15.10 Deutéronome 8.16
3 Bwana alinitokea zamani, akisema, Naam nimekupenda kwa upendo wa milele, ndiyo maana nimekuvuta kwa fadhili zangu.
Osée 11.4 Esaïe 54.8-54.9 Deutéronome 33.3 Deutéronome 7.7-7.9 Malachie 1.2
4 Mara ya pili nitakujenga, nawe utajengwa, Ee bikira wa Israeli mara ya pili utapambwa kwa matari yako, nawe utatokea katika michezo yao wanaofurahi.
Jérémie 33.7 Jérémie 31.13 Juges 11.34 Psaumes 149.3 Psaumes 51.18
5 Mara ya pili utapanda mizabibu juu ya milima ya Samaria; wapanzi watapanda, nao watayafurahia matunda yake.
Amos 9.14 Deutéronome 28.30 Zacharie 3.10 1 Samuel 21.5 Ezéchiel 36.8
6 Maana kutakuwa siku moja, ambayo walinzi watalia juu ya vilima vya Efraimu, Inukeni, tukaende Sayuni, kwa Bwana, Mungu wetu.
Jérémie 50.4-50.5 Jérémie 6.17 Actes 8.5-8.8 Osée 1.11 Ezéchiel 33.2
7 Maana Bwana asema hivi, Mwimbieni Yakobo kwa furaha, mkampigie kelele mkuu wa mataifa, tangazeni, sifuni, mkaseme, Ee Bwana, uwaokoe watu wako, mabaki ya Israeli.
Psaumes 14.7 Psaumes 28.9 Esaïe 37.31 Jérémie 23.3 Michée 2.12
8 Tazama, nitawaleta toka nchi ya kaskazini, na kuwakusanya katika miisho ya dunia, na pamoja nao watakuja walio vipofu, na hao wachechemeao, mwanamke mwenye mimba, na yeye pia aliye na utungu wa kuzaa; watarudi huko, jeshi kubwa.
Michée 4.6 Jérémie 23.8 Ezéchiel 34.16 Esaïe 42.16 Ezéchiel 34.13
9 Watakuja kwa kulia, na kwa maombi nitawaongoza; nitawaendesha penye mito ya maji, katika njia iliyonyoka; katika njia hiyo hawatajikwaa; maana mimi ni baba wa Israeli, na Efraimu ni mzaliwa wa kwanza wangu.
Jérémie 3.4 Exode 4.22 Jérémie 50.4 Jérémie 31.20 Esaïe 63.13
10 Lisikieni neno la Bwana, enyi mataifa, litangazeni visiwani mbali; mkaseme, Aliyemtawanya Israeli atamkusanya, na kumlinda, kama mchungaji alindavyo kundi lake.
Esaïe 40.11 Ezéchiel 34.12 Esaïe 66.19 Deutéronome 30.4 Zacharie 9.16
11 Kwa maana Bwana amemweka huru Yakobo, amemkomboa mkononi mwake aliyekuwa hodari kuliko yeye.
Esaïe 48.20 Esaïe 44.23 Psaumes 142.6 Jérémie 15.21 Esaïe 49.24
12 Nao watakuja, na kuimba katika mlima Sayuni, wataukimbilia wema wa Bwana, nafaka, na divai, na mafuta, na wachanga wa kondoo na wa ng’ombe; na roho zao zitakuwa kama bustani iliyotiwa maji; wala hawatahuzunika tena kabisa.
Esaïe 35.10 Esaïe 58.11 Joël 3.18 Jean 16.22 Ezéchiel 17.23
13 Ndipo bikira atafurahi katika kucheza, na vijana na wazee pamoja; maana nitageuza masikitiko yao kuwa furaha, nami nitawafariji, na kuwafurahisha waache huzuni zao.
Psaumes 30.11 Esaïe 51.11 Esaïe 61.3 Jérémie 31.4 Psaumes 149.3
14 Nami nitaishibisha roho ya makuhani kwa unono, na watu wangu watashiba kwa wema wangu, asema Bwana
Jérémie 31.25 Jérémie 33.9 Apocalypse 5.10 Ephésiens 3.19 Esaïe 61.6
15 Bwana asema hivi, Sauti imesikiwa Rama, kilio, na maombolezo mengi, Raheli akiwalilia watoto wake; asikubali kufarijiwa kwa watoto wake, kwa kuwa hawako,
Jérémie 40.1 Jérémie 10.20 Genèse 42.13 Genèse 37.35 Josué 18.25
16 Bwana asema hivi, Zuia sauti yako, usilie, na macho yako yasitoke machozi; Maana kazi yako itapata thawabu, nao watakuja tena toka nchi ya adui; Ndivyo asemavyo Bwana.
Jérémie 30.3 Ruth 2.12 Hébreux 6.10 Jérémie 30.18 Jérémie 29.14
17 Tena liko tumaini kwa siku zako za mwisho, asema Bwana; na watoto wako watarejea hata mpaka wao wenyewe.
Lamentations 3.21 Jérémie 29.11-29.16 Lamentations 3.18 Psaumes 102.13-102.14 Lamentations 3.26
18 Hakika nimemsikia Efraimu, akijililia hivi, Umeniadhibu, nami nikaadhibika, kama ndama asiyeizoelea nira; unigeuze, nami nitageuzwa; kwa maana wewe u Bwana, Mungu wangu.
Psaumes 80.3 Jérémie 31.9 Job 5.17 Lamentations 5.21 Jérémie 3.21-3.22
19 Hakika baada ya kugeuzwa kwangu, nalitubu; na baada ya kufundishwa kwangu, nalijipiga pajani; nalitahayarika, naam, nalifadhaika, kwa sababu naliichukua aibu ya ujana wangu.
Ezéchiel 36.31 Jérémie 3.25 Ezéchiel 21.12 Luc 18.13 Zacharie 12.10
20 Je! Efraimu siye mwanangu mpendwa? Je! Siye mtoto apendezaye? Maana kila nisemapo neno juu yake, ningali nikimkumbuka sana; kwa sababu hiyo moyo wangu unataabika kwa ajili yake; bila shaka nitamrehemu, asema Bwana.
Esaïe 55.7 Esaïe 63.15 Cantique 5.4 Juges 10.16 Esaïe 16.11
21 Jiwekee alama za njia; jifanyie miti ya kukuongoza; uuelekeze moyo wako kwenye njia kuu, njia ile ile uliyoiendea; rudi tena, Ee bikira wa Israeli, irudie hii miji yako.
Jérémie 50.5 Esaïe 48.20 Jérémie 31.4 Jérémie 3.14 Esaïe 62.10
22 Hata lini utatanga-tanga, Ee binti mwenye kuasi? Kwa maana Bwana ameumba jambo jipya duniani; mwanamke atamlinda mwanamume.
Jérémie 49.4 Jérémie 2.23 Jérémie 3.6 Genèse 3.15 Esaïe 7.14
23 Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Watatumia tena neno hili katika nchi ya Yuda, na katika miji yake, nitakapowarudisha mateka yao; Bwana na akubariki, Ee kao la haki, Ee mlima wa utakatifu.
Zacharie 8.3 Esaïe 1.26 Jérémie 50.7 Jérémie 33.15-33.26 Ruth 2.4
24 Na Yuda, na miji yake yote, watakaa humo pamoja; wakulima, nao waendao huko na huko pamoja na makundi yao.
Zacharie 8.4-8.8 Ezéchiel 36.10 Zacharie 2.4 Jérémie 33.11-33.13
25 Kwa maana nimeishibisha roho yenye uchovu, nami nimeiridhisha kila roho yenye huzuni.
Psaumes 107.9 Jean 4.14 Matthieu 5.6 Jérémie 31.14 Matthieu 11.28
26 Basi, nikaamka, nikaangalia; na usingizi wangu ulikuwa mtamu kwangu.
Psaumes 127.2 Zacharie 4.1-4.2
27 Tazama, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapoipanda nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda, mbegu ya mwanadamu na mbegu ya mnyama.
Osée 2.23 Ezéchiel 36.9 Ezéchiel 36.11 Zacharie 10.9 Jérémie 30.19
28 Tena itakuwa, kwa kadiri nilivyowaangalia, ili kung’oa, na kubomoa, na kuangusha, na kuangamiza, na kutesa; kwa kadiri iyo hiyo nitawaangalia, ili kujenga, na kupanda, asema Bwana.
Jérémie 1.10 Jérémie 44.27 Jérémie 24.6 Jérémie 45.4 Daniel 9.14
29 Siku zile, hawatasema tena, Baba za watu wamekula zabibu kali, na meno ya watoto wao yametiwa ganzi.
Lamentations 5.7 Ezéchiel 18.2-18.3 Jérémie 31.30
30 Bali kila mtu atakufa kwa sababu ya uovu wake mwenyewe; kila mtu alaye zabibu kali, meno yake yatatiwa ganzi.
Ezéchiel 18.20 Esaïe 3.11 Deutéronome 24.16 Galates 6.5 Ezéchiel 18.4
31 Angalia, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapofanya agano jipya na nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda.
Ezéchiel 37.26 Hébreux 10.16-10.17 Jérémie 32.40 Luc 22.20 2 Corinthiens 3.6
32 Si kwa mfano wa agano lile nililolifanya na baba zao, katika siku ile nilipowashika mkono, ili kuwatoa katika nchi ya Misri; ambalo agano langu hilo walilivunja, ingawa nalikuwa mume kwao, asema Bwana.
Ezéchiel 16.8 Deutéronome 1.31 Deutéronome 5.3 Exode 19.5 Exode 24.6-24.8
33 Bali agano hili ndilo nitakalofanya na nyumba ya Israeli, baada ya siku zile, asema Bwana; Nitatia sheria yangu ndani yao, na katika mioyo yao nitaiandika; nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.
2 Corinthiens 3.3 Hébreux 10.16 Jérémie 24.7 Hébreux 8.10 Ezéchiel 11.19-11.20
34 Wala hawatamfundisha kila mtu jirani yake, na kila mtu ndugu yake, wakisema, Mjue Bwana; kwa maana watanijua wote, tangu mtu aliye mdogo miongoni mwao hata aliye mkubwa miongoni mwao, asema Bwana; maana nitausamehe uovu wao, wala dhambi yao sitaikumbuka tena.
Esaïe 43.25 Esaïe 54.13 Jérémie 33.8 Jérémie 50.20 Michée 7.18
35 Bwana asema hivi, awapaye watu jua, ili kuwa nuru wakati wa mchana, na amri za mwezi na nyota, ili kuwa nuru wakati wa usiku, aichafuaye bahari, hata mawimbi yake yakavuma; Bwana wa majeshi, ndilo jina lake;
Esaïe 51.15 Jérémie 10.16 Psaumes 136.7-136.9 Jérémie 32.18 Psaumes 19.1-19.6
36 Amri hizi zikiondoka, zisiwe mbele zangu, asema Bwana, ndipo wazao wa Israeli nao wataacha kuwa taifa mbele zangu milele.
Esaïe 54.9-54.10 Jérémie 33.20-33.26 Psaumes 89.36-89.37 Psaumes 148.6 Amos 9.8-9.9
37 Bwana asema hivi, Kama mbingu zikiweza kupimwa, na misingi ya dunia ikiweza kugunduliwa huko chini, ndipo wazao wa Israeli pia nitawatupilia mbali, kwa ajili ya hayo yote waliyoyatenda, asema Bwana.
Jérémie 33.24-33.26 Jérémie 33.22 Esaïe 40.12 Romains 11.26-11.29 Jérémie 30.11
38 Tazama, siku zinakuja, asema Bwana, mji huu utakapojengwa kwa ajili ya Bwana, toka buruji ya Hananeli hata lango la pembeni.
2 Rois 14.13 Zacharie 14.10 Jérémie 30.18 Jérémie 31.27 2 Chroniques 26.9
39 Na kamba ya kupimia itaendelea moja kwa moja hata mlima Garebu, tena itazunguka na kufika Goa.
Zacharie 2.1-2.2 Ezéchiel 40.8
40 Na bonde lote la mizoga, na majivu, na mashamba yote mpaka kijito Kidroni, mpaka pembe ya lango la farasi, upande wa mashariki, patakuwa patakatifu kwa Bwana; hapatang’olewa, wala hapatabomolewa, hata milele.
Joël 3.17 2 Samuel 15.23 Jean 18.1 2 Chroniques 23.15 2 Rois 11.16

Cette Bible est dans le domaine public.