Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 17
Bible en Swahili de l’est


Le péché gravé dans le cœur

1 Dhambi ya Yuda imeandikwa kwa kalamu ya chuma, na kwa ncha ya almasi; imechorwa katika kibao cha moyo wao, na katika pembe za madhabahu zenu;
Proverbes 3.3 2 Corinthiens 3.3 Proverbes 7.3 Osée 12.11 Lévitique 4.25
2 na wakati huo watoto wao wazikumbuka madhabahu zao, na maashera yao, karibu na miti yenye majani mabichi juu ya milima mirefu.
2 Chroniques 24.18 Jérémie 2.20 Esaïe 17.8 Esaïe 1.29 Jérémie 7.18
3 Ee mlima wangu wa uwandani, nitatoa mali zako na hazina zako zote ziwe nyara, na mahali pako palipoinuka, kwa sababu ya dhambi, katika mipaka yako yote.
Jérémie 15.13 2 Rois 24.13 Jérémie 26.18 Esaïe 39.4-39.6 Ezéchiel 6.3
4 Nawe, naam, wewe nafsi yako, utaachana na urithi wako niliokupa; nami nitakulazimisha kuwatumikia adui zako katika nchi usiyoijua; maana umewasha moto katika hasira yangu, utakaowaka milele.
Jérémie 15.14 Jérémie 16.13 Jérémie 7.20 Jérémie 27.12-27.13 Esaïe 14.3
5 Bwana asema hivi, Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha Bwana.
Psaumes 118.8-118.9 Psaumes 146.3-146.4 Esaïe 2.22 2 Chroniques 32.8 Esaïe 31.1-31.9
6 Maana atakuwa kama fukara nyikani, Hataona yatakapotokea mema; Bali atakaa jangwani palipo ukame, Katika nchi ya chumvi isiyokaliwa na watu.
Deutéronome 29.23 Jérémie 48.6 Job 39.6 Job 20.17 Ezéchiel 47.11
7 Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea Bwana, Ambaye Bwana ni tumaini lake.
Psaumes 34.8 Proverbes 16.20 Psaumes 40.4 Esaïe 30.18 Psaumes 84.12
8 Maana atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji, Uenezao mizizi yake karibu na mto; Hautaona hofu wakati wa hari ujapo, Bali jani lake litakuwa bichi; Wala hautahangaika mwaka wa uchache wa mvua, Wala hautaacha kuzaa matunda.
Ezéchiel 31.4-31.10 Psaumes 1.3 Esaïe 58.11 Psaumes 92.10-92.15 Ezéchiel 47.12
9 Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua?
Marc 7.21-7.22 Proverbes 28.26 Hébreux 3.12 Ecclésiaste 9.3 Matthieu 15.19
10 Mimi, Bwana, nauchunguza moyo, navijaribu viuno, hata kumpa kila mtu kiasi cha njia zake, kiasi cha matunda ya matendo yake.
Jérémie 32.19 Romains 8.27 Jérémie 11.20 1 Samuel 16.7 Psaumes 62.12
11 Kama kware akusanyaye makinda asiyoyazaa, ndivyo alivyo mtu ajipatiaye mali, wala si kwa haki, katikati ya siku zake zitaachana naye, na mwisho wake atakuwa mpumbavu.
Proverbes 28.8 Luc 12.20 Proverbes 21.6 Proverbes 15.27 Proverbes 28.20
12 Kiti cha enzi, cha utukufu, kilichowekwa juu tangu mwanzo, ndicho mahali patakatifu petu.
Jérémie 3.17 Psaumes 96.6 Jérémie 14.21 Ezéchiel 43.7 Ezéchiel 1.26
13 Ee Bwana, tumaini la Israeli, wote wakuachao watatahayarika. Wao watakaojitenga nami wataandikwa katika mchanga, kwa sababu wamemwacha Bwana, kisima cha maji yaliyo hai.
Esaïe 1.28 Jérémie 14.8 Psaumes 73.27 Jean 8.6-8.8 Luc 10.20
14 Uniponye, Ee Bwana, nami nitaponyeka; uniokoe, nami nitaokoka; kwa maana wewe ndiwe uliye sifa zangu.
Deutéronome 10.21 Psaumes 6.2 Psaumes 109.1 Esaïe 57.18-57.19 Psaumes 6.4
15 Tazama, wao waniambia, Neno la Bwana liko wapi? Na lije, basi.
Esaïe 5.19 2 Pierre 3.3-3.4 Ezéchiel 12.22 Jérémie 20.7-20.8 Ezéchiel 12.27-12.28
16 Mimi hapa sikufanya haraka kuacha kuwa mchungaji nyuma yako; wala sikuitamani siku ya maradhi ya kufisha; wewe unajua; yaliyotoka midomoni mwangu yalikuwa mbele za uso wako.
Jérémie 4.19-4.20 Amos 7.14-7.15 Jérémie 20.9 2 Corinthiens 2.17 Jérémie 14.17-14.21
17 Usiwe sababu ya hofu kuu kwangu mimi; wewe ndiwe uliye kimbilio langu siku ya uovu.
Jérémie 16.19 Nahum 1.7 Psaumes 88.15-88.16 Psaumes 59.16 Job 31.23
18 Na waaibike watu wanaoniudhi, lakini nisiaibike mimi; na waone hofu kuu, lakini mimi nisione hofu kuu; ulete juu yao siku ya uovu; uwaangamize maangamizo maradufu.
Psaumes 35.4 Psaumes 40.14 Psaumes 35.8 Jérémie 11.20 Jérémie 20.11

Le respect du sabbat

19 Bwana akaniambia hivi, Enenda ukasimame katika lango la wana wa watu hawa, waingiapo wafalme wa Yuda, na watokeapo, na katika malango yote ya Yerusalemu,
Jérémie 7.2 Jérémie 26.2 Proverbes 9.3 Proverbes 1.20-1.22 Actes 5.20
20 ukawaambie, Lisikieni neno la Bwana, enyi wafalme wa Yuda, na Yuda wote, nanyi wenyeji wote wa Yerusalemu, ninyi mwingiao kwa malango haya;
Jérémie 19.3 Jérémie 22.2 Psaumes 49.1-49.2 Ezéchiel 2.7 Ezéchiel 3.17
21 Bwana asema hivi, Jihadharini nafsi zenu, msichukue mzigo wo wote siku ya sabato, wala msiulete ndani kwa malango ya Yerusalemu;
Néhémie 13.15-13.21 Nombres 15.32-15.36 Deutéronome 4.15 Jean 5.9-5.12 Marc 4.24
22 wala msitoe mzigo katika nyumba zenu siku ya sabato, wala msifanye kazi yo yote; bali itakaseni siku ya sabato, kama nilivyowaamuru baba zenu;
Ezéchiel 20.12 Esaïe 58.13 Esaïe 56.2-56.6 Exode 20.8-20.10 Deutéronome 5.12-5.15
23 lakini hawakusikiliza, wala hawakutega masikio yao, bali walifanya shingo zao kuwa ngumu, ili wasisikilize wala wasipokee mafundisho.
Jérémie 11.10 Proverbes 29.1 Jérémie 19.15 Actes 7.51 Zacharie 7.11-7.12
24 Na itakuwa, kama mkinisikiliza mimi kwa bidii, asema Bwana, msiingize mzigo wo wote kwa malango ya mji huu siku ya sabato, bali mkiitakasa siku ya sabato, bila kufanya kazi yo yote siku hiyo;
Deutéronome 11.13 Jérémie 17.21-17.22 Exode 15.26 Esaïe 55.2 Esaïe 21.7
25 ndipo watakapoingia wafalme na wakuu kwa malango ya mji huu; wataketi katika kiti cha enzi cha Daudi, na kupanda magari na farasi, wao, na wakuu wao, watu wa Yuda, na wenyeji wa Yerusalemu; na mji huu utakaa hata milele.
Jérémie 22.4 Esaïe 9.7 Jérémie 33.17 2 Samuel 7.16 Jérémie 33.15
26 Nao watatoka miji ya Yuda, na mahali palipo pande zote za Yerusalemu, na nchi ya Benyamini, na Shefela, na milima,na upande wa Negebu,wakileta sadaka za kuteketezwa,na dhabihu,na sadaka za unga,na ubani,wakileta pia sadaka za shukurani,nyumbani kwa BWANA.
Zacharie 7.7 Jérémie 33.13 Jérémie 32.44 Psaumes 107.22 Jérémie 33.11
27 Lakini kama hamtaki kunisikiliza, kuitakasa siku ya sabato, kutokuchukua mzigo na kuingia kwa malango ya Yerusalemu siku ya sabato; basi, nitawasha moto malangoni mwake, nao utaziteketeza nyumba za enzi za Yerusalemu, wala hautazimika.
2 Rois 25.9 Jérémie 7.20 Lamentations 4.11 Jérémie 21.14 Jérémie 17.21-17.22

Cette Bible est dans le domaine public.